Bodi ya Mikopo yasema imetumia Tsh. Milioni 623.2 kuwafadhili wanafunzi wa Masters

Bodi ya Mikopo yasema imetumia Tsh. Milioni 623.2 kuwafadhili wanafunzi wa Masters

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Snapinst.app_474915343_18214766224291835_5816539007441518690_n_1080.jpg
ORODHA YA WANUFAIKA WA 'SAMIA SCHOLARSHIP' NGAZI YA SHAHADA YA UMAHIRI YATANGAZWA

Tsh. Milioni 623.2 zatumika kuwafadhili

■Jumla ya wanafunzi 80 wa Shahada za Uzamili katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) ambao wamedahiliwa katika programu za sayansi na ubunifu, wamepangiwa ruzuku zenye thamani ya TZS 623.2 milioni kupitia 'Samia Scholarship'.

■Wanafunzi walioomba fursa hizo wanashauriwa kuangalia taarifa zao kupitia akaunti walizoombea (SIPA). Aidha, wanafunzi husika watatakiwa kujisajili kwenye mfumo wa malipo wa kidigitali (DiDiS) kupitia kwa Maafisa wa HESLB watakaoratibu zoezi hilo chuoni NM-AIST kuanzia Januari 22, 2025.

■Hii ni mara ya kwanza kwa Serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu kutoa 'Samia Scholarship' kwa wanafunzi wa fani za Sayansi waliodahiliwa katika ngazi ya Shahada za Uzamili.

■Kwa taarifa hii, wanafunzi wote walioomba fursa za 'Samia Scholarship' katika ngazi ya Shahada za Umahiri wanajulishwa kuwa zoezi la upangaji ruzuku hizo kwa mwaka 2024/2025 limefikia mwisho.

Imetolewa na: Mkurugenzi Mtendaji

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Dar es Salaam, Januari 22, 2025

Pia soma ~ Wanufaika wa Ufadhili wa Masomo ya Masters kupitia Samia Suluhu Scholarship tumetelekezwa bila muongozo
 
Back
Top Bottom