Bima ya Afya kwa wote Tanzania is impossible

Bima ya Afya kwa wote Tanzania is impossible

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Uchumi, mila, dini, desturi na huduma zetu za afya haviruhusu kutoa Bima ya afya kwa wote. Matibabu ni hitaji la nne la binadamu nyuma ya hewa, maji na chakula (Maslow's). Jiulize je, jamii yote inapata hewa, maji na chakula? Kama jibu ni bado basi bima ya afya kwa wote ni kitendawili.

Uchumi wetu: Wananchi hawana pesa ya kulipia ugonjwa ambao haujatokea wakati Kuna shida Leo inayoshindikana kutatuliwa kwa ukosefu wa pesa.

Dini na Mila: mtu mmoja ana wake na watoto wengi sana kuliko idadi inayotakiwa na bima. Mke yupi atibiwe na nani aachwe? Watoto wepi wasitibiwe?

Huduma za afya: Watu wakiwa na bima wanahamasika wengi kwenda kutibiwa hata kwa ugonjwa kidogo sana ili hela yake isipotee bure. Je, tunao watumishi wa afya wa kutosha kuhudumia ongezeko hilo? Vifaa je? Wodi je? Dawa je?

Tabia za maskini: maskini wanaugua sana kutokana na uwezo mdogo wa kufuata kanuni za afya. Kila siku watakwenda hospital.

Hata mataifa makubwa yameshindwa kutoa Bima ya afya kwa wote sembuse sisi?

Huduma zitakuwa hovyohovyo kabisa.
 
Umesahau kitu kingine "hatuna viwanda vinavyo vitakavyo zalisha vifaa tiba na dawa

Leo tu 21 percent waliopo (kwamana ya watumishi serikalini wanajuta) madawa yooote yanaazia Bei 70000 kwenda juu kwenye famasi muhimbili na maeneo mengine zinakosekana

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
 
Malengo ya Serikali ya Tanzania katika suala la bima ya afya kwa wote sio Huduma! Ila wanaforce wapate hela za kusimamisha tena NHIF ili wawe wanajikopesha vizur na kula vizur hela za wananchi, kuhusu huduma ya afya tutajua wenyewe
 
Nimefuatilia namna ya utekelezaji wa zoezi hili ulivyopangwa kutekelezwa,naamini mafanikio yatakuepo japo hitafikiwa 100% kama hivyo inavyoitwa "bima ya afya kwa wote".

Kama ambavyo unavyoona sasa kwamba huwezi pata line ya simu bila ya namba ya nida Basi na kwa issue ya bima ya afya itakuwa hivyo kwa baadhi ya mambo fulani;

Mfano huwezi pata leseni ya biashara ama leseni ya udereva ama kusajiriwa chuo chochote pasipo bima ya afya.Hapa utaona ya kwamba kwa muundo huu lazima wataongeza idadi ya watu wenye bima ya afya hili ndilo lengo.Watu wakifikiwa wengi hata kiwango chakuchangia nacho kitashuka.

Ulipolala wewe leo wenzako ndipo walipoamkia jana,wanafahamu fika nchi hii watu wake ni masikini na hakuna atakae kamatwa eti kwa sababu hana bima ya afya.

Kupitia makundi fulani kubanwa,na kwakuwa kila mnufaika atakuwa na wategemezi kadhaa,hawa masikini wengi nao watakua sehemu ya wanufaika kupitia ndugu zao waliolipa bima.

Kimsingi ukitizama kwa undani utagundua wanachokitafuta serikali ni kuongeza nguvu/pesa kwenye mfuko wa bima ya afya ya taifa ili usifilisike, na si watu wote kuwa na bima kama wengi wanavyodhani,japokuwa kama ikitokea watu wote wamekuwa na bima basi kwa serikali itakua bora pia.

Natumai nimeeleweka japo umfuko ukishatuna wanatabia yakuhamisha pesa kwenda kwenye matumizi mengine ,

Asante.
 
Impossible is nothing


Hili ni jambo jema na serikali walishikie kidete liweze kutekelezwa kwa ufasaha

Wazee tasaf zao zitahusika nk hivyo ni jambo jemaaaa

Kwangu naomba lianze mara moja
 
Kama serikali imeshindwa kutoa huduma kwa hawa wachache walionao,wanatarajia watatoa vipi huduma kwa lundo wanalotaka kulitengeneza?!! Wanachotafuta ni pesa ya kufidia magap ya pesa walizokula tayari..hakuna kitu kitafeli nchi hii kama hiyo bima ya afya kwa wote..waache kabisa huu upuuzi
 
Muhimu uwe na bima ya afya iwe chf, nhif, aar nk

Hawa kupangii uwe na bima gani ila uwe na bima, ukitaka bima binafsi Au hizi za kutoka serikali...

