Frank Wanjiru
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 22,719
- 40,739
Tulipokuwa tunawaambia njooni mjifunze Yanga mkawa mnajifanya nyinyi wakubwa,haya sasa kila mtu kawa kambale huko.Am so disappointed, najiandaa kisaikolojia kuuacha kwanza mpira wa bongo. Klabu yangu pendwa Iko shimoni.
Hatari sana.Mjumbe wa Bodi ya Simba SC CPA ISSA MASOUD akiongea na Waandishi wa habari Jana, amekiri kwamba shilingi bil. 20 alizoahidi mwekezaji Mohamed Dewij "Mo" hazijawahi kuwekwa popote Bali aligeuza fedha anazotoa Kwa matumizi ya kawaida (kununua mchicha, boxer na kandambili) ndo zihesabike kama uwekezaji wa 20b.
Alichotushangaza zaidi ni pale aliposema Jambo hili wanalijua Kwa miaka 3 Sasa lakini wamekuwa wakitoa Taarifa ya Bodi kwenye mikutano mikuu kuonyesha Mambo ni shwari.
Akaenda mbali zaidi akasema hata usajili wa Wachezaji unafanyika Kwa kificho Bodi haijui na kwamba kuanzia Sasa hawataruhusu hilo maana Hali hiyo imesababisha kusajiliwa Kwa Wachezaji wasio na kiwango Bora cha kuchezea Simba SC.
Hoja yangu ni kwamba, Kwa nini Bodi hii hasa wajumbe waliochaguliwa na wanachama wamekubali Kwa miaka yote 3 kuwauza wanachama waliowachagua na kuungana na wajumbe wa upande wa Mwekezaji kutengeneza Taarifa feki na kuwasomea wanachama kwenye mikutano mikuu?
Kwa hali hii nini faida ya wanachama kuwa na wawakilishi kwenye Bodi kama nao wanaungana na mwekezaji "kudanganya" wanachama? Hata kama lengo ilikuwa kutunza Siri za Bodi, walitegemea kutunza Siri hii Kwa Muda gani?
Kwa hili wajumbe wa Bodi mliochaguliwa na wanachama mmewauza waajiri wenu, Wajibikeni.
Mjumbe wa Bodi ya Simba SC CPA ISSA MASOUD akiongea na Waandishi wa habari Jana, amekiri kwamba shilingi bil. 20 alizoahidi mwekezaji Mohamed Dewij "Mo" hazijawahi kuwekwa popote Bali aligeuza fedha anazotoa Kwa matumizi ya kawaida (kununua mchicha, boxer na kandambili) ndo zihesabike kama uwekezaji wa 20b.
Alichotushangaza zaidi ni pale aliposema Jambo hili wanalijua Kwa miaka 3 Sasa lakini wamekuwa wakitoa Taarifa ya Bodi kwenye mikutano mikuu kuonyesha Mambo ni shwari.
Akaenda mbali zaidi akasema hata usajili wa Wachezaji unafanyika Kwa kificho Bodi haijui na kwamba kuanzia Sasa hawataruhusu hilo maana Hali hiyo imesababisha kusajiliwa Kwa Wachezaji wasio na kiwango Bora cha kuchezea Simba SC.
Hoja yangu ni kwamba, Kwa nini Bodi hii hasa wajumbe waliochaguliwa na wanachama wamekubali Kwa miaka yote 3 kuwauza wanachama waliowachagua na kuungana na wajumbe wa upande wa Mwekezaji kutengeneza Taarifa feki na kuwasomea wanachama kwenye mikutano mikuu?
Kwa hali hii nini faida ya wanachama kuwa na wawakilishi kwenye Bodi kama nao wanaungana na mwekezaji "kudanganya" wanachama? Hata kama lengo ilikuwa kutunza Siri za Bodi, walitegemea kutunza Siri hii Kwa Muda gani?
Kwa hili wajumbe wa Bodi mliochaguliwa na wanachama mmewauza waajiri wenu, Wajibikeni.
Kwani Semaji la Shirikisho Ahmed Ally anasemaje?Huu mgogoro ni hatari sana kwa mustakabari wa timu.
Namuunga mkono.Haya tuchukulie kuwa MO ana matatizo ya ujanja au hata utapeli halafu kuna mjumbe wa bodi aliyeaminiwa na wanachama ambaye ni CPA (T) halafu yupo anaona madudu yote hayo ya Mo akaamua kukaa kimya kwa miaka 3+. Ghafla tu leo anaibuka kwenye vyombo vya habari bila aibu anasema kwa takribani miaka mitatu kuna matatizo Simba!
Swedi Mkwabi apewe maua yake kwa sababu yeye aliona madudu mapema na akajiuzulu lakini hao wapuuzi wakina CPA Masoud hawana cha kujitetea kwani wao ni sehemu ya hayo madudu yote wanayomuangushia Mo sasa hivi.
Kuna mambo lazima yawekwe sawa kabla ya kuendelea.Muda wa kufanya usajiri sisi tupo kwenye marumbano baadae tuta anza kulaumu Yanga ana nunua mechi