Binadamu tunaishi ili iweje? Au tupo duniani kufanya nini? Why Do We Live?

Binadamu tunaishi ili iweje? Au tupo duniani kufanya nini? Why Do We Live?

TOUGHMAN

New Member
Joined
Aug 24, 2009
Posts
1
Reaction score
11

Bila-shaka hakuna swali lisilo na jibu japokuwa kila jibu litolewalo si lazima liwe sahihi. Waulize swali moja wanafunzi wa chekeachea, shule ya msingi, sekondari na vyuo kwa nini unasoma shule?

Majibu mengi yaliyotolewa yalikuwa majibu ya kunakili kutoka kwa wazazi au walezi wa hao watoto. Wangi wao walisema wanasoma hili maisha yao ya baadaye yawe mazuri. Nilipowauliza nini maana ya maisha mazuri?

Nilipokuwa nasoma chekechea ak.a kindergarten mwalimu alinifundisha kuwa moja toa mbili jibu lake ni haiwezekani. Nilipoingia darasa la kwanza mwalimu huyo huyo wa chekechea akanifundisha kuwa moja toa mbili jibu lake ni (-) hasi moja. Swali moja majibu mawili tofauti lakini yote ni sahihi.

Baada ya maelezo hayo machache nikukaribisheni mtoe maoni yenu katika kujibu swali hilo hapo juu.
 
Nawasiki watu wa imani mbalimbali wakijadili kuwa binadamu hapa duniani ni wapitaji tu na wengine wakitufundisha tujiandae kwa maisha ya milele baada kufa. Je kama kuna maisha baada ya kufa kwanini watu wanamsifia na kumshukuru mungu sana kila wanapoamka asubuhi wakiwa wazima? Kama kuna maisha mengine hapa dunia tumekuja kufanya nini?. Nini hasa sababu ya sisi kuishi hapa duniani?.
 
Last edited by a moderator:
Nawasiki watu wa imani mbalimbali wakijadili kuwa binadamu hapa duniani ni wapitaji tu na wengine wakitufundisha tujiandae kwa maisha ya milele baada kufa. Je kama kuna maisha baada ya kufa kwanini watu wanamsifia na kumshukuru mungu sana kila wanapoamka asubuhi wakiwa wazima? Kama kuna maisha mengine hapa dunia tumekuja kufanya nini?. Nini hasa sababu ya sisi kuishi hapa duniani?.
Ni Mungu pekee anayejua madhumuni ya kutuumba sisi binadamu na kutuleta duniani na kutufanya tuishi kwa kipindi fulani.

Hata hivyo ninachojua Mungu ametuwekea 'speed governer' katika ubongo wetu, ambapo ametuwekea 'limit' ya upeo wa kujua mambo ya Mungu.

Mfano utacrack kichwa chako kutaka kujua inakuwaje Mungu awe Alpha na Omega hutapata majibu.

Vile vile ukitafakari wakati wa uumbaji wake wa dunia na vyote vilivyomo duniani pamoja na sayari zote zinazozunguuka dunia, 'material' ya kuumbia sayari hizi, hutapata majibu, na badala yake utaumiza kichwa tu.

Ukitaka kuthibitisha ukuu wa Mungu ni kuwa hata maScientists, ambao wamekuwa 'wagumu' wa kukiri uwepo wa Mungu, lakini hata wao wanakiri kuwa dunia na vyote vilivyomo duniani na sayari zinazoizunguka, havikuja 'vyenyewe' tu, bali lazima kuna aliyeviumba, yaani CREATOR!!

Kwa hiyo sisi bibadamu tunapowaza maajabu ya Mungu ya uumbaji, tunaishia kutojua zaidi kutokana na Mungu kutuwekea 'speed governer' kwenye bongo zetu na hatimaye tunaishia tu kujisemea kimoyo moyo kuwa, mwacheni Mungu aitwe Mungu!!!!!!!!!!!
 
Haiba ya kuvurugwa tumbo na maswali magumu ni haiba ya kushindwa kuhalalisha ujuzi wa binadamu.

Uchunguzi unahusika mara zote. Imani ni sumu ya ujuzi.

naimani kwamba una maana ila hii lugha uliyotumia sidhani kwamba itamsaidia mleta uzi.
 
Swali zima la "tunaishi ili iweje" lina assume kwamba kuna sababu za kila kitu kuelekea. Kitu ambacho si kweli.

Prove to me that it is not true, na sio longa longa zisizo na mshiko na zilizo pitwa na wakati.

Kila kitu kinasababu, dispute if you can.
 
Haiba ya kuvurugwa tumbo na maswali magumu ni haiba ya kushindwa kuhalalisha ujuzi wa binadamu.

Uchunguzi unahusika mara zote. Imani ni sumu ya ujuzi.

That is your fallacy which can not be proved.
 
I have not found one argument against existential nihilism.

Life must have a meaning, for there to be a purpose.

Kila mmoja wetu ana maana yake ya maisha na hivyo kila mmoja wetu ana "purpose" yake ya kuishi.

