Binadamu anaweza kutibu ugonjwa wa kuzeeka?

Binadamu anaweza kutibu ugonjwa wa kuzeeka?

Wale haki na ukwa wa kwenye movi za nigeria [sijajua majina yao ila wapo hata kwenye wimbo wa kamilion ifugallo] mnawazungumziaje mana nilisikia mwaka 2010 mmoja ana 45 mwingn 38 lakn ukiwaangalia utazan wana 16 tungewauliza kwanza wao wanatumia nini uhenda tungepata jibu
 
Naamini kwa miaka 1000 ijayo kwa kasi ya teknolojia inavyokwenda uzee na kifo vitadhibitiwa.
Kiukweli kifo ni jambo linaloweza kudhibitiwa kbsa kwasbb hata kwenye vitabu vya dini kuna maandiko ya uzima wa milele. Hivyo tusitegemee huo uzima wa milele utaletwa na na kushushwa na Mungu kama mvua ila kitakachofanyika ni kumtumia binadamu kuuleta huo uzima wa milele kwasbb God ni nishat hawezi kuonekana wala kushikika hivyo uzima wa milele utaletwa na wanadamu wenyewe kupitia nguvu zake Mungu nadhani nimeeleweka
 
Hizo ni ndoto.kufa kuliwekwa na yule aliyeiweka dunia.Hakuna kiumbe ambacho kitaweza kugeuza uumbaji wake ata ipite miaka mingapi.
Hata wagunduzi wa ndege 🛫 walipoleta wazo la chombo kuweza kuruka angani ilionekana ndoto isiyowezekana.

Elon musk kwa sasa anajaribu kufanya majaribio ya Neuralink kwa binadamu na trust me itawezekana.
 
Oprah Winfrey hazeeki pia Dolly Parton kajifunze kwao...pia baadhi ya wa Japan
 
Kuzeeka sio Ugonjwa... Kuzeeka kunapelekea mwili kushindwa kuimili magonjwa... Juwa kutofautisha kuzeeka na kupata magonjwa.

Hapa duniani hakuna kiumbe hai, narudia tena kiumbe hai kinachoweza kuishi milele.

Viumbe vyote hai vimekuwa programmed kufa. Seli zetu zote mwilini zimekuwa programmed kuishi kwa muda fulani baada ya hapo kwa sababu zinakuwa zimepunguza uwezo wa kutenda kazi kwa ufanisi. Na njia moja wapo ta kugundua seli za mwili wako zimeanza kufa, ni kuanza kuona mvi. Mvi ni taarifa ya kwamba seli ambazo zinatakiwa kuipa nywele rangi zimeanza kushindwa kufanya kazi au zimeanza kufa.

Sasa seli za mwili uwa zinaanza kufa kwa sababu ziko programmed kuishi kwa kipindi fulani tu, sasa umri unavyozidi kwenda ndipo seli zako nyingi uanza kufikia ukomo wa kujitengeneza kwa sababu zimekuwa programmed kuwa hivyo. Sasa zile ambazo zimetengenezwa zikaanza kufa zinakosa seli mbadala kwa sababu kiwanda cha kutengenezea seli nacho wafanyakazi wake nao wameanza kuzeeka na kufa. Hapo ndipo magonjwa yanaanza kukunyemelea uzeeni kwa sababu mwili umeanza kukosa wanajeshi wa kutosha kupambana na magonjwa... Ndio maana wazee wengi inakuwa rahisi kuumwa. Au muda mwingine viungo kama moyo, figo na viungo vingine ukosa nguvu kwa sababu seli hazina uwezo tena wa kuchapa kazi kutokana na zimeanza kubaki chache.

Kwa sasa bado hakuna teknolojia ya kufanya seli zisizeeke, sijasemq kufa, nimesema kuzeeka, kwa sababu kufa kuko palepale... Sana sana sayansi itazifanya seli ziweze kuishi muda mrefu tu na kumpeleka binadamu kuchelewa kuzeeka, lakini bado zitazeeka tu na kufa. Lakini Teknolojia ya robots inaweza kufanya mageuzi na akili za binaadam na ufahamu ukaamishiwa kwenye robots. Yani tukawa Cyborg.
Mbuzi naona umeongea takataka kama posti zako nyinyi humu
Yaani umeeongea kama unajadili stori za kijiweni bila hypothesis wala postulation
Basi tu umeamua na mimi nichangie
it is better to remain silent and be thought a fool than to talk and remove all doubt.”
 
Oprah Winfrey hazeeki pia Dolly Parton kajifunze kwao...pia baadhi ya wa Japan
Uzee ni kuanzia miaka 50?, nadhan tusiangalie muonekano. Kikubwa ukifikisha hiyo miaka wewe unahesabika mzee.
Hata uwe na sura ya kitoto
 
Back
Top Bottom