Binadamu Ana Hofu Mbili Za Asili, Hizi Ngingine Amefundishwa

Binadamu Ana Hofu Mbili Za Asili, Hizi Ngingine Amefundishwa

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Screenshot_20250202_151533_Google.jpg


Binadamu kiasili ameumbwa na hofu mbili tu,yaani hofu hizi ndio asili yake

Hofu ya kwanza ni kuanguka,hii ni hofu ya asili tangu tukiwa utotoni, ndio maana mtoto ambaye anaanza kusimama mara nyingi huwa na hofu ya kuanguka

Hofu ya pili ni ya sauti, hizi hofu mbili hatukufundishwa bali tumekuwa nazo kiasili tangu utotoni

Hofu nyingine zote tumefundishwa katika makuzi yetu,mfano mtoto ambaye hajajua hatar ya nyoka hawezi kumuogopa nyoka,na si ajabu ukamkuta anacheza na nyoka

Mtoto ambaye hajajua hatar ya moto labda mpaka umuunguze au aambiwe huo moto utaungua,ndio maana kuna msemo kama mtoto akililia wembe mpe kwani akijikata atajua kuwa wembe ni hatar

Ninachotaka kusema hapa,si kila jambo ni la kuhofia kwasababu hofu yako wewe sio hofu yangu mie,kama wewe unahofia single maza kwangu mimi ni watamu na wazuri tu

Kama wewe unahofia ndoa,basi usiniambukize hiyo hofu yako baki nayo mwenyewe mtuache sie ambao ndoa ndio msingi wa kujenga taasisi ya familia bora

Kwahiyo kwa hofu yoyote ambayo tumeaminishwa ipo na inasumbua jamii basi jitahidi usiwe sehemu ya hofu hiyo kwani hofu nyingine ni kwa watu dhaifu tu


Ni hayo tu!
 
Vipi kuhusu kifo.
Tumefundishwa pia, nikupe mfano mtu ambaye hajajifunza mambo ya dini kabisa,hajui pepo na moto,huyu kifo hakitamuogopesha kwakuwa atajua kifo ni kama kulala tu milele

Ila ambao tumefundishwa kupitia dini kwamba kuna pepo kwa wema na moto kwa wabaya lazima tuogope kifo

Lkn mcha mungu huwa haogopi kifo kwakuwa anajua anaenda kukutana na mola wake hali akiwa radhi nae
 
Tumefundishwa pia, nikupe mfano mtu ambaye hajajifunza mambo ya dini kabisa,hajui pepo na moto,huyu kifo hakitamuogopesha kwakuwa atajua kifo ni kama kulala tu milele

Ila ambao tumefundishwa kupitia dini kwamba kuna pepo kwa wema na moto kwa wabaya lazima tuogope kifo

Lkn mcha mungu huwa haogopi kifo kwakuwa anajua anaenda kukutana na mola wake hali akiwa radhi nae
Sio kweli mfano mtoto wako mdogo ukimkuta kalazwa hospitali hoi huwezi kuogopa kumpoteza
 
Sio kweli mfano mtoto wako mdogo ukimkuta kalazwa hospitali hoi huwezi kuogopa kumpoteza
Ndio hofu ambayo umejifunza kwamba kumbe kuna kifo,hapo hofu yako ni ya kumpoteza mtoto

Kwakuwa unajua kifo kitamchukua mpendwa wako
 
 
Back
Top Bottom