Bima ya Afya, mnachokifanya mnajua madhara yake?

Bima ya Afya, mnachokifanya mnajua madhara yake?

DENAMWE

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2019
Posts
862
Reaction score
871
Mimi ni mstaafu mwandamizi niliyepo wilaya ya Ngara mkoa wa Kagera.

Nilipata tetesi za kuwapo kwa uhakiki wa wastaafu walio kwenye mfuko wa bima ya Afya tangu mwezi Machi mwaka huu. Kila aliyeniambia nilipomuuliza alikozipata taarifa, naye aliniambia ameambiwa na mwingine.
Hakukuwapo uthibitisho wa chanzo.

Nilihisi kuwa ni jumbe za kitapeli ambazo zinatumwa mara kwa mara. Jana, jamaa yangu akanitumia na kuniuliza iwapo nimepata ujumbe huu:

"NHIF 17.03.2023 SAA 03:11PM NDG. MWANACHAMA MSTAAFU,TAFADHALI FIKA NA MWENZAWAKO KTK. OFISI YA MFUKO ILIYO KARIBU KWA AJILI YA ZOEZI LA UHAKIKI KABLA YA 30.04.2023. AIDHA, FIKA NA NA. YAKO YA NIDA NA NA. MWENZA WAKO. KWA UFAFANUZI _ PIGANA. 199 BILA MALIPO. SENDER HENRY".

Naye alitumiwa na mstaafu mwenzetu. Sikuamini kuwa huo ni ujumbe halali. Mtindo/namna ya uandishi haikuniongoza kuamini kuwa umetumwa na taasisi hii kubwa. Kuna makosa mengi ya kiuandishi na hata ya kimantiki. Hilo tuliache.

Niliingia kwenye tovuti yao. Sikuona tangazo hilo. Niliwasiliana nao kupitia simu hiyo 199. Nilipata ushirikiano mkubwa kwa aliyenipokea. Niliambiwa yafuatayo:

1. Ni kweli uhakiki upo. Unahusisha wastaafu na walioko kazini. Wanataka mstaafu aende na mweza wake.

2. Kila mhusika alishaarifiwa kupitia simu yake na kila mmoja ana tarehe yake. Mimi na wastaafu sita niliowauliza hatuna ujumbe huu.

3. Uhakiki unafanyika makao makuu ya mkoa.

4. Mwisho wa uhakiki ni Mei 30.

Inaelekea bima ya afya hawafahamu kuwa Wastaafu (wateja wao):
i) Ni wazee
ii) Wengi ni wagonjwa
iii) Wengi wana pato duni mno ambalo huenda halitoshi hata gharama ya kwenda mkoani.
iv) Baadhi ni walemavu
v) Kuna ambao hawawezi kusoma jumbe hizo

Yaani wao kwenye simu zao wanafahamu kubonyeza kitufe kimoja tu. Cha kupokelea simu.
Hawa hawawezi kuweka vocha, kukata simu baada ya maongezi, kuongeza salio, kuunga kifurushi nk.
Sembuse kusoma au kuandika ujumbe!

Ushauri:
1. Uhakiki ufanywe jirani na wahusika. Ikiwezekana kwenye Kata. Kuwalazimisha kwenda mkoani kuachwe. Haya ni mateso. Mateso makubwa mno.

Mstaafu aliyepo kijiji cha Muganza wilayani Ngara, mkoa wa Kagera, uhakiki huu utamgharimu siku 5 (kwenda Bukoba na Kurudi). Baadhi ya wastaafu wanahitaji kusindikizwa/kupata wasaidizi. Mbali ya adha za safari, fikiria muda na gharama za safari. Mkifika kwenye kata zao ni vema zaidi.

2. Zoezi hili lifanyike kwa uwazi na kwa haki. Tangazeni kwenye vyombo vya habari. Wekeni kwenye tovuti yenu.
Wasilianeni vema na wateja/wadau wenu. Uduni wa taarifa hizi na hata uandishi wa sms ya wito tunautofautishaje na sms nyingine za kitapeli tunazotumiwa mara kwa mara.