Ni mpango safi sana...

Mambo ya kuambiwa mjomba Au bibi shangazi ana umwa hana pesa hii ina tusaidia, bima unayo kwa nini usiende kutibiwa

Mtoto yupo shule ana umwa na bima anayo kwann asiende kutibiwa

Hili jambo ni safi sana

Leo ukitaka kuingia ktk baadhi ya mataifa lazima uwe na bima ya afya ndio una pewa visa ya kuingia

Ili udailiwe ktk shule zao lazima uwe na bima ya afya

Ili upewe kibali cha kazi lazima uwe na bima ya afya

Nk

Hili swala ni muhimu, kufeli kwao kusiwe sababu na sisi tufeli

Ngoja twende na tuta kapo fika na changamoto totakazo kutana nazo basi tuta tafuta namna ya kukabiliana nazo
 
Uchumi, mila, dini, desturi na huduma zetu za afya haviruhusu kutoa Bima ya afya kwa wote.

Uchumi wetu: Wananchi hawana pesa ya kulipia ugonjwa ambao haujatokea wakati Kuna shida Leo inayoshindikana kutatuliwa kwa ukosefu wa pesa.

Dini na Mila: mtu mmoja ana wake na watoto wengi sana kuliko idadi inayotakiwa na bima. Mke yupi atibiwe na nani aachwe? Watoto wepi wasitibiwe?

Huduma za afya: Watu wakiwa na bima wanahamasika wengi kwenda kutibiwa hata kwa ugonjwa kidogo sana ili hela yake isipotee bure. Je, tunao watumishi wa afya wa kutosha kuhudumia ongezeko hilo? Vifaa je? Wodi je? Dawa je?

Tabia za maskini: maskini wanaugua sana kutokana na uwezo mdogo wa kufuata kanuni za afya. Kila siku watakwenda hospital.

Hata mataifa makubwa yameshindwa kutoa Bima ya afya kwa wote sembuse sisi?

Huduma zitakuwa hovyohovyo kabisa.
Kavulata! Naungana na wewe!

Kama maswali ya muhimu Kwa jamii kama maji, Shule Hospitali zilizopo zenyewe dawa unaandikiwa hadi upate kitumia siku zinaenda! Hii ni kitendawili kulifanikisha.

Na isitoshe bado hatuna uke utaalamu wa kuweka kumbukumbu kimtandao.

Hii tabia ya kuweka kumbukumbu kwenye makaratasi zaidi nayo shida. Hiki ni kipindi Hospitali zote nchini ziwe na uwekaji kumbukumbu kwenye computer.

Mpangilio wa kuwaona wagonjwa nao uboreshwe sio wanakusanyika Hospitali kutwa mzima.

MaDr. Naonwaelewe kazi zao kwani nao ni tatizo.
 
Ondoa negative energy yako katika maendeleo ya nchi yetu walahi [emoji2959]
Nafumba mdomo wako na chochote utakacho nena au kuwaza kisitokee kabisa shindwa na ulegee walahi!
 
Uchumi, mila, dini, desturi na huduma zetu za afya haviruhusu kutoa Bima ya afya kwa wote.

Uchumi wetu: Wananchi hawana pesa ya kulipia ugonjwa ambao haujatokea wakati Kuna shida Leo inayoshindikana kutatuliwa kwa ukosefu wa pesa.

Dini na Mila: mtu mmoja ana wake na watoto wengi sana kuliko idadi inayotakiwa na bima. Mke yupi atibiwe na nani aachwe? Watoto wepi wasitibiwe?

Huduma za afya: Watu wakiwa na bima wanahamasika wengi kwenda kutibiwa hata kwa ugonjwa kidogo sana ili hela yake isipotee bure. Je, tunao watumishi wa afya wa kutosha kuhudumia ongezeko hilo? Vifaa je? Wodi je? Dawa je?

Tabia za maskini: maskini wanaugua sana kutokana na uwezo mdogo wa kufuata kanuni za afya. Kila siku watakwenda hospital.

Hata mataifa makubwa yameshindwa kutoa Bima ya afya kwa wote sembuse sisi?

Huduma zitakuwa hovyohovyo kabisa.

Hizo pesa za bima zikishachangwa zitaitwa pesa za rais, na huko zitachotwa kupelekwa kwenye shughuli nyingine hasa za kusaka sifa za kisiasa, na hakuna mwananchi ataweza kuhoji. Kibaya zaidi bado huduma za afya zitaendelea kuwa duni.
 
Ondoa negative energy yako katika maendeleo ya nchi yetu walahi [emoji2959]
Nafumba mdomo wako na chochote utakacho nena au kuwaza kisitokee kabisa shindwa na ulegee walahi!

