Bomba la mafuta la Afrika Mashariki: Diplomasia ya uchumi ya urithi wa Hayati Magufuli na mapato ya Tsh 76.32bn kwa mwaka

Bomba la mafuta la Afrika Mashariki: Diplomasia ya uchumi ya urithi wa Hayati Magufuli na mapato ya Tsh 76.32bn kwa mwaka

Kinuju

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2021
Posts
2,386
Reaction score
5,325
BOMBA LA MAFUTA LA AFRIKA MASHARIKI: DIPLOMASIA YA UCHUMI YA URITHI WA JPM NA MAPATO YA TSH 76.32bn KWA MWAKA

Mnamo Septemba 27, 2020 Uganda na Tanzania ziliingia makubaliano kupitisha Bomba la Mafuta ya Afrika Mashariki kutokea Hoima (Uganda) hadi Bandari ya Tanga (Tanzania). Hii ni moja ya mafanikio makubwa ya Diplomasia ya Uchumi ya Hayati JPM. Maana iliua kabisa ndoto za Kenya kupitishia bomba hilo kwenda Bandari yake ya Lamu.

Mradi huu ni alama ya urithi itakayo ihakikishia Tanzania kiasi cha $12.7 kwa kila pipa litakalo safirishwa katika bomba hilo kutokea Uganda.

Hivyo kibiashara na kiuchumi, huu ulikuwa ni ushindi wa kimkakati kwa Tanzania wenye uwekezaji wa takribani $3.6bn na zaidi ya asilimia 70 ya bomba litapitia Tanzania hivyo itakuwa imevutia kiasi kikubwa cha uwekezaji kutoka nje kati hizi $3.6bn.

Bomba hili linatarajiwa kupitisha pipa la kwanza mnamo 2025. Na kwa siku yatasafirishwa mapipa 216,000 ya mafuta ghafi. Hii itaihakikishia Tanzania takribani $2.743 mil (Tsh 6.36bn) kwa siku. Hii ni sawa na $32.92mil (Tsh 76.32bn) kwa mwaka kama tozo ya kusafirishia mafuta hayo. Haya ni mapato mapya.

Kuna kama mapipa 6.5bn ambayo yamekwisha thibitishwa huko Uganda katika visima Kingfisher na Tilenga. Hivyo Tanzania itakuwa na uhakika wa kutengeneza mapato mengi zaidi kwa takribani miaka 30 ijayo kutokana na Mkataba uliohitimishwa siku ya Jumapili tarehe 11 Aprili 2021 wakati Rais Samia Suluhu Hassan aliposhuhudia utiwaji wa mikataba hiyo ya kimkakati. Kazi inaendelea. Huku Rais Yoweri K. Museveni akisema siku huyo ilikuwa ni siku ya Ushindi wa aina Tatu (Kitiva, Kisiasa na Kiuchumi) kwani Tanzania imekuwa sehemu ya kupigania ukombozi wa Uganda kutoka wa mikono ya Idd Amini pamoja na ukombozi wa bara la Afrika. Hivyo hii pia ni sababu iliyorahisisha uamuzi wa kuifanya Tanzania kuwa njia ya kusafirishia mafuta hayo ili Tanzania nayo ipata kitu kutokana na majotoleo yake katika Ukombozi wa Afrika.

Ndiyo maana ninaamini kuwa hapa JPM aliacha legacy kubwa..na ni ushindi kwa Tanzania katika Diplomasia ya Uchumi katika Afrika Mashariki dhidi ya Taifa lenye Uchumi mkuwa kwa sasa katika Ukanda huu.

Ninaamini pia faida zitakuwa ni nyingi zaidi ya tozo hii ya $12.7 kwa kila pipa litakalosafirishwa kwa siku. BOMBA hili kitakuwa linapashwa joto ili mafuta hayo ghafi nyenye mnato mkubwa (viscocity) yaweze kupita. Ninaamini kwa kuwa na Umeme wa uhakika pia tutapata mapato ya ziada yanayoweza kusaidia kurejesha fedha nyingi zilizowekezwa katika vyanzo vya Umeme hada bwawa la JNHPP-2115MW. Faida nyingine ni Ajira za muda mfupi na muda mrefu zinazofikia elfu kumi (10).

Lakini Prof Assad hana impact hata kwenye ukoo wake.
 
Prof Assad sio size yako.

Cheo alichowahi kuwa nacho mpaka Katiba ya JMT inakitambua.

Wewe hapo ulipo hata Sheria ya kitongoji haitaji cheo wala kazi yako.

Acheni watu waongee wapunguze hasira, unaleta propaganda huku ukijua JPM kama mwanadamu kuna sehemu aliteleza ama hakushauriwa vema.

Tunamtakia pumziko la amani, sote tutakufa tupendane madaraka huisha.
 
Magufuli au Kikwete, As sad na hayati ni vitu 2tofauti Mkuu, hayati asingeweza kuwa Kama Assad, but Assad angeweza kuwa kama hayati, mnaweka usimba na uyanga katika maswala ya nchi na ndio maana nchi haiendi.
 
Usichanganye siasa na uchumi hivyi vitu haviendi pamoja.