3. Fungueni ofisi wilayani au muweke dawati lenu ama kwa Mkuu wa wilaya au Halmashauri. Mnataka wazee hawa wafe kwa ajali barabarani kwa safari? Mara uhakiki wa PSSSF mkoani na sasa uhakiki huu nao mkoani.
Magonjwa mengine yanatokana adha hizi.

Wazee mnaowasumbua na kuwatesa leo walitumikia nchi hii kwa bidii na uaminifu mkubwa. Msiwalipe mateso kwa kuwajaza majuto na kihoro.

KWA HALI HII, UZEE SI DHAHABU BALI NI ADHABU.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Mimi ni mstaafu mwandamizi niliyepo wilaya ya Ngara mkoa wa Kagera.

Nilipata tetesi za kuwapo kwa uhakiki wa wastaafu walio kwenye mfuko wa bima ya Afya tangu mwezi Machi mwaka huu.
Kila aliyeniambia nilipomuuliza alikozipata taarifa, naye aliniambia ameambiwa na mwingine.
Nimelia sana ...
[emoji24][emoji24][emoji24]
 
Hata mfuko wao unapumulia mashine sababu ya ufisadi wakifanya ivyo wakahakiki wote itakula kwao. Tatizo limeanzia mbali.
 
Kuna watu tunatamani hata kupata hyo bima we umeambiwa kuhakiki tuu unaanza kulia lia, unataka wakufate?? Kuna vijana wanahangaika kufanya usaili Dodoma , too complicated , ukijua namna wengine wanavyosota kwenye hii nchi yaani kwa ahueni uliyo nayo kimya kimya ungeenda kuhakikiwa mkoani kwako
 
Kuna watu tunatamani hata kupata hyo bima we umeambiwa kuhakiki tuu unaanza kulia lia, unataka wakufate?? Kuna vijana wanahangaika kufanya usaili Dodoma , too complicated , ukijua namna wengine wanavyosota kwenye hii nchi yaani kwa ahueni uliyo nayo kimya kimya ungeenda kuhakikiwa mkoani kwako
Asante sana kwa mawazo yako.
Watakujibu wengine.
 
Hata mfuko wao unapumulia mashine sababu ya ufisadi wakifanya ivyo wakahakiki wote itakula kwao. Tatizo limeanzia mbali.
Watuambie tuchangie gharama za uhakiki na posho zao kisha waje huku tuliko.
Tutawachangia.
 
Mimi ni mstaafu mwandamizi niliyepo wilaya ya Ngara mkoa wa Kagera.

Nilipata tetesi za kuwapo kwa uhakiki wa wastaafu walio kwenye mfuko wa bima ya Afya tangu mwezi Machi mwaka huu. Kila aliyeniambia nilipomuuliza alikozipata taarifa, naye aliniambia ameambiwa na mwingine.
Hakukuwapo uthibitisho wa chanzo.

Nilihisi kuwa ni jumbe za kitapeli ambazo zinatumwa mara kwa mara. Jana, jamaa yangu akanitumia na kuniuliza iwapo nimepata ujumbe huu:

"NHIF 17.03.2023 SAA 03:11PM NDG. MWANACHAMA MSTAAFU,TAFADHALI FIKA NA MWENZAWAKO KTK. OFISI YA MFUKO ILIYO KARIBU KWA AJILI YA ZOEZI LA UHAKIKI KABLA YA 30.04.2023. AIDHA, FIKA NA NA. YAKO YA NIDA NA NA. MWENZA WAKO. KWA UFAFANUZI _ PIGANA. 199 BILA MALIPO. SENDER HENRY".

Naye alitumiwa na mstaafu mwenzetu. Sikuamini kuwa huo ni ujumbe halali. Mtindo/namna ya uandishi haikuniongoza kuamini kuwa umetumwa na taasisi hii kubwa. Kuna makosa mengi ya kiuandishi na hata ya kimantiki. Hilo tuliache.

