Bodaboda igeni hili litawapa Mileage Kibiashara na Kijamii

Bodaboda igeni hili litawapa Mileage Kibiashara na Kijamii

TODAYS

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
14,747
Reaction score
24,250
20240426_095823.jpg

Kundi la waendesha pikipiki huko jimbo la Arizona Marekani liitwalo 'Bikers Against Child Abuse' ambalo huwaweka salama wahathiliwa wa unyanyasaji hasa watoto, ikiwa ni pamoja na kulinda nyumba zao usiku ikiwa mnyanyasaji hayupo gerezani.

Pia hawa jamaa huhudhuria mahakamani kushuhudia na kusikiliza kesi zilizotokana na madhara yaliyosababishiwa watoto, pamoja na kuwalinda ili wasilazimishwe au kuingia katika mtego wa kisheria.

20240426_095923.jpg


Hawa jamaa walianza kwa kujitolea mtaani kwao ila wakajiongeza ili kuepusha unyanyasaji wa watoto na kuunda shirika la hisani la waendesha pikipiki.

Shirika linafanya kazi ya kulinda watoto katika nchi kumi na nane dhidi ya watu binafsi katika hali za hatari.

Kulingana na mmoja wa memba wa kundi hilo anasema, tangu kuanzishwa kwake mwaka wa 1995, mtaalamu wa tiba na mhudumu wa jamii John Paul Lilly, shirika lao "lipo kwa nia ya kuweka mazingira salama kwa watoto wanaonyanyaswa".

Haya nsugu zangu bodaboda someni hiyo!.
 
Hao ni bikers, sio boda boda,
Halafu kwanin kwenye jamii yetu kila mtu anasukumizia majukumu kwa wengine?
Wew hapo mkuu kwenye kada yako mkiiga hicho kitu huoni itakuwa vizuri? Kwanin wawe boda boda na sio wew ?
 
Sasa wawo wenyewe Bodaboda wanahitaji uangalizi na usalama wa maisha yao

Hawajijari hata chembe,

Je hilo ndilo wataliweza shehe?

Mzungu ni mzungu na Mweusi ni mweusi
 
Bodaboda wetu ndio kwanza wanaongoza kuwatoa bikra
 
Hapa bongo wako bikers rider huwa wanafanyaga charity magerezani na vituo vya watoto yatima
 
Jua kutofautisha mtoa mada.

Mfano.
Anacho. Hana
Tanzania. Marekani
 
Hao ni bikers, sio boda boda,
Halafu kwanin kwenye jamii yetu kila mtu anasukumizia majukumu kwa wengine?
Wew hapo mkuu kwenye kada yako mkiiga hicho kitu huoni itakuwa vizuri? Kwanin wawe boda boda na sio wew ?
a) Hapa bongoland kuna bikers unaowafaham na wana umoja?.

b) Hakuna anayemsukumia mtu jambo labda huko kwenu, hapa tumetoa mfano wa jambo zuri, lililo zuri uigwa kwa jinsi lilivyo.

c) Mimi nina nafasi yangu ambayo jamii inatambua au unataka niandike ujue?.

d) Fulsa huwezi kuzibeba zote mwenyewe lazima uzitawanye uenda kuna mmoja unamfungukia njia kupitia hilo.

e) Tambua; karama yako haitofanana na ya babako.
 
Kiwango Cha unyanyasaji kwa watoto US ni Cha juu mno ni sawa kuwa na asasi za kiraia kama hizo hapa kwetu nadhani mwamko uanzie kwenye jamii na sio ku point bodaboda au kundi lolote kama ndio lifanye hiyo kazi
 
Back
Top Bottom