Hawa BM hawasikii wala nini. Mimi niliambiwa niripoti saa moja, hadi saa hii ni 09:15 gari halijafika. Kama hii biashara hawaiwezi wakalime matikiti maji turiani huko. Shenzi taipuOh okay sawa.wamekuckia
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hawa BM hawasikii wala nini. Mimi niliambiwa niripoti saa moja, hadi saa hii ni 09:15 gari halijafika. Kama hii biashara hawaiwezi wakalime matikiti maji turiani huko. Shenzi taipuOh okay sawa.wamekuckia
Wawekezaji wa ndani hao. Walindwe kwa wivu mkubwaNikiri kuwa nimekuwa mpenzi wa BM Coach kwa muda mrefu sasa ila hili la safari hii limeanza kunichefua.
Alhamisi ya tarehe 07/09/2023 nilisafiri na basi la 1.30 asubuhi. Mshangao wa kwanza ni kutokuta basi nililoahidiwa kwenye tiketi kwa kiwango cha nauli. Nilikata basi la 40,000 likaja la 37,000. Wakaomba radhi wakaturudishia 3,000 tukapotezea.
Kurudi 10/09/ 2023 Basi linalopita moshi saa 3 asubuhi jambo lile likajirudia bila hata samahani. KIBAYA ZAIDI HATA CHENJI YEU HATUKUPEWA. Hatujui ni mmiliki/meneja/ au konda aliyepita na chenji yetu. MZEE ANGALIA WATU WAKO. Namba zetu wanazo. Watupe chenji zetu.
Jambo lingine baya ni kuanza kujaza watu. Haswa hapo mbele....tukiwauliza mara oo ndugu wa askari, mara oo staff...haina hata maana kukata siti za mbele... unaishia kuangalia vichogo vya watu.
Lililonitia shaka ni hii biashara ya vifurushi pori anavyopewa konda kabla ya kuondoka na watu wanaomsubiri njiani kumpa na kupokea.... MZEE BM angalia magari yako yasigeuzwe punda wa unga.... vifurushi vipite ofisini. Waache njaa.
La mwisho. Simu za madereva. Ni nyingiiiiii. Kusogoa njia nzima. Wapunguze...ndio zibaki zile muhimu na zingine awaambie tu , nadrive...niakupigia... watu watakuja pokea simu za msiba watubwage....ohooo...
Au mpaka tupeleke ushahidi LATRA? Ya nini yote hayo?