Niliingia kwenye tovuti yao. Sikuona tangazo hilo. Niliwasiliana nao kupitia simu hiyo 199. Nilipata ushirikiano mkubwa kwa aliyenipokea. Niliambiwa yafuatayo:

1. Ni kweli uhakiki upo. Unahusisha wastaafu na walioko kazini. Wanataka mstaafu aende na mweza wake.

2. Kila mhusika alishaarifiwa kupitia simu yake na kila mmoja ana tarehe yake. Mimi na wastaafu sita niliowauliza hatuna ujumbe huu.

3. Uhakiki unafanyika makao makuu ya mkoa.

4. Mwisho wa uhakiki ni Mei 30.

Inaelekea bima ya afya hawafahamu kuwa Wastaafu (wateja wao):
i) Ni wazee
ii) Wengi ni wagonjwa
iii) Wengi wana pato duni mno ambalo huenda halitoshi hata gharama ya kwenda mkoani.
iv) Baadhi ni walemavu
v) Kuna ambao hawawezi kusoma jumbe hizo

Yaani wao kwenye simu zao wanafahamu kubonyeza kitufe kimoja tu. Cha kupokelea simu.
Hawa hawawezi kuweka vocha, kukata simu baada ya maongezi, kuongeza salio, kuunga kifurushi nk.
Sembuse kusoma au kuandika ujumbe!

Ushauri:
1. Uhakiki ufanywe jirani na wahusika. Ikiwezekana kwenye Kata. Kuwalazimisha kwenda mkoani kuachwe. Haya ni mateso. Mateso makubwa mno.

Mstaafu aliyepo kijiji cha Muganza wilayani Ngara, mkoa wa Kagera, uhakiki huu utamgharimu siku 5 (kwenda Bukoba na Kurudi). Baadhi ya wastaafu wanahitaji kusindikizwa/kupata wasaidizi. Mbali ya adha za safari, fikiria muda na gharama za safari. Mkifika kwenye kata zao ni vema zaidi.

2. Zoezi hili lifanyike kwa uwazi na kwa haki. Tangazeni kwenye vyombo vya habari. Wekeni kwenye tovuti yenu.
Wasilianeni vema na wateja/wadau wenu. Uduni wa taarifa hizi na hata uandishi wa sms ya wito tunautofautishaje na sms nyingine za kitapeli tunazotumiwa mara kwa mara.

3. Fungueni ofisi wilayani au muweke dawati lenu ama kwa Mkuu wa wilaya au Halmashauri. Mnataka wazee hawa wafe kwa ajali barabarani kwa safari? Mara uhakiki wa PSSSF mkoani na sasa uhakiki huu nao mkoani.
Magonjwa mengine yanatokana adha hizi.

Wazee mnaowasumbua na kuwatesa leo walitumikia nchi hii kwa bidii na uaminifu mkubwa. Msiwalipe mateso kwa kuwajaza majuto na kihoro.

KWA HALI HII, UZEE SI DHAHABU BALI NI ADHABU.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Hawawezi kufanya hayo kwa sababu hizo akili hawana wala huo ubunifu hawana.

Huku ni genge la ndugu wa VIONGOZI na watoto wao kupiga pesa.

Ubunifu wao ni kwenye kuiba pesa tuu na kulipana posho.

Pole sana mstaafu, hawana nia njema nawe.
 
Watuambie tuchangie gharama za uhakiki na posho zao kisha waje huku tuliko.
Tutawachangia.
Sasa nawe umekuwa mbinafsi, unafikiri wastaafu wote Wana hizo hela za kuchezea ??

Kuna wastaafu hata elfu mbili ya nauli hana ndio ije kumchangia afisa wa NHIF

WAJE KUWAHUDUMIA HUKO NA HELA ZAO KAMA WALIVYOFANYA PSSSF
 
Mbona kwenye ujumbe wa NHIF wanasema ofisi ya
Mimi ni mstaafu mwandamizi niliyepo wilaya ya Ngara mkoa wa Kagera.

