John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,374
Tilly Smith akiwa na umri wa miaka 10, kwenye mapumziko katika Ufukwe wa Maikhao nchini Thailand mwaka 2004, aliona kuna kitu hakipo sawa ufukweni hapo.
Ilikuwa zimepita wiki mbili tu tangu aliposoma katika somo la Geography kuhusu Tsunami nchini kwao England, hivyo kwa kukumbuka kile alichofundishwa akaona kuna kitu hakipo sawa ufukweni hapo.
Hivyo, haraka sana binti huyo akawaambia watu wa familia yake na watalii wengine zaidi ya 100 wakasikia kile alichokizungumza wakaondoka eneo hilo, japokuwa awali mama yake alitaka kukataa kuondoka na hata alipokubali akikuwa mtu wa mwisho katika famili yake kuondoka ufukweni.
Muda mfupi baada ya wao kuondoka ufukweni hapo kukatokea Tsunami kubwa ambayo iliua idadi kubwa ya watu na kuharibu mali nyingi. (inadawa zaidi ya watu 250)
Alipokuja kuulizwa baadaye alisema alijifunza darasani kile kilichotokea katika Kisiwa cha Hawaii mwaka 1946, hivyo akajua kuwa Tsunami inaweza kusababishwa na tetemeko la ardhi na mlipuko wa volkano.
Mwaka mmoja baada ya tukio hilo la Ufukwe wa Maikhao, binti huyo alipewa tuzo maalum nchini Uingereza kwa ushujaa wake huo, kwa sasa ana umri wa miaka 28.
Ilikuwa zimepita wiki mbili tu tangu aliposoma katika somo la Geography kuhusu Tsunami nchini kwao England, hivyo kwa kukumbuka kile alichofundishwa akaona kuna kitu hakipo sawa ufukweni hapo.
Hivyo, haraka sana binti huyo akawaambia watu wa familia yake na watalii wengine zaidi ya 100 wakasikia kile alichokizungumza wakaondoka eneo hilo, japokuwa awali mama yake alitaka kukataa kuondoka na hata alipokubali akikuwa mtu wa mwisho katika famili yake kuondoka ufukweni.
Muda mfupi baada ya wao kuondoka ufukweni hapo kukatokea Tsunami kubwa ambayo iliua idadi kubwa ya watu na kuharibu mali nyingi. (inadawa zaidi ya watu 250)
Alipokuja kuulizwa baadaye alisema alijifunza darasani kile kilichotokea katika Kisiwa cha Hawaii mwaka 1946, hivyo akajua kuwa Tsunami inaweza kusababishwa na tetemeko la ardhi na mlipuko wa volkano.
Mwaka mmoja baada ya tukio hilo la Ufukwe wa Maikhao, binti huyo alipewa tuzo maalum nchini Uingereza kwa ushujaa wake huo, kwa sasa ana umri wa miaka 28.