Bodi ya mikopo ya wanafunzi elimu ya juu wamefuta allocations za wanafunzi ambao walipangiwa mikopo 2024/25

Bodi ya mikopo ya wanafunzi elimu ya juu wamefuta allocations za wanafunzi ambao walipangiwa mikopo 2024/25

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Mnamo tarehe 28 Septemba bodi ya mikopo HESLB ilianza kutangaza waliopangiwa mkopo awamu ya kwanza yenye wanafunzi 21,509 wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2024/2025.

Kadhalika Bodi ya Mikopo ya Wanafurnzi wa Elimu ya Juu (HESLB) siku ya Jumatano (Oktoba 09, 2024) ilitangaza awamu ya pili ya orodha ya wanafunzi wenye sifa waliopangiwa mikopo na ruzuku kwa ajili ya mwaka wa masomo 2024/2025.
Img_2024_10_13_18_47_48.jpeg

Kilichonishangaza ni baada ya kutembelea Chuo kimoja kilichopo jijini Dar es salaam na kukutana na mtu ambaye ni mtumishi hapo na kunieleza kuwa bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB) wamefuta allocations walizokuwa wamezitoa kwa wanafunzi ambao walikidhi vigezo huku sababu ya kufuta allocations hizo ikiwa haijulikani na kuwaacha njiapanda baadhi ya wanafunzi wanaotegemea mikopo hiyo huku vyuo vikiwa vimeanza kufunguliwa.

Swala hilo likanifanya nitafute mwanafunzi ambaye alipangiwa mkopo ili kuthibitisha hilo na baada ya kuangalia account aliyotumia kuomba mkopo hivi ndivyo inavyoonekana.

Screenshot_20241013-184910.png

Awali kabla ya hilo kutokea allocation yake ilikuwa ikionekana hivi

IMG-20241013-WA0001~2.jpg

Mpaka sasa bodi ya mikopo hawajasema chochote juu ya jambo hili wakati ambao baadhi ya vyuo vikiwa vimefungua na usajili wa wanafunzi ukiendelea HESLB ni vema mkatoa ufafanuzi haraka sana.
 
Mnamo tarehe 28 Septemba bodi ya mikopo HESLB ilianza kutangaza waliopangiwa mkopo awamu ya kwanza yenye wanafunzi 21,509 wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2024/2025.

Kadhalika Bodi ya Mikopo ya Wanafurnzi wa Elimu ya Juu (HESLB) siku ya Jumatano (Oktoba 09, 2024) ilitangaza awamu ya pili ya orodha ya wanafunzi wenye sifa waliopangiwa mikopo na ruzuku kwa ajili ya mwaka wa masomo 2024/2025.

Kilichonishangaza ni baada ya kutembelea Chuo kimoja kilichopo jijini Dar es salaam na kukutana na mtu ambaye ni mtumishi hapo na kunieleza kuwa bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB) wamefuta allocations walizokuwa wamezitoa kwa wanafunzi ambao walikidhi vigezo huku sababu ya kufuta allocations hizo ikiwa haijulikani na kuwaacha njiapanda baadhi ya wanafunzi wanaotegemea mikopo hiyo huku vyuo vikiwa vimeanza kufunguliwa.

Swala hilo likanifanya nitafute mwanafunzi ambaye alipangiwa mkopo ili kuthibitisha hilo na baada ya kuangalia account aliyotumia kuomba mkopo hivi ndivyo inavyoonekana.


Awali kabla ya hilo kutokea allocation yake ilikuwa ikionekana hivi


Mpaka sasa bodi ya mikopo hawajasema chochote juu ya jambo hili wakati ambao baadhi ya vyuo vikiwa vimefungua na usajili wa wanafunzi ukiendelea HESLB ni vema mkatoa ufafanuzi haraka sana.
Hili nalo mkalitizame by kizimkazi
 
Mwanangu mwaka juzi alipata mkopo Bach one. Nikascreen shoot kabisa maandalizi yakafanyika akafika chuo.
Tobaaaa kuja kwenye harakati za usajiri system ya chuo inamkataa aimtambui kama mnufaika wa mkopo.
Kuja kuchungulia sipa yake Sasa mkopo Amna umefutwa tumekalibishwa dilisha la rufani nikasema ujinga huo sifanyi akuna rufani hapa.
Nb.bodi ndio tabia yao kiwanusishwa mikopo watoto wa watu then wanawakwapua juu kwa juu.
 
Hivi kwa nini wambemblezwe kukupa mkopo ambao mwisho utalipa? Nakumbuka walivyokuwa wanatusumbua kwa kutecheleweshea mpaka tunaandama mpaka tunapigwa na polisi! Lakini sasa hivi wanavyodai sasa. Mbaya wanatumbambikia madeni mimi walinikata mpaka hela books and stationary ambayo sikuwahi kupewa. Nalipa lakini nilitesheka sana mpak niandamane ndiyo waweke boom
 
Back
Top Bottom