Birmingham City masharti lukuki kutua Dar

Birmingham City masharti lukuki kutua Dar

kilimasera

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2009
Posts
3,068
Reaction score
277
MABINGWA wa Kombe la Carling nchini England, Birmingham City, wanatarajiwa kutua nchini Julai mwaka huu kwa ziara maalumu ya kimichezo ambapo watakipiga na vigogo wa soka nchini, Simba na Yanga, jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Simba, Alhaj Ismail Aden Rage, alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa baadhi ya maofisa wa juu wa timu hiyo, akiwemo kocha msaidizi, Andy Watson, pamoja na daktari Ian Mc Guinness, wanatarajiwa kuwasili nchini Mei 9 kwa ajili ya kukagua Uwanja na Hoteli.

Rage alisema, ujumbe huo utakagua Uwanja wa Taifa utakaotumika, pamoja na hoteli ya Kilimanjaro Kempinski ili kuona kama vinakidhi vigezo vya timu hiyo, ambayo itaambatana na mashabiki wasiopungua 1,000 ambao watajilipia gharama za hoteli na uwanjani.

Alisema, usiku wa Julai 7, Birmingham itakipiga na Simba kabla ya jioni ya Julai 12 kukipiga na mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2010/2011, Yanga.

“Tunafurahi kupata wasaa wa kuwa wenyeji wa timu kubwa kama hiyo, ujio wao huo utafungua mipaka ya kimataifa baina yetu na wao…tayari tumeshazungumza na watu wa Wizara ya Maliasili na Utalii juu ya ujio huo,” alisema Rage.

Katika hatua nyingine, Rage alisema mkutano mkuu wa mwaka wa wanachama wa klabu hiyo, unatarajiwa kufanyika Mei 15 katika Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam na wanachama watakaoruhusiwa kushiriki ni wale ambao watakuwa wamelipa ada ya mwaka ambayo ni sh 12,000 pamoja na ile ya uwanja sh 20,000 na kwamba malipo hayo yafanywe katika akaunti ya wanachama.

Pia Rage alisema, uongozi umetoa saa 48 kwa wapangaji wanaotaka kuendelea kupanga katika jengo lao kuwasiliana na uongozi, kinyume cha hapo watakwenda kuomba kibali chama mahakama kwa ajili ya kuwaondoa kwa nguvu.

Wakati huo huo, beki wa timu hiyo Kelvin Yondani amewasilisha barua ya kuomba msamaha kutokana na utovu wa nidhamu huku akisihi arudishwe kundini, wakati mshambuliaji Mussa Hassan Mgosi ambaye naye aliadhibiwa kutokana na kukiuka mkataba kwa kuzungumza sana na vyombo vya habari, akitakiwa kusoma upya mkataba wake na kutoa maelezo.
 
Birmingham City masharti lukuki kutua Dar
• Rage aishangaa Yanga, aanika Nchunga ndiye aliyemwaga wino