Tatizo ni pale kunapokuwa na mila, desturi na imani. Kwamba katika maisha lazima uamini mungu, uende shule, uwe na kazi, uoe/uolewe, uwe na watoto etc. Hivyo vitu kama hivyo vinabebwa na jamii na kufanywa "purpose" ya maisha kwa wote.

Lakini si kweli kwa sababu si kila mtu ana maana moja ya maisha. Mwingine anaweza kusema maisha haya ni a one time shot that's never coming back. Kwa mfano mtu anaweza kuamua kusema hakuna purpose yoyote ya kuishi na kuamua kujiua, mwingine anaweza sema maisha yangu nitasafiri dunia nzima, mwingine nitasoma as much as I can na kuamua kuishi bookstores, etc etc..

So bottom line, life has no objective meaning, it's what you make it.

Hakuna sehemu inayosema binadamu tupo hapa ku-achieve something. So you decide what you want out of this life.
 
Kuna sababu za msingi zilizomleta kila mmoja wetu hapa duniani. Tatizo ni kujua kilichokuleta. Na kama utaishi bila kujua
kilichokuleta, wengine watakutumia ili wakamilishe mipango iliyowaleta.

Mfano :

Kijana anapenda kuwa mhandisi wa mawasiliano lakini kwa sababu amepata alama fulani chuo kinamwambia huko
unakotaka kumejaa labda usome kemia na kijana hana uwezo wa kifedha. Huyu kijana anenda kusoma kemia na anamaliza stashahada au shahada, anaanza kufanya kazi kama mkemia. Lakini kumbe laiti kama angesomea mambo ya mawasiliano angeweza kufanya maajabu katika taaluma hiyo na dunia ikatambua uwepo wake. Vivo hivyo unakuta kijana kapata daraja la kwanza na pointi tatu katika kidato cha sita. Anataka kusoma uhandisi fulani na anakipaji cha hali ya juu katika hilo ila tu kwa sababu wanaofaulu sana huwa wanaenda kusoma kozi fulani na ye anafuata mkumbo na kuishia kutafuta mkate wake wa kila siku na utaalamu huo.

Wapo watu wamekuja hapa duniani kama mitihani kwa wengine, wapo waliokuja kutuachia teknolojia fulani, wapo waliokuja kutuonyesha mambo ambayo tulidhani hayawezekani kwenye michezo, siasa, biashara, sayansi, n.k.
 
Kuna sababu za msingi zilizomleta kila mmoja wetu hapa duniani.

Ni sababu zipi hizo na umejuaje zina-apply kwa kila mmoja wetu?

Tatizo ni kujua kilichokuleta.

Ni kitu gani kimetuleta? Umejuaje?

Na kama utaishi bila kujua kilichokuleta, wengine watakutumia ili wakamilishe mipango iliyowaleta.

Unajuaje wewe hutumiki kukamilisha mipango ya wengine?
 
Ni sababu zipi hizo na umejuaje zina-apply kwa kila mmoja wetu?



Ni kitu gani kimetuleta? Umejuaje?



Unajuaje wewe hutumiki kukamilisha mipango ya wengine?

Hehehe, introvert unanifurahisha. By the way na mi ni intovert wa ISFJ.
Haya turudi kwenye mada,

1. Sababu hizo unatakiwa uzijue wewe mwenyewe na sio mimi. Hata nikikwambia kuwa wewe inabidi
uachane na A na uanze kushughulika na B(ndiko mahala pako) bado jukumu la kuridhia litabaki kwako
wewe mwenyewe. Kuna watu wametajirika kwa vipaji vyao na kuna ambao wametajirika katika maeneo
ambayo hawana vipaji. Furaha ya watu hawa wawili ni tofauti kabisa, hata ufanisi wao haufanani kabisa.
Ukifanya kazi iliyo kuleta duniani kwanza utakuwa na furaha sana halafu vitu kama pesa, n.k havita kuwa
sababu ya msingi itayokufanya ubadili kazi hiyo. Hujawahi kuona mzazi anauza duka, watoto wake wanamfungulia
biashara kubwa lakini yeye anang'ang'ania kuuza duka ? Ni wa sababu anona pale ndio mahala pale.

2. Isingewezekana kila mtu awe ni bosi au mtawala hapa duniani. Nani angekuwa mtumwa? Hivyo basi hata kama mimi
nasaidia kutimiza malengo ya mtu mwingine, huwezi jua sababu hata ROCKET SCIENCE sio teknolojia ya mtu mmoja.
Kwa hiyo wengine wamekuja kukamilisha mambo ya watu wengine na ndiyo kazi iliyo waleta. Usiseme najicontradict!
Hapa simaanishi NASA wanakutumia sababu tu wanajua kichwani uko vizuri~ hapana. Bali ni ridhio lako wewe mwenyewe na ni moja ya ndoto zako kufanya kazi na NASA. Kwa lugha nyingine unafurahia na unakipaji kikubwa katika jukumu hilo.
 
Back
Top Bottom