Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Dar es Salaam. Bodi ya Wadhamini wa Klabu ya Soka ya Simba imefungua kesi kupinga mkutano mkuu wa klabu hiyo.
Mkutano mkuu wa klabu hiyo unatarajiwa kufanyika Jumapili ijayo.
Hata hivyo Bodi ya Wadhamini wa klabu hiyo wamefungua kesi hivi punde katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ikiiomba mahakama hiyo izuie kufanyika kwa mkutano huo.
Wakili wa bodi hiyo ya wadhamini, Juma Nassoro amelieleza Mwananchi kuwa kesi hiyo inatarajiwa kusikilizwa saa aaba mchana huu na Hakimu Thomas Simba.
Kabla ya kufikia uamuzi huo leo wa kufungua kesi, bidii hiyo ya wadhamini uliuonya uongozi wa klabu hiyo kuachana na mipango ya maandalizi ya mkutano huo na kwamba kama wakiendelea basi itakwenda mahakamani kuuzuia.
Uamuzi huo wa bodi ya wadhamini ni kinyume na kanuni za Fifa inayokataza masuala ya mpira kwenda mahakamani hivyo kuna uwezekano wa Simba ikapoteza nafasi ya kushiriki Ligi Kuu pamoja na mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
mwananchi