Binadamu anapokufa roho yake humrudia Mungu au huenda mbinguni au jehanamu?

Binadamu anapokufa roho yake humrudia Mungu au huenda mbinguni au jehanamu?

raslimali

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2014
Posts
1,958
Reaction score
1,744
Kitabu cha Mhubiri, moja ya vitabu vya biblia, sura ya 12 aya ya 7 inasema baada ya kufa roho ( nguvu/kani ya uzima iliyo ndani ya mwanadamu) humrudia Mungu aliyeitoa. Mafundisho ya roho ya mwanadamu kwenda Mbinguni/paradiso au jehenamu baada ya kufa yametoka wapi?
 
Labda umrudia, ili yeye ndio akaiambie sababu za kuipeleka motoni au mbinguni.

Sina uhakika lakini, nimeona kuwasubiria hadi watoke kwa mwamposa ndio wakujibu, utaganda sana.
 
Kitabu cha Mhubiri, moja ya vitabu vya biblia, sura ya 12 aya ya 7 inasema baada ya kufa roho ( nguvu/kani ya uzima iliyo ndani ya mwanadamu) humrudia Mungu aliyeitoa. Mafundisho ya roho ya mwanadamu kwenda Mbinguni/paradiso au jehenamu baada ya kufa yametoka wapi?
Mungu akiamua kuirudisha roho kwa Mtu aliyemuumba ili kumpongeza kushiriki karamu ya ufalme wa mbinguni tokana na kazi nzuri aliyoifanya duniani kabla ya kuwa Marehemu utamkataza?

Mungu ni muweza wa yote na hapangiwi chochote na Binadamu.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Hata wafu wenyewe hawajui roho zao zilienda wapi siku waliokufa.
Vitu vingine vipo nje ya uelewa wetu Ni Bora kuachana navyo tu.
 
If we both believe in Reincarnation Maybe we will have a chance in the next life.
 
Hapa Mhubiri anaweka wazi kwamba “mwanadamu na mnyama wote huenda mahali pamoja”, hivyo kudai kwamba roho zinaenda kuwa hai na kuishi mbinguni ni sawa na kusema roho za wanyama nazo huenda kuwa hai na kuishi mbingu au jehanamu!
Muhubiri 12:7 “Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.”

Neno la kiebrania lililotumika hapo kwenye neno “roho” ni ר֫וּחַ (ruach) – [roo’-akh] linalomaanisha “pumzi” au “upepo”. Hivyo Muhubiri 12:7 inasema mtu akifa mwili wake unarudi mavumbini, lakini pumuzi ya uhai inamrudia Mungu aliyeiweka ndani yake tangu mwanzo. Ayubu 27:3 inathibitisha kwa kusema, “(Kwa kuwa uhai wangu ukali mzima ndani yangu, Na roho ya Mungu i katika pua yangu😉” Hapa anaonyesha uhai na roho kuwa kitu kimoja katika pua ya mtu. Kuthibitisha ukweli huu zaidi katika Mwanzo 7:22 inasema, “kila kitu chenye pumzi ya roho ya uhai puani mwake kikafa, kila kilichokuwako katika nchi kavu.”

Pumzi ya roho ya uhai, hii inamaanisha ni ule uhai alionao mtu ambao ukiondolewa mtu anakufa Yakobo 2:26 inasema, “Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa.” Hapa analinganisha kati ya mwili na imani, na roho na matendo, kama mwili bila roho[pumzi ya Mungu] umekufa, vivyo hivyo imani bila mtendo imekufa. Mwanzo 2:7 inaweka wazi ukweli huu.

Mwanzo 2:7 “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.”

Hivyo mtu anapokufa mwili wake huyarudia mavumbi na pumzi ya uhai humrudia Mungu mwenyewe.
 
Sisi ni wanyama kama walivyo wanyama wengine , acha ngano za dini jiulize hao ngombe unaokula nyama zao Kila siku, mbuzi kuku na samaki roho zao zinaenda wapi.

Kimsingi hakuna kitu kinachoitwa roho Bali mifumo mikuu ya mwilinikipata hitilafu ndio mzunguko wa ufanyaji kazi wa viungo vingine husimama na ndio inakuwa mwisho hapo kama gari likiharibika.

Tunadanganyana Sana kujiona kuwa sisi ni WA muhimu kuliko viumbe vingine kwa sababu viumbe hao hatujui lugha zao, nao wanajitapa wao kwa wao kuwa Wana umuhimu Sana na sisi ni vijakazi wao
 
Roho uenda kuzimu au mbinguni kulingana na matendo ya mtu
 
Unless kuna server ambayo ndo inatunza kumbukumbu na ubongo ni receiver tu basi kwa fikra zangu za kibinadamu roho haina kumbukumbu wala ufahamu sababu ubongo unabaki ardhini na kuharibika.
 
Luka 16:19
Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa.

Luka 16:20
Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi,

Luka 16:21
naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake.

Luka 16:22
Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.

Luka 16:23
Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.

Luka 16:24
Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.

Luka 16:25
Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.

Luka 16:26
Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.

Luka 16:27
Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,

Luka 16:28
kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.

Luka 16:29
Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.

Luka 16:30
Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.

Luka 16:31
Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.
 
Acheni kuleta vitu vya kutunga. Kufa ni kufa tu. Kwani Duniani viumbe ni binadamu tu. Kwani sokwe. Nyani. Kuku. Mbwa . Ngombe . Punda nao roho zao zitakwenda Kwa nani. Mbona wengi wanasema kilichomo Duniani ni Cha mungu. Iweje binadamu tu ndiyo ànatajwa kwenda baada ya kufa. Acheni uongo nyie
 
Luka 16:19
Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa.

Luka 16:20
Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi,

Luka 16:21
naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake.

Luka 16:22
Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.

Luka 16:23
Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.

Luka 16:24
Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.

Luka 16:25
Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.

Luka 16:26
Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.

Luka 16:27
Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,

Luka 16:28
kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.

Luka 16:29
Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.

Luka 16:30
Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.

Luka 16:31
Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.
Nimekuelewa bt ukweli ndio huo
 
Back
Top Bottom