Bodi ya Maziwa kuharibu maziwa ya ng'ombe kwa kuyamwagia mafuta ya taa

Bodi ya Maziwa kuharibu maziwa ya ng'ombe kwa kuyamwagia mafuta ya taa

Tanzania tuna import maziwa yenye thamani ya zaidi ya bil 500 kila mwaka ikiwamo maziwa ya azam yakitokea India na kuwa reconstituted.

Bodi ya maziwa walau ingejenga platform/bridge ili tuongeze capacity ya kuzalisha maziwa kama hao wauzaji wa ubungo na kuchakata pia.

Kwanini tunakosa innovators kwenye bodi za muhimu kama maziwa, kahawa, korosho. Labda niseme kitu, mara nyingi sana bodi huwa zinaongozwa na wastaafu au watu ambao wanakaribia umri wa kustaafu.
Ningeshauri kwa baadhi ya bodi maziwa na vijana wenye maono ya namna gani tunaweza ku-invent the wheel.

Bodi inge-open avenue ya kuwa na policy na kushirikiana na wizara ya mifugo na wizara ya fedha ili kuziba pengo la ku-import UHT milk kwa kuhakisha uzalishaji unafanyika ndani.

Watanzania wenye uwezo wa kuanzisha miradi kama hii tupo, fedha za uwekezaji mwaka jana zimebaki nyingi tu TIB kwa mujibu wa waziri wa fedha wakati anasoma bajeti. Wangeondoa urasimu kwenye access ya investment credit, nchi hii ingekuwa kwa haraka kiuwekezaji na kuwapa Watanzania unafuu wa bei ya maziwa badala ya kutegemea imports.

View attachment 1489881

Hii ni moja ya falsafa ya uongozi ambapo hata bodi ya maziwa wanawajibika kutafuta uhitaji wa watu/wadau kwenye sekta ya maziwa ili kuikuza sekta ya maziwa.
Changamoto iliyopo kwenye hizo bodi nyingi zilitengenezwa katika mfumo wa kutawala na siyo kufanya hizo innovation and capacity building.
 
Changamoto iliyopo kwenye hizo bodi nyingi zilitengenezwa katika mfumo wa kutawala na siyo kufanya hizo innovation and capacity building.
Uko sawa kabisa mkuu.
Bodi hizi zingehama kwenye kuwa regulatory authorities na kuwa majukumu ya kujenga platforms za kuruhusu innovation, bila shaka tungekuwa kwa haraka zaidi ukilinganisha na kasi ambayo inatufanya tuzidi kuwa nyuma.
Nchi kama Netherlands, Israel, New Zealand zikiunganishwa kwa pamoja zina eneo dogo sana. Isipokuwa kila nchi inafanya vema sana kwenye sekta ya maziwa (milk products).

Siku bodi ikipata watu wenye innovation DNA tutaona matokeo ya tofauti.
 
Kuna mwenyekiti wa bodi ya kituo Cha Afya yeye hushinda kituoni kutwa akiangalia watumishi wanavyofanya kazi Hadi usiku huwa ananyemelea kuona Nani yupo wapi na anafanya nn? Ni shida balaa
 
Haya mabodi yanasaidia nn!!? Kwenye maziwa yetu pendwa au TFDA na maafisa afya na maafisa Rishe Wana kazi gani
 
Hii taarifa haieleweki.. Why hiyo bodi imwagie mafuta ya taaa??? Je hao kina mama wanapewa hayo maziwa na bodi au waoo ndo wanaiuzia bodi maziwa???? Kama wanaiuzia bodi sasa bodi si ndo inapata hasaraa na kama Bodi inawauzia kina mama maziwa still naona kuna hasaraa maana watakataa kuyanunua may b mtu anieleweshe hapa
 
ITV leo asubuhi imemuonyesha Waziri wa Mifugo, Mhe. Luhaga Mpina akitoa maelekezo ya kuzuia vitendo vya KISHETANI vinavyofanywa na Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania kuchafua maziwa ya ng'ombe yanayouzwa na Wajasiriamali wanawake katika eneo la Ubungo kwa kuyamwagia mafuta ya taa, au rangi ili yasifae kutumika.

Maziwa hayo huwa yanauzwa yakiwa katika ndoo safi za plastic zenye mifuniko.

Najiuliza: Matendo ya Watendaji wa Bodi ya Maziwa ya kutumia pesa za Umma kwa kununua mafuta ya taa na kwenda kuyamwaga juu ya maziwa na hivyo kuwahujumu Wajasiriamali, tena akina mama, hakina ujinai ndani yake?
1st degree murder.
 
Labda ni masharti ya magharibi watz wasipate afya ya akili na mwili.
 
Hakuna ushabiki maana hii ni taarifa ya ITV ya saa 12.00 asubuhi, Ijumaa tarehe 26.6.2020.
Waziri wa Mifugo amefika Ubungo, sehemu yanapouzwa hayo maziwa saa 11.00 alfajiri, akakutana na akina mama wauza maziwa, kisha Msajili wa Bodi ya Maziwa, akiwa na Mtumishi mwenzake mmoja wakasema ni kweli wanamwagia mafuta ya taa kwenye maziwa na kuyatia rangi ili yasitumiwe na binadamu.
Kosa lililotajwa ni kwamba kuna kifungu cha sheria kinasema maziwa yauziwe kwenye 'container' ya aluminium.
Hawa wanauzia kwenye ndoo za plastic.
Watumiaji wote wa maziwa nchini tunahifadhi maziwa kwenye ndoo za plastic.
Kwa Bodi ya Maziwa, adhabu yetu ni kumwagiwa mafuta ya taa.
Tena yaliyonunuliwa kwa kodi zetu.
Kwa bahati nzuri Waziri Mpina amepiga marufuku tabia hiyo ya kuwahujumu hao akina mama Wajasiriamali.
Swali langu, hao Watumishi wa Bodi ya Maziwa, hawastahili kupelekwa Kisutu?
Hivi maziwa ya asas tunayokuta dukani huwa kwenye package za aluminium?
 
Hivi hizi bodi sijui za nyama, mara sijui maziwa ni nani alizobuni, mbona ni kama vijiwe vya kupeana ulaji tu?
 
Back
Top Bottom