Bilionea wa Nigeria amzawadia Tayo $350,000 baada ya kushindwa kuzinyakua $300,000 za BBA Hotshot

Bilionea wa Nigeria amzawadia Tayo $350,000 baada ya kushindwa kuzinyakua $300,000 za BBA Hotshot

dexterous

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
2,037
Reaction score
3,134
Imeripotiwa kuwa baada ya mshiriki wa Nigeria kwenye shindano la Big Brother Afrika, Tayo kuzikosa dola laki tatu za Biggie zilizomwendea Idris wa Tanzania Jumapili iliyopita, mshiriki huyo wa Naija amezawadiwa $350,000 sawa na zaidi ya milioni 600 kutoka kwa shabiki wake bilionea.

Bilionea huyo aitwaye Ayiri Emami ameamua kuongeza dola 50,000 juu zaidi ya ile ambayo ilitolewa na Biggie ambayo ni $300,000 kutokana na kuwa shabiki mkubwa wa Tayo.

Staa wa Nigeria Davido ameshare picha ya story hiyo Instagram na kuandika "we do this easy, bar dey".

Inasemekana hii si mara ya kwanza kwa bilionea huyo kumwaga mkwanja mrefu kwa wasanii anaowapenda, aliwahi kufanya hivyo kwenye harusi ya 2Face 2010 ambapo inasemekana alitoa zaidi ya Naira milioni 20 (sawa na zaidi ya Tsh 189,000,000) na kumzawadia Range Rover mpya, na pia alimzawadia msanii mwingine aitwaye Durella gari aina ya Toyota Prado Jeep.

=======================

Mnigeria Tayo alitoka mikono mitupu #BBAHotshots 2014, Bilionea kampa fungu hili Nigeria

Tayorr.jpg

Mshiriki wa BBA Hotshots 2014 kutoka Nigeria, Tayo Folarin.

Baada ya East Africa yote kuinua shangwe kubwa siku ya Jumapili Desemba 7 kusherehekea ushindi wa nguvu alioupata Mtanzania Idris kwenye BBAHotshots, kulikuwa na story kwenye mitandao ya kijamii ambazo hazikuwapendeza watu wengi kwani ilionekana kama baadhi ya watu kama Nigeria hawakuwa na amani kuukosa ushindi huo na kuuona ukija Tanzania.

Sasa mpya kutoka Nigeria ni kwamba bilionea mmoja hakupendezwa kumuona mwakilishi wao Tayo akiambulia patupu, bilionea huyo Ayiri Emami amempatia Tayo Folarin pesa ambazo ni zaidi hata ya kiwango ambacho kimetolewa na BBAHotshotskwa mshindi wa kwanza.
Tunawafahamu mabilionea wachache kutoka Nigeria wakiongozwa na Aliko Dangote,Emami leo anakaa kwenye headlines karibu zote za Nigeria kwa kumpatia Tayo dola laki tatu na nusu (350,000/=)

AYIRI-EMAMI-3.jpg

Bilionea Ayiri Emami


Kiasi hicho ni backup kwa Tayo ambaye alionekana mnyonge sana usiku ambao Idris alitangazwa mshindi, hii itampa Amani ya kuendelea maisha na mpenzi wake na mtoto wake mmoja ambaye alizaliwa wakati Tayo akiwa ndani ya Jumba la Big Brother.

Chanzo: MillardAyo.com

========

UPDATE: Mshindi wa Pili wa BBA Hotshots 2014: Akanusha kupewa pesa na tajiri wa Nigeria


Mshindi wa pili wa BBA Hotshots, Tayo kutoka Nigeria amekanusha ripoti zilisambaa wiki hii kuwa amezawadiwa $350,000 na bilionea wa Nigeria baada ya kuzikosa $300,000 za BBA zilizonyakuliwa na mshindi wa kwanza mwaka huu Idris wa Tanzania.

Tayo.jpg

Idris (kushoto) Tayo (kulia)

Ripoti hizo zilidai kuwa Tayo alipewa zawadi hiyo na bilionea aitwaye Ayiri Emani kama kifuta jasho au fidia ya kuzikosa $300,000 za mshindi wa HotShots.

Tayo amekanusha habari hizo alipohojiwa na kituo cha Radio 1 South Africa. Amesema kuwa habari hizo za kuwa amepewa kiasi hicho kikubwa cha pesa na huku hata hamfahamu bilionea huyo, zimemletea usumbufu kwasababu watu wengi watadhani yeye ni milionea na huku sio kweli.

Tayo aliongeza kuwa yeye na Idris ni marafiki na anatarajia kuja Tanzania mapema iwezekanavyo.

Chanzo: Big Brother Africa 2014
 
mmmh hii kali....yani hawataki kushindwa.....aya nigeria hongera zenu......
 
Either way...ushindi bado utabaki kwa Idriss tu hata kama angepewa billion 321
 
Ni juzi tu tulishuhudia ushindi wa kijana wetu idris ndani ya jumba la BBA akijinyakulia kitita cha dola 300000 na kuwaacha wenzake patupu hasa mshindi wa pili kutoka Nigeria mr R

Jamaa kahuzunika sana na akawa myonge ile mbaya sasa kilichonifanya nivute huu uzi hapa ni leo hii tajiri mmoja au bilionear wa kineigeria kaamua kumpa mshikaji ali aondokane na unyonge wa kutoka patupu kitita cha dola 350000 ni.zaidi ya kile cha kwenye mjengo hii sijui kama ingekua tz ingekuaje
 
ni kama kushow off,wanasahau ile ni tuzo inaweka historia na heshima tena africa lote.

True...inaonekana imewauma sana kukosa tena mwaka huu, tatizo wanajiona wapo superior sana siku hizi, ila ukweli unabaki palepale na historia tayari ishawekwa
 
Ebwana inaonekana wanaigeria wamekasirika sana huo ushindi wa Idris.
 
Hii ishu inanikumbusha Munya wa Zimbabwe
 
Kaamua kumpa mnajeria mwenzake mkwanja easy like that. .cjui hawataki kushindwa mnayosema nyie..kwani ni mara moja ishu kama izo kutokea...
 
Angempa hata trillion lakini kaweka history tayari kuwa ni mshindi wa Bba hotshosts kimewauma sana watajibeba
 
Wanaigeria kwa sifa wakati kuna mafukara wa kutupwa
 
Asilimia kubwa ya Wanaigeria hawana sehemu ya kulala, wanalala mabarabarani na chini ya madaraja, ni masikini wa kutupwa,
 
Rugemalila mbona amumpi pongezi alitoa million 400 mchango wa harusi
 
Back
Top Bottom