Nimewaangalia simba jana wakifungwa lakini sikushtuka kwa sababu matatizio wanayalea wenyewe. Kwanza wachezaji hawana morali kabisa ukiondoa kichuya, nyoni na mlipili hao waliobaki walikuwa wanacheza kama wamelazimishwa. Pili Omog huwa hana mbinu mbadala kabisa. timu ikibanwa hautokaa uone imebadilisha mbinu. Tatu simba haina washambuliaji wa mwisho wenye vipaji binafsi vya ufungaji au hata wenye kufosi goli lipatikane. Akishakosekana Okwi au akibanwa na mabeki simba kwishney.
Makosa mawili makubwa viongozi wa simba waliyofanya ni kumuondoa Mayanja na kumuacha Omog. Kosa lingine ni kupoteza muda mwingi kumsajili kwasi badala ya kushughulikia washambuliaji wapya wa kumpa boko changamoto na kuiewka timu kambini mapema kujiandaa na mechi dhidi ya green wariors.
Simba ukiiangalia vizuri dakika zake ni 60 tu wanaanza poteana hamna pumzi wala stamina hili Omog limemshinda kabisa. wakikutana na timu zinazocheza mpira wa nguvu na zenye pumzi hasa timu za jeshi simba hawanaga ujanja. Pia hawachezi kitimu kabisa kila mtu anacheza anavyojua yeye.
Kama kweli wanataka ubingwa mwaka huu wamtimue Omog wamrudishe mtaalamu mayanja. Vile vile wamtimue yule msemaji wao sijui naitwa nani nimesahau jina lake. Ila kwa kukosa washambuliaji mahiri wa kati ubingwa naona kama utarudi yanga tena au kwenda azam.
Makosa mawili makubwa viongozi wa simba waliyofanya ni kumuondoa Mayanja na kumuacha Omog. Kosa lingine ni kupoteza muda mwingi kumsajili kwasi badala ya kushughulikia washambuliaji wapya wa kumpa boko changamoto na kuiewka timu kambini mapema kujiandaa na mechi dhidi ya green wariors.
Simba ukiiangalia vizuri dakika zake ni 60 tu wanaanza poteana hamna pumzi wala stamina hili Omog limemshinda kabisa. wakikutana na timu zinazocheza mpira wa nguvu na zenye pumzi hasa timu za jeshi simba hawanaga ujanja. Pia hawachezi kitimu kabisa kila mtu anacheza anavyojua yeye.
Kama kweli wanataka ubingwa mwaka huu wamtimue Omog wamrudishe mtaalamu mayanja. Vile vile wamtimue yule msemaji wao sijui naitwa nani nimesahau jina lake. Ila kwa kukosa washambuliaji mahiri wa kati ubingwa naona kama utarudi yanga tena au kwenda azam.