na Juma Kasesa


amka2.gif
WAKATI benchi la Ufundi la mabingwa wa Carling Cup, Birmingham City ya England, likitarajiwa kutua jana usiku, uongozi wa klabu hiyo umeanika masharti lukuki kabla ya kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Simba na Yanga Julai mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, alisema benchi hilo la ufundi linakuja kwa ajili ya kuja kukagua uwanja, hoteli na hospitali ambavyo watavitumia wakitua jijini kwa michezo hiyo.
Akifafanua kuhusu masharti hayo, Rage alisema mabingwa hao wa Carling, wanataka kucheza mechi hizo katika uwanja usio wa nyasi za bandia, huku ukisisitiza kuwa ziwe na urefu usiozidi sentimeta sita.
Alisema, licha ya kugoma kucheza uwanja wa nyasi bandia, pia Birmingham wanataka kufikia katika hoteli yenye hadhi ya kimataifa na kutibiwa katika Hospitali ya Agakhan, ambayo benchi hilo la ufundi linatarajiwa kwenda kufanya ukaguzi ili kujiridhisha kabla ya timu hiyo kuja jijini Dar es Salaam.
Bechi hilo la ufundi linaongozwa na meneja msaidizi na daktari wa timu hiyo kwa ajili ya kufanya ukaguzi, tayari kwa mechi hizo za kirafiki, ambazo zitakuwa ni sehemu yao ya maandalizi kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu nchini England.
Birmingham ambao wako katika nafasi ya 16 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England ambao hivi karibuni walilitwaa Kombe la Carling baada ya kuifunga Arsenal 1-0 kwenye Uwanja wa Wembley, bao lao likifungwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Nigeria, Obafemi Martins, itaanza kutupa karata yake kwanza kwa kukipiga na Simba Julai 12 kabla ya kuvaana na mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga, Julai 14 Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Katika hatua nyingine, Rage alisema, ameshangazwa na hatua ya uongozi wa Yanga kusema hauna taarifa za michezo hiyo, ilhali mwenyekiti wake, Lloyd Nchunga, ndiye aliyesaini makubaliano ya kucheza mechi hizo.
 
ingekuja Man U je, si tungedeki hotel wanayofikia kwa ulimi, chakula chao kitoke england kwa ndege maalum - duh kazi ipo.

Kitimu chenyewe kipo hatarini kushuka daraja, makeke kibao.
 
kisa sie hatuonekani kwenye 'ramani ya soka' ndio maana hata timu isiyo na mashiko kwao kwetu yataka kututoa kamasi!
 
ingekuja Man U je, si tungedeki hotel wanayofikia kwa ulimi, chakula chao kitoke england kwa ndege maalum - duh kazi ipo.

Kitimu chenyewe kipo hatarini kushuka daraja, makeke kibao.
Hahaha lol
 
Birmingham City masharti lukuki kutua Dar
• Rage aishangaa Yanga, aanika Nchunga ndiye aliyemwaga wino

na Juma Kasesa


amka2.gif
WAKATI benchi la Ufundi la mabingwa wa Carling Cup, Birmingham City ya England, likitarajiwa kutua jana usiku, uongozi wa klabu hiyo umeanika masharti lukuki kabla ya kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Simba na Yanga Julai mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, alisema benchi hilo la ufundi linakuja kwa ajili ya kuja kukagua uwanja, hoteli na hospitali ambavyo watavitumia wakitua jijini kwa michezo hiyo.
Akifafanua kuhusu masharti hayo, Rage alisema mabingwa hao wa Carling, wanataka kucheza mechi hizo katika uwanja usio wa nyasi za bandia, huku ukisisitiza kuwa ziwe na urefu usiozidi sentimeta sita.
Alisema, licha ya kugoma kucheza uwanja wa nyasi bandia, pia Birmingham wanataka kufikia katika hoteli yenye hadhi ya kimataifa na kutibiwa katika Hospitali ya Agakhan, ambayo benchi hilo la ufundi linatarajiwa kwenda kufanya ukaguzi ili kujiridhisha kabla ya timu hiyo kuja jijini Dar es Salaam.
Bechi hilo la ufundi linaongozwa na meneja msaidizi na daktari wa timu hiyo kwa ajili ya kufanya ukaguzi, tayari kwa mechi hizo za kirafiki, ambazo zitakuwa ni sehemu yao ya maandalizi kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu nchini England.
Birmingham ambao wako katika nafasi ya 16 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England ambao hivi karibuni walilitwaa Kombe la Carling baada ya kuifunga Arsenal 1-0 kwenye Uwanja wa Wembley, bao lao likifungwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Nigeria, Obafemi Martins, itaanza kutupa karata yake kwanza kwa kukipiga na Simba Julai 12 kabla ya kuvaana na mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga, Julai 14 Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Katika hatua nyingine, Rage alisema, ameshangazwa na hatua ya uongozi wa Yanga kusema hauna taarifa za michezo hiyo, ilhali mwenyekiti wake, Lloyd Nchunga, ndiye aliyesaini makubaliano ya kucheza mechi hizo.
BIRMINGHAM CITY ARE PLANNING PRE-SEASON TPIP TO TANZANIA
first team coach.Andy Watson and Chief medical officer Ian Mc Guinnes have travelled to Africa to inspect facilities. Birmingham are expected to undertake a four days trip,although details have not yet been finalised.Tanzania top flight sides Simba and Yanga could provide opposition at the National stadium in Dar es salaam. Watson said 'The people of Tanzania that we have met have been very hospitable and kind.For what we've seen of country so far it looks an amazing place.We have been made aware of how much the people of Tanzania love their football-especially the Premier league when everythng is fully in the place we look forward to coming in july and playing."
source THE SUN 11/5/2011​
 
