Biteko afuta likizo zote za Watumishi wa TANESCO

Biteko afuta likizo zote za Watumishi wa TANESCO

Siku mkiwaondoa wakimbizi, mgawo wa umeme utaisha
 
Eti anafuta likizo za wafanyakazi, kwa kutumia sheria gani?
Oneni sasa juu ya umuhimu wa Katiba mpya.

Kama mfanyakazi Ali book likizo yake watarudisha Pesa zaje?
 
Naibu Waziri Mkuu, Dk Doto Biteko ametangaza kufuta likizo kwa watumishi wote wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) akiwataka wote wawe kazini kukabiliana na changamoto ya upungufu wa umeme.

Amesema hakuna mtumishi wa Tanesco atatakiwa kwenda likizo wakati huu wa changamoto ya mgawo wa umeme na kwamba, kila mmoja kwenye eneo lake atatakiwa kufanya kazi kwa bidii.

Dk Biteko, ambaye pia ni Waziri wa Nishati ametoa agizo hilo leo Ijumaa, Februari 23, 2024 wakati alipotembelea chanzo cha kuzalisha umeme cha Kidato mkoani Morogoro.

Naibu Waziri Mkuu huyo yupo kwenye ziara kukagua vyanzo vya kuzalisha umeme, kuangalia shughuli za uzalishaji ikiwa ni mkakati kumaliza changamoto ya upungufu wa umeme nchini.

Hatua hiyo ya Dk Biteko imetokana na kupewa taarifa kwamba, Meneja wa Tanesco Mkoa wa Morogoro, kuwa amekwenda likizo.

“Huu ni muda wa kukimbiza kutatua changamoto zilizopo mbele yetu. Nitoe wito kwa uongozi wa Tanesco kuwa hakutakuwa na likizo kipindi hiki ambacho watanzania wanakabiliwa na changamoto ya umeme.

Hakuna likizo tena kuanzia sasa hivi kwenda mbele kwa mtu yeyote anayefanya kazi Tanesco. Nilivyosema Tanesco hamtalala wakati huu wa mgawo nilikuwa naaminisha, haiwezekani tuko kwenye changamoto halafu kuna wengine wanataka kulala.

Sisi wenyewe tunazunguka kila mahali kuhakikisha wananchi wanapata umeme. Katika hili tutachukua hatua kwa aliyeidhinisha likizo n ahata huyo aliyeomba likizo wakati huu ametoa wapi ujasiri,” amesema Dk Biteko.

Itasaidia nini

Huyu ni failure
 
Afadhali waziri uwazuwie likizo,hawa ndiyo wanachangia,sisi kukaa gizani kisa mgao,wangepunguziwa na mishahara + posho
 
Sijui tupo episode ya ngapi, ila title ya episode ni "Kufuta likizo"
 
Hiyo inaweza ikawa suluhu kweli??
Kwani ni upungufu au ukosefu? Kama vyanzo au miundombinu havina maji au nyenzo, hii haiwezi kusaidia
Walibeza juhudi za marehemu kwenye JNHPP waliupiga vita mradi, sasa Mungu anawaonesha msibeze neema zake
 
Afadhali waziri uwazuwie likizo,hawa ndiyo wanachangia,sisi kukaa gizani kisa mgao,wangepunguziwa na mishahara + posho
Pitia hata comments za wadau ujifunze kitu, haihitaji hata elimu ya chekechea kujua hiyon hatua ya kihuni kuuhadaa umma.

Hatua za ajabu ajabu huchukuliwa na viongozi wahuni kuwahadaa raia wengi wenye uwezo duni wa kufikiri.

Huwezi kutatua tatizo la umeme lililopo nchi hii kwa kuwazuia watumishi haki zao za kisheria, ni ujuha.

Yeye ndiye jipu namba moja hapo ila hatumbuliki, atavumiliwa kwa sababu ya uzembe wa serikali na kulinda heshima ya licheo hilo jingine la ajabu ajabu alilopewa
 
Hiyo inaweza ikawa suluhu kweli??

Kwenye hili yupo sahihi. Tena wafanyakazi wote wa TANESCO walistahili kulipwa nusu mishahara mpaka siku umeme utakapokuwa wa uhakika.
 
Na VYAMA vya wafanyakazi vimekaa kimya tuh,vinasubiri mei mosi waandae miwaraka ya kuisifu serikali badala ya kusimama na wanachama wao,hata wakikaa miaka kumi wasiende likizo tatizo Hilo kwani litaisha?
 
Naibu Waziri Mkuu, Dk Doto Biteko ametangaza kufuta likizo kwa watumishi wote wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) akiwataka wote wawe kazini kukabiliana na changamoto ya upungufu wa umeme.

Amesema hakuna mtumishi wa Tanesco atatakiwa kwenda likizo wakati huu wa changamoto ya mgawo wa umeme na kwamba, kila mmoja kwenye eneo lake atatakiwa kufanya kazi kwa bidii.

Dk Biteko, ambaye pia ni Waziri wa Nishati ametoa agizo hilo leo Ijumaa, Februari 23, 2024 wakati alipotembelea chanzo cha kuzalisha umeme cha Kidato mkoani Morogoro.

Naibu Waziri Mkuu huyo yupo kwenye ziara kukagua vyanzo vya kuzalisha umeme, kuangalia shughuli za uzalishaji ikiwa ni mkakati kumaliza changamoto ya upungufu wa umeme nchini.

Hatua hiyo ya Dk Biteko imetokana na kupewa taarifa kwamba, Meneja wa Tanesco Mkoa wa Morogoro, kuwa amekwenda likizo.

“Huu ni muda wa kukimbiza kutatua changamoto zilizopo mbele yetu. Nitoe wito kwa uongozi wa Tanesco kuwa hakutakuwa na likizo kipindi hiki ambacho watanzania wanakabiliwa na changamoto ya umeme.

Hakuna likizo tena kuanzia sasa hivi kwenda mbele kwa mtu yeyote anayefanya kazi Tanesco. Nilivyosema Tanesco hamtalala wakati huu wa mgawo nilikuwa naaminisha, haiwezekani tuko kwenye changamoto halafu kuna wengine wanataka kulala.

Sisi wenyewe tunazunguka kila mahali kuhakikisha wananchi wanapata umeme. Katika hili tutachukua hatua kwa aliyeidhinisha likizo n ahata huyo aliyeomba likizo wakati huu ametoa wapi ujasiri,” amesema Dk Biteko.
Sasa kama kuna changamoto ya kimfumo kwenye distribution network, inayohitaji uwekezaji mkubwa kutoka serikalini na zaidi ya mwaka mmoja wa matengenezo, kumnyima Mfagizi wa TANESCO Morogoro kwenda likizo yake kutasaidia nini hapo?
 
Kwenye hili yupo sahihi. Tena wafanyakazi wote wa TANESCO walistahili kulipwa nusu mishahara mpaka siku umeme utakapokuwa wa uhakika.
Wafanyakazi wengine wa TANESCO mtawaonea tu.

Kuna matatizo ya kimfumo kutoka serikalini huko.

Serikali inafanya biashara ya umeme kijamaa, haiuzi umeme kwa bei halisi, Zanzibar wana deni sugu la umeme hawalipi, taasisi za serikali zenyewe zina madeni sugu hazilipi, wananchi wanapenda umeme wa bei chee, mifumo ya umeme inachakaa bila kufanyiwa matengenezo.

Umeme ukiwa unakatika kwa sababu hizo za kimfumo, mfanyakazi wa ngazi ya kati au chini TANESCO utamlaumu vipi hapo?
 
Back
Top Bottom