Biriani ya nyama

Biriani ya nyama

Hahahaha hupasuki tumbo bwana..m
Laa laa...kwa mtindo huu uloanzisha hakuna Msalliye kwa siye tunaoendekeza mloo usitupite !! hapatapona mtu!!
Yaani mwezi mzima wateremsha mapochpocho 5 stars bila mapumziko..... Mmmh unania mbaya binti Nass!!
Tiisllam yedeiki !!
 
Laa laa...kwa mtindo huu uloanzisha hakuna Msalliye kwa siye tunaoendekeza mloo usitupite !! hapatapona mtu!!
Yaani mwezi mzima wateremsha mapochpocho 5 stars bila mapumziko..... Mmmh unania mbaya binti Nass!!
Tiisllam yedeiki !!

Hahahaaahha.....wewe kula tu mwili haujengwi kwa matofali lol
 
farkhina kuna chakula kimoja nimessahau jina lake nlishawahi kuekezwa siku moja kupika miaka mingi sana kama unajua nisaidie nakitamaniii sana.
Zinakuwa kama mkate wa ufuta ila hauweki hamira unabonda bonda unga ila unakandia maziwa sijui tui la nazi sikumbuki unaweka nyama na njegere katikati size zinakuwa kama mkate wa ufuta halafu unazikaanga kama na mafuta mengi kama ya kukaangia maandazi.Nitaaamu sana kama umeelewa naomba nisaidie mupenzi.
Mwaaaa mwaaa mwaaa
 
Last edited by a moderator:
farkhina kuna chakula kimoja nimessahau jina lake nlishawahi kuekezwa siku moja kupika miaka mingi sana kama unajua nisaidie nakitamaniii sana.
Zinakuwa kama mkate wa ufuta ila hauweki hamira unabonda bonda unga ila unakandia maziwa sijui tui la nazi sikumbuki unaweka nyama na njegere katikati size zinakuwa kama mkate wa ufuta halafu unazikaanga kama na mafuta mengi kama ya kukaangia maandazi.Nitaaamu sana kama umeelewa naomba nisaidie mupenzi.
Mwaaaa mwaaa mwaaa

Wacha nkifikirie then ntakwambia ni nini...kama nakifahamu ntakuambia
 
Last edited by a moderator:
Mahitaji

Nyama nusu

Chumvi kiasi

Mafuta 1 Kikombe

Vitunguu maji 3 vikubwa

Nyanya 3 kubwa

Nyanya kopo

Thomu 1 table spoon

Tangawazi 1 table spoon

Pilipili mbichi iliyosagwa 1 tea spoon

Kotmiri (giligilani) iliyokatwa 2 Vijiko vya chakula

Viazi 6

Uzile wa unga 1table spoon

Mtindi ¼ Kikombe cha chai

NAMNA YA KUTAYARISHA KUPIKA

1. Kwenye karai au (sufuria) mimina mafuta Yakishapata moto mimina vitunguu vikaange mpaka viwe rangi ya hudhurungi. Vitowe viweke pembeni.

2. Kaanga viazi na viweke pembeni.

3. Chukua sufuria tia nyama, thomu, tangawizi, pilipili, nyanya, nyanya ya kopo, mtindi. Chemsha mpaka iive.

4. Tia vile vitungu ulioyovikaanga, tia viazi, uzile, kotmiri na yale mafuta uliokaangia vitunguu kama ¼ kikombe, acha moto mdogo mdogo kama ¼ saa, epua weka pembeni.

VIPIMO VYA WALI

Mchele kg 1

Mdalasini mzima wa vijiti

Zafarani ½ kijiko cha chai

Rangi ya biriani ¼ Kijiko cha chai

Mafuta yaliyokaangiwa vitunguu ½ Kikombe

Chumvi kiasi

Zabibu kavu.

Roweka zafarani na rangi kwenye kikombe na ¼ kikombe cha maji. Roweka kabla ya robo saa.

NAMNA YA KUTAYARISHA

1. Osha mchele uroweke kwenye maji muda wa dakika 20.

2. Chemsha maji kwenye sufuria kama magi 10.

3. Tia mdalasini.

4. Yakishachemka unatia mchele,chemsha usiive sana, unamwaga maji.

5. Unamimina tena ule mchele ½ yake kwenye sufuria, unatia rangi na zafrani kidogo na zabibu halafu unamimina mchele uliyobakia unatia rangi iliyobakia.

6. Mafuta yake unayachemsha mpaka yachemke unamimina juu ya mchele, unarudisha motoni unaweka moto mdogo ukisha kuiva, tayari kupakuliwa.

7. Unapakuwa wali unaweka chini kwenye sahani na juu yake sosi ya nyama.

Umesomeka mamaaa.
Uzile ndio nini,hapo sijaelewa bado. Naomba unilekeze duka/mahali hapa dsm ambapo naweza pata spices/viungo vya kunogesha maanjumati ambavyo often unavitajaga humu jamvini km hiyo uzile,zafarani,zabibu kavu e.t.c
 
Umesomeka mamaaa.
Uzile ndio nini,hapo sijaelewa bado. Naomba unilekeze duka/mahali hapa dsm ambapo naweza pata spices/viungo vya kunogesha maanjumati ambavyo often unavitajaga humu jamvini km hiyo uzile,zafarani,zabibu kavu e.t.c

Uzile ni bizari ya pilau...

Maduka ya viungo kwa dsm sifaham ngoja wenyewe wa dar waje watakuambia
 
Umesomeka mamaaa.
Uzile ndio nini,hapo sijaelewa bado. Naomba unilekeze duka/mahali hapa dsm ambapo naweza pata spices/viungo vya kunogesha maanjumati ambavyo often unavitajaga humu jamvini km hiyo uzile,zafarani,zabibu kavu e.t.c

Ni binzari nyembamba
 
Nenda kariakoo, pale Shimoni, kwa nyuma kuna solo la nje, wanauza viungo vya kila aina mule ndani, Pia upande wa pili ule upande wa maduka ya Tahfif kuna duka moja kubwa sana la viungo, limeandikwa SPICE....something....hutokosa kiungo chochote pale.

Kila la kheri Ndesalee
 
Last edited by a moderator:
Karibu sana

Sasa hv nishakaribia humu jamvini. Mana nimechoka kula migahawani kila siku.
Wkt nipo primary to O-Level mamangu alikuwa ananifundishaga kupika. Nashukuru jikoni mimi sio mgeni sana,ingawa nimezaliwa na kukulia mjini.
 
Nenda kariakoo, pale Shimoni, kwa nyuma kuna solo la nje, wanauza viungo vya kila aina mule ndani, Pia upande wa pili ule upande wa maduka ya Tahfif kuna duka moja kubwa sana la viungo, limeandikwa SPICE....something....hutokosa kiungo chochote pale.

Kila la kheri Ndesalee

Nasubiri kukuche vizuri niende maeneo hayo leo. Ila naomba ni PM spices ambazo ni vzr nikawa nazo ndani kwa ajili ya mambo ya maakuli mbali mbali sio based on pilau tu.
 
Last edited by a moderator:
Sasa hv nishakaribia humu jamvini. Mana nimechoka kula migahawani kila siku.
Wkt nipo primary to O-Level mamangu alikuwa ananifundishaga kupika. Nashukuru jikoni mimi sio mgeni sana,ingawa nimezaliwa na kukulia mjini.[/QUOTE

Usijali basi ntakua naku mention nikiweka mapishi mapya nawe uwe unatuwekea makulati yako ati lol
 
Back
Top Bottom