Prof Asad ni mtaalamu wa uchumi na mambo ya fedha ila sio mtaalam wa siasa

Unaweza kuwa unajua siasa lakini hujui siasa ya uchumi

kuongelea siasa ni rahisi lakini unaweza kupanga kitu juu ya meza lakini usiwe na vision ya mbele kitakachotokea

Mbona hujaongelea bomba la mafuta la Tanzania-Zambia lipo zaidi ya miaka 30 tija yake kwa taifa ni ipi

Uzuri wa mkuu wetu aliyetangulia mbele za haki mungu alimjalia sana kuwa na uwezo wa kutoa maamuzi magumu lakini implication ya baadae ilikuwa inakuwa kisiasa zaidi sio the real situation.

Nitoe mfano ndege zilizonunuliwa kwa madai ni hela za ndani faida yake ni ipi hadi sasa

Ujenzi wa uwanja wa Chato faida yake ni ipi kwa taifa ungejengwa Geita ingekuwa bora zaidi au ungepanuliwa wa Bukoba

Ujenzi wa CRDB bank Chato kwa bank yenyewe faida yake ni ipi bank zinajengwa mahali penye mzunguko wa hela na ndio maana benki zinajengwa zaidi mijini huwezi jenga benki katikati ya mbuga ya serengeti.

Kuhamisha wanyama ambao wanaishi mazingira kulingana na ecosystem yao mungu aliyowapa achilia mbali wanyama wa zoo maana hawa wanalishwa hawajitafutii wenyewe.Nina wasiwasi wale wanyama watakuwa wamehamia nchi ya jirani.

Swala la bomba la mafuta ni jambo la wazi na kawaida kabisa maana hata Nyerere na Kaunda waliwazaga kitu kama hicho hicho na ndio maana wakajenga reli ya Tanzania-Zambia.

Ndege duniani hazinunuliwagi kwa cash kama inavyodaiwa ukiona mtu kafanya hivyo kuna sehemu amebana na kuna wadau wengine wanaumia kwa uamuzi huo.Mfano mzuri watu kutokupanda madaraja makazini mishahara kutokuongezwa na wastaafu kutokulipwa mafao yao kwa wakati muafaka.

Na nukuu baba wa Taifa Nyerere "huwezi kusema unaleta maendeleo maendeleo lazima kwanza yawe people's centred sio maendeleo ya vitu'' mwisho wa kunukuu

Unaweza ukawa na mandege 100 lakini watu wako hao hao wakawa hawana uwezo wa kupanda hizo ndege
 
Usichanganye siasa na uchumi hivyi vitu haviendi pamoja.

Prof Asad ni mtaalamu wa uchumi na mambo ya fedha ila sio mtaalam wa siasa

Unaweza kuwa unajua siasa lakini hujui siasa ya uchumi

kuongelea siasa ni rahisi lakini unaweza kupanga kitu juu ya meza lakini usiwe na vision ya mbele kitakachotokea

Mbona hujaongelea bomba la mafuta la Tanzania-Zambia lipo zaidi ya miaka 30 tija yake kwa taifa ni ipi

Uzuri wa mkuu wetu aliyetangulia mbele za haki mungu alimjalia sana kuwa na uwezo wa kutoa maamuzi magumu lakini implication ya baadae ilikuwa inakuwa kisiasa zaidi sio the real situation.

Nitoe mfano ndege zilizonunuliwa kwa madai ni hela za ndani faida yake ni ipi hadi sasa

Ujenzi wa uwanja wa Chato faida yake ni ipi kwa taifa ungejengwa Geita ingekuwa bora zaidi au ungepanuliwa wa Bukoba

Ujenzi wa CRDB bank Chato kwa bank yenyewe faida yake ni ipi bank zinajengwa mahali penye mzunguko wa hela na ndio maana benki zinajengwa zaidi mijini huwezi jenga benki katikati ya mbuga ya serengeti.

Kuhamisha wanyama ambao wanaishi mazingira kulingana na ecosystem yao mungu aliyowapa achilia mbali wanyama wa zoo maana hawa wanalishwa hawajitafutii wenyewe.Nina wasiwasi wale wanyama watakuwa wamehamia nchi ya jirani.

Swala la bomba la mafuta ni jambo la wazi na kawaida kabisa maana hata Nyerere na Kaunda waliwazaga kitu kama hicho hicho na ndio maana wakajenga reli ya Tanzania-Zambia.

Ndege duniani hazinunuliwagi kwa cash kama inavyodaiwa ukiona mtu kafanya hivyo kuna sehemu amebana na kuna wadau wengine wanaumia kwa uamuzi huo.Mfano mzuri watu kutokupanda madaraja makazini mishahara kutokuongezwa na wastaafu kutokulipwa mafao yao kwa wakati muafaka.

Na nukuu baba wa Taifa Nyerere "huwezi kusema unaleta maendeleo maendeleo lazima kwanza yawe people's centred sio maendeleo ya vitu'' mwisho wa kunukuu

Unaweza ukawa na mandege 100 lakini watu wako hao hao wakawa hawana uwezo wa kupanda hizo ndege
Walikua wanatoa hadi magawio fake ili ionekane zinaleta faida, sasa