0,,10412%7E9665358,00.jpg
Blues are set to visit the African country of Tanzania on pre-season tour this July.
Although exact dates and details are yet to be confirmed the four-day trip is expected to include a game against one of the Tanzanian top flight sides Simba and Yanga, or possibly both, in the National Stadium (pictured, above) in Dar-es-Salaam.
0,,10412%7E9665342,00.jpg

First team coach Andy Watson and chief medical officer Ian McGuinness are currently in the country inspecting facilities.
Watson told bcfc.com: "The people of Tanzania that we have met have been very hospitable and kind and from what we've seen of the country so far it looks an amazing place.
"We have been made aware of just how much the Tanzanian people love their football - especially the Barclays Premier League - and when everything is fully in place we look forward to coming back in July and playing."
As and when more details are available you will be able to find about them first here at bcfc.com.
0,,10412%7E9665349,00.jpg
 
ingekuja Man U je, si tungedeki hotel wanayofikia kwa ulimi, chakula chao kitoke england kwa ndege maalum - duh kazi ipo.

Kitimu chenyewe kipo hatarini kushuka daraja, makeke kibao.

Ndo hadhi wanayostahili, kwa akili yako ulitaka wafikie wapiwapi guest house?
 
ingekuja Man U je, si tungedeki hotel wanayofikia kwa ulimi, chakula chao kitoke england kwa ndege maalum - duh kazi ipo.

Kitimu chenyewe kipo hatarini kushuka daraja, makeke kibao.

Afya na Usalama wa mchezaji ni kitu muhimu sana katika professional football. Usikute hata Madrid ya jk haikuja kwa vile walichunguza na kukuta hatuko vizuri iwapo ingetokea Sergio Ramos kaumizwa na Canavaro.
 
Hawa waandishi wenu wa habari wameona uvivu hata ku-google matokeo halisi ya fainali ya carling cup? Au wamefanya hesabu ya 2-1=1?
 
Rage kishaanza kulikoroga,mpaka alinywe.Asije kuanza sanaa zake.mara wameghairi,mara nini sijui.Au anataka umaarufu tu hamna kitu?
 
Najaribu kujiuliza lengo hasa la ziara hii na mantiki yake, huenda wanakuja kugonga kikombe au kutalii na njia rahisi ni minajiri ya kukipiga nchini, sijasikia kama hizo hoteli nani atagharamika, isije kuwa mambo ya Brazil hapa.........
 
ingekuja Man U je, si tungedeki hotel wanayofikia kwa ulimi, chakula chao kitoke england kwa ndege maalum - duh kazi ipo.

Kitimu chenyewe kipo hatarini kushuka daraja, makeke kibao.

Kweli Man U ni mashetani na mashetani ni mapepo, mnayatumikia na kuyashabikia mapepo, tena nayo yanawatumikisha thats y mko tayari kupiga deki kwa ulimi kwa kuwa nyie ni watumwa wa mashetani mekundu
 
Back
Top Bottom