Nilipata tetesi za kuwapo kwa uhakiki wa wastaafu walio kwenye mfuko wa bima ya Afya tangu mwezi Machi mwaka huu. Kila aliyeniambia nilipomuuliza alikozipata taarifa, naye aliniambia ameambiwa na mwingine.
Hakukuwapo uthibitisho wa chanzo.

Nilihisi kuwa ni jumbe za kitapeli ambazo zinatumwa mara kwa mara. Jana, jamaa yangu akanitumia na kuniuliza iwapo nimepata ujumbe huu:

"NHIF 17.03.2023 SAA 03:11PM NDG. MWANACHAMA MSTAAFU,TAFADHALI FIKA NA MWENZAWAKO KTK. OFISI YA MFUKO ILIYO KARIBU KWA AJILI YA ZOEZI LA UHAKIKI KABLA YA 30.04.2023. AIDHA, FIKA NA NA. YAKO YA NIDA NA NA. MWENZA WAKO. KWA UFAFANUZI _ PIGANA. 199 BILA MALIPO. SENDER HENRY".

Naye alitumiwa na mstaafu mwenzetu. Sikuamini kuwa huo ni ujumbe halali. Mtindo/namna ya uandishi haikuniongoza kuamini kuwa umetumwa na taasisi hii kubwa. Kuna makosa mengi ya kiuandishi na hata ya kimantiki. Hilo tuliache.

Niliingia kwenye tovuti yao. Sikuona tangazo hilo. Niliwasiliana nao kupitia simu hiyo 199. Nilipata ushirikiano mkubwa kwa aliyenipokea. Niliambiwa yafuatayo:

1. Ni kweli uhakiki upo. Unahusisha wastaafu na walioko kazini. Wanataka mstaafu aende na mweza wake.

2. Kila mhusika alishaarifiwa kupitia simu yake na kila mmoja ana tarehe yake. Mimi na wastaafu sita niliowauliza hatuna ujumbe huu.

3. Uhakiki unafanyika makao makuu ya mkoa.

4. Mwisho wa uhakiki ni Mei 30.

Inaelekea bima ya afya hawafahamu kuwa Wastaafu (wateja wao):
i) Ni wazee
ii) Wengi ni wagonjwa
iii) Wengi wana pato duni mno ambalo huenda halitoshi hata gharama ya kwenda mkoani.
iv) Baadhi ni walemavu
v) Kuna ambao hawawezi kusoma jumbe hizo

Yaani wao kwenye simu zao wanafahamu kubonyeza kitufe kimoja tu. Cha kupokelea simu.
Hawa hawawezi kuweka vocha, kukata simu baada ya maongezi, kuongeza salio, kuunga kifurushi nk.
Sembuse kusoma au kuandika ujumbe!

Ushauri:
1. Uhakiki ufanywe jirani na wahusika. Ikiwezekana kwenye Kata. Kuwalazimisha kwenda mkoani kuachwe. Haya ni mateso. Mateso makubwa mno.

Mstaafu aliyepo kijiji cha Muganza wilayani Ngara, mkoa wa Kagera, uhakiki huu utamgharimu siku 5 (kwenda Bukoba na Kurudi). Baadhi ya wastaafu wanahitaji kusindikizwa/kupata wasaidizi. Mbali ya adha za safari, fikiria muda na gharama za safari. Mkifika kwenye kata zao ni vema zaidi.

2. Zoezi hili lifanyike kwa uwazi na kwa haki. Tangazeni kwenye vyombo vya habari. Wekeni kwenye tovuti yenu.
Wasilianeni vema na wateja/wadau wenu. Uduni wa taarifa hizi na hata uandishi wa sms ya wito tunautofautishaje na sms nyingine za kitapeli tunazotumiwa mara kwa mara.

3. Fungueni ofisi wilayani au muweke dawati lenu ama kwa Mkuu wa wilaya au Halmashauri. Mnataka wazee hawa wafe kwa ajali barabarani kwa safari? Mara uhakiki wa PSSSF mkoani na sasa uhakiki huu nao mkoani.
Magonjwa mengine yanatokana adha hizi.

