BIMA ya NHIF ina Packages zake, mara nyingi kwa JKCI nimeona NHIF huwa ipo kwa packages za NAJALI, WEKEZA, TIMIZA na NHIF ambayo ikiingia katika system huwa inasoma kama NHIF tu bila kuwa specified.
Kama NHIF yako ni aina ya NAJALI, WEKEZA, TIMIZA hapo kuna usumbufu utapata kwa baadhi ya huduma kulingana na Package yako.
Kama una NHIF ya kawaida ambayo haiko specified na packages nilizozitaja hapo juu.. Utapata huduma zote kulingana na utaratibu wa Bima ya NHIF na usumbufu kidogo unapungua.
Pia kuna zile NHIF ambazo huwa zina mkono wa taasisi na mashirika ya serikali mfano NHIF BUNGE, NHIF TRA, NHIF NMB BANK, NHIF BOT, nk. hawa huwa ni VIP Bima zao hazina longo longo wanapata kila kitu wakifika JKCI.
Ila kwa vyovyote vile ukiwa na kadi ya BIMA ya NHIF unaepuka usumbufu mkubwa sana ukienda JKCI, Unakuwa rahisi sana kuhudumiwa na kuonana na Daktari kwa kuwa mfumo wao pale una favor kuchakata taarifa za mtu aliyekuwa na BIMA kuliko mtu asiyekuwa nayo.
Muhimu mpeleke tu mtoto akapate huduma hayo mambo mengine watakusidia wahusika na isitoshe ofisi za Bima zipo karibu tu pale mule mule Muhimbili, kwahiyo changamoto yoyote ile inaweza kupatiwa ufumbuzi siku hiyo hiyo.