Kama mlijipanga kupata fedha za kununulia maVX na kujichotea pesa za wajinga, basi mjue mmechemsha.
 
Kama mlijipanga kupata fedha za kununulia maVX na kujichotea pesa za wajinga, basi mjue mmechemsha.
Bima ya afya kwa wote lazima iwepo, nyie wakosoaji na wajinga wachache hamuwezi kukwamisha, mnataka watu waendelee kufa kwa marelia kwa kukosa fedha za matibabu
 
Bima ya afya kwa wote lazima iwepo, nyie wakosoaji na wajinga wachache hamuwezi kukwamisha, mnataka watu waendelee kufa kwa marelia kwa kukosa fedha za matibabu

Sisi tutajitibu wenyewe, hiyo Bima ya Afya wapeni wanaohitaji kushikiwa fedha za matibabu na serikali ya majizi.
 
Nimefuatilia namna ya utekelezaji wa zoezi hili ulivyopangwa kutekelezwa,naamini mafanikio yatakuepo japo hitafikiwa 100% kama hivyo inavyoitwa "bima ya afya kwa wote".

Kama ambavyo unavyoona sasa kwamba huwezi pata line ya simu bila ya namba ya nida Basi na kwa issue ya bima ya afya itakuwa hivyo kwa baadhi ya mambo fulani;

Mfano huwezi pata leseni ya biashara ama leseni ya udereva ama kusajiriwa chuo chochote pasipo bima ya afya.Hapa utaona ya kwamba kwa muundo huu lazima wataongeza idadi ya watu wenye bima ya afya hili ndilo lengo.Watu wakifikiwa wengi hata kiwango chakuchangia nacho kitashuka.

Ulipolala wewe leo wenzako ndipo walipoamkia jana,wanafahamu fika nchi hii watu wake ni masikini na hakuna atakae kamatwa eti kwa sababu hana bima ya afya.

Kupitia makundi fulani kubanwa,na kwakuwa kila mnufaika atakuwa na wategemezi kadhaa,hawa masikini wengi nao watakua sehemu ya wanufaika kupitia ndugu zao waliolipa bima.

Kimsingi ukitizama kwa undani utagundua wanachokitafuta serikali ni kuongeza nguvu/pesa kwenye mfuko wa bima ya afya ya taifa ili usifilisike, na si watu wote kuwa na bima kama wengi wanavyodhani,japokuwa kama ikitokea watu wote wamekuwa na bima basi kwa serikali itakua bora pia.

Natumai nimeeleweka japo umfuko ukishatuna wanatabia yakuhamisha pesa kwenda kwenye matumizi mengine ,

Asante.
Unaelewa maana ya Bima?

Tuanzie hapo
 
Uchumi, mila, dini, desturi na huduma zetu za afya haviruhusu kutoa Bima ya afya kwa wote.

Uchumi wetu: Wananchi hawana pesa ya kulipia ugonjwa ambao haujatokea wakati Kuna shida Leo inayoshindikana kutatuliwa kwa ukosefu wa pesa.

Dini na Mila: mtu mmoja ana wake na watoto wengi sana kuliko idadi inayotakiwa na bima. Mke yupi atibiwe na nani aachwe? Watoto wepi wasitibiwe?

Huduma za afya: Watu wakiwa na bima wanahamasika wengi kwenda kutibiwa hata kwa ugonjwa kidogo sana ili hela yake isipotee bure. Je, tunao watumishi wa afya wa kutosha kuhudumia ongezeko hilo? Vifaa je? Wodi je? Dawa je?

Tabia za maskini: maskini wanaugua sana kutokana na uwezo mdogo wa kufuata kanuni za afya. Kila siku watakwenda hospital.

Hata mataifa makubwa yameshindwa kutoa Bima ya afya kwa wote sembuse sisi?

Huduma zitakuwa hovyohovyo kabisa.
Hawa ni wapumbavu Sana, hata Ulaya kuna nchi wameshindwa kitu hiki, sasa maccm mataahira wanadanganya watz; pumbavu Sana, siasa za maji taka, takataka kabisa!
 
Kimsingi ukitizama kwa undani utagundua wanachokitafuta serikali ni kuongeza nguvu/pesa kwenye mfuko wa bima ya afya ya taifa ili usifilisike, na si watu wote
Hili haliwezekani. Na ndicho anachokiongelea mleta mada.

Ongezeko la pesa linaenda sambamba na ongezeko la wanufaika. Kama wameshindwa kutoa huduma bora za bima ya afya kwa wachangiaji wachache wenye uhakika wa vipato (watumishi wa umma), hawataweza kabisa endapo maskini wakianza kuchangia
 
Mf. Nataka leseni ya biashara, naambiwa niwe na bima ya afya ili nipate. Nakosa biashara na serikali inakosa mapato.
 
Back
Top Bottom