Wazee mnaowasumbua na kuwatesa leo walitumikia nchi hii kwa bidii na uaminifu mkubwa. Msiwalipe mateso kwa kuwajaza majuto na kihoro.

KWA HALI HII, UZEE SI DHAHABU BALI NI ADHABU.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Nashindwa kuelewa mbona tangazo la ujumbe mfupi linasema ofisi iliyo karibu na wewe unasema makao makuu ya mkoa?
 
Hawawezi kufanya hayo kwa sababu hizo akili hawana wala huo ubunifu hawana.

Huku ni genge la ndugu wa VIONGOZI na watoto wao kupiga pesa.

Ubunifu wao ni kwenye kuiba pesa tuu na kulipana posho.

Pole sana mstaafu, hawana nia njema nawe.
Asante sana.
 
Sasa nawe umekuwa mbinafsi, unafikiri wastaafu wote Wana hizo hela za kuchezea ??

Kuna wastaafu hata elfu mbili ya nauli hana ndio ije kumchangia afisa wa NHIF

WAJE KUWAHUDUMIA HUKO NA HELA ZAO KAMA WALIVYOFANYA PSSSF
Si ubinafsi rafiki.
Ni kutapatapa.
Nimewaza hivi kwa kuwa tunatakiwa twende mkoani ambako gharama ni kubwa mno.
Hatuimudu.
Heri nusu shari......
 
Mbona kwenye ujumbe wa NHIF wanasema ofisi ya
Nashindwa kuelewa mbona tangazo la ujumbe mfupi linasema ofisi iliyo karibu na wewe unasema makao makuu ya mkoa?
Hakuna ofisi ya wilaya.
 
Kama kweli ni wasikivu,lazima watatoa maelekezo mapya maana umeeleza kwa ufasaha na imeeleweka.
 
Mimi ni mstaafu mwandamizi niliyepo wilaya ya Ngara mkoa wa Kagera.

Nilipata tetesi za kuwapo kwa uhakiki wa wastaafu walio kwenye mfuko wa bima ya Afya tangu mwezi Machi mwaka huu. Kila aliyeniambia nilipomuuliza alikozipata taarifa, naye aliniambia ameambiwa na mwingine.
Hakukuwapo uthibitisho wa chanzo.

Nilihisi kuwa ni jumbe za kitapeli ambazo zinatumwa mara kwa mara. Jana, jamaa yangu akanitumia na kuniuliza iwapo nimepata ujumbe huu:

"NHIF 17.03.2023 SAA 03:11PM NDG. MWANACHAMA MSTAAFU,TAFADHALI FIKA NA MWENZAWAKO KTK. OFISI YA MFUKO ILIYO KARIBU KWA AJILI YA ZOEZI LA UHAKIKI KABLA YA 30.04.2023. AIDHA, FIKA NA NA. YAKO YA NIDA NA NA. MWENZA WAKO. KWA UFAFANUZI _ PIGANA. 199 BILA MALIPO. SENDER HENRY".

Naye alitumiwa na mstaafu mwenzetu. Sikuamini kuwa huo ni ujumbe halali. Mtindo/namna ya uandishi haikuniongoza kuamini kuwa umetumwa na taasisi hii kubwa. Kuna makosa mengi ya kiuandishi na hata ya kimantiki. Hilo tuliache.

Niliingia kwenye tovuti yao. Sikuona tangazo hilo. Niliwasiliana nao kupitia simu hiyo 199. Nilipata ushirikiano mkubwa kwa aliyenipokea. Niliambiwa yafuatayo:

1. Ni kweli uhakiki upo. Unahusisha wastaafu na walioko kazini. Wanataka mstaafu aende na mweza wake.

2. Kila mhusika alishaarifiwa kupitia simu yake na kila mmoja ana tarehe yake. Mimi na wastaafu sita niliowauliza hatuna ujumbe huu.

3. Uhakiki unafanyika makao makuu ya mkoa.

4. Mwisho wa uhakiki ni Mei 30.

Inaelekea bima ya afya hawafahamu kuwa Wastaafu (wateja wao):
i) Ni wazee
ii) Wengi ni wagonjwa
iii) Wengi wana pato duni mno ambalo huenda halitoshi hata gharama ya kwenda mkoani.
iv) Baadhi ni walemavu
v) Kuna ambao hawawezi kusoma jumbe hizo

Yaani wao kwenye simu zao wanafahamu kubonyeza kitufe kimoja tu. Cha kupokelea simu.
Hawa hawawezi kuweka vocha, kukata simu baada ya maongezi, kuongeza salio, kuunga kifurushi nk.
Sembuse kusoma au kuandika ujumbe!

Ushauri:
1. Uhakiki ufanywe jirani na wahusika. Ikiwezekana kwenye Kata. Kuwalazimisha kwenda mkoani kuachwe. Haya ni mateso. Mateso makubwa mno.

Mstaafu aliyepo kijiji cha Muganza wilayani Ngara, mkoa wa Kagera, uhakiki huu utamgharimu siku 5 (kwenda Bukoba na Kurudi). Baadhi ya wastaafu wanahitaji kusindikizwa/kupata wasaidizi. Mbali ya adha za safari, fikiria muda na gharama za safari. Mkifika kwenye kata zao ni vema zaidi.

2. Zoezi hili lifanyike kwa uwazi na kwa haki. Tangazeni kwenye vyombo vya habari. Wekeni kwenye tovuti yenu.
Wasilianeni vema na wateja/wadau wenu. Uduni wa taarifa hizi na hata uandishi wa sms ya wito tunautofautishaje na sms nyingine za kitapeli tunazotumiwa mara kwa mara.

3. Fungueni ofisi wilayani au muweke dawati lenu ama kwa Mkuu wa wilaya au Halmashauri. Mnataka wazee hawa wafe kwa ajali barabarani kwa safari? Mara uhakiki wa PSSSF mkoani na sasa uhakiki huu nao mkoani.
Magonjwa mengine yanatokana adha hizi.

Wazee mnaowasumbua na kuwatesa leo walitumikia nchi hii kwa bidii na uaminifu mkubwa. Msiwalipe mateso kwa kuwajaza majuto na kihoro.

KWA HALI HII, UZEE SI DHAHABU BALI NI ADHABU.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Hapo lengo ni kupunguza watu ili kutua mzigo.

Usipoenda ndio furaha yao, wanachukulia labda umeshakufa.


Huo mfuko ni trash kabisa
 
Na hii ishu ya BIMA ya Afya kuwanyima huduma za Dharura wanaopoteza vitambulisho eti mpaka waje na Vitambulisho vya NIDA ni mbaya sana. Huyu mtu wakati akishughulikia kupata hiyo namba ya NIDA akipata changamoto ya afya afanyeje sasa?.

Zamani mlikubali kuandikisha watu kwa kutumia vitambulisho vya mpiga kura, leo mtu ana dharura ya matibabu baada ta kupoteza kadi yake, kafuata procedure zote including Loss report ya polisi, kujaza fomu zenu upya, mihuri ya mwajiri kila kitu kipo halafu mnasema hamumpi nyaraka za dharura za matibabu mpaka aje na kadi ya NIDA, Huo ni Uchawi kuliko uchawi. Kwenye system zenu mtu mnamuona, ana shida ya dharura ya matibabu hamumpi, lakini kila mwezi bado mnakata hela ya mchangiaji. Huo kama siyo Udhalimu ni nini?

NHIF, acheni bureaucracy, Hudumieni watu, acheni kubadilibadili magoli wakati hela kila mwezi mnachukua.

Mimi au mtegemezi wangu akipata dharura kwa nyie kukataa kumpa matibabu kisa hana namba ya NIDA wakati kipindi najiandikisha mlitoa options kibao , sasa akidhurika nawashitaki!.
 
Back
Top Bottom