KERO Boda boda waache kupita katika njia za watembea kwa miguu

KERO Boda boda waache kupita katika njia za watembea kwa miguu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Pendragon24

Member
Joined
Aug 8, 2018
Posts
68
Reaction score
97
Katika kuadhimisha wiki ya nenda kwa usalama barabarani 2024.

Tuitumia wiki hii kuwalinda watu wanaotembea kwa miguu katika njia maalumu zilizotengenezwa kwa ajili ya wao kutembea kwa uhuru.

Maana wapo boda boda na baadhi ya bajaji ambao sio wastaarabu huacha njia zao na kutumia njia maalumu za watembea kwa miguu kupitisha vyombo vyao vya usafiri tena kwa spidi isiyokuwa ya kawaida.

Hali hii inapelekea watembea kwa miguu wengi sana kukosa amani wakiwa wanatembea katika njia hizo saa nyingine kugongwa na kusukumiwa njia kuu ambapo magari yanapita kwa kasi sana.

Yaani boda boda anaacha njia kuu aliyotakiwa kupita na kuja kutumia njia za watembea kwa miguu ili awahi kufikisha abiria pasipo kuangalia usalama wake, watembea kwa miguu na hata huyo abiria wake.

Tunaitaka mamlaka kushughulikia kero hii kwa haraka kwani inatishia usalama wa watembea kwa miguuu.

Wiki ya usalama barabarani...
Endesha salama
Fika salama.
Na wengine pia wabaki salama wakiwa njiani.
 

Attachments

  • 20240829_094541.jpg
    20240829_094541.jpg
    2 MB · Views: 9
Katika kuadhimisha wiki ya nenda kwa usalama barabarani 2024.

Tuitumia wiki hii kuwalinda watu wanaotembea kwa miguu katika njia maalumu zilizotengenezwa kwa ajili ya wao kutembea kwa uhuru.

Maana wapo boda boda na baadhi ya bajaji ambao sio wastaarabu huacha njia zao na kutumia njia maalumu za watembea kwa miguu kupitisha vyombo vyao vya usafiri tena kwa spidi isiyokuwa ya kawaida.

Hali hii inapelekea watembea kwa miguu wengi sana kukosa amani wakiwa wanatembea katika njia hizo saa nyingine kugongwa na kusukumiwa njia kuu ambapo magari yanapita kwa kasi sana.

Yaani boda boda anaacha njia kuu aliyotakiwa kupita na kuja kutumia njia za watembea kwa miguu ili awahi kufikisha abiria pasipo kuangalia usalama wake, watembea kwa miguu na hata huyo abiria wake.

Tunaitaka mamlaka kushughulikia kero hii kwa haraka kwani inatishia usalama wa watembea kwa miguuu.

Wiki ya usalama barabarani...
Endesha salama
Fika salama.
Na wengine pia wabaki salama wakiwa njiani.
Sana hii ni kero, na unakuta kama una earphones wakipiga kelele zao za hukusikia wanakutukana mitusi mikubwa tu
 
Ingawa bodaboda ndiyo ajira Kwa vijana kwangu Mimi napinga ajira hii ya hovyo. Serikali inatakiwa kulaumiwa Kwa kuruhusu bajaj na bodaboda kufanya watakalo barabarani
Hatari sana, bodaboda wanapita service road huku wamepakiza nondo,mabati, mageti ,vitanda,miwa n.k hakuna Askari anaye wakamata.
Ubungo darajani bodaboda zinavuka kwenye zebra .
 
Back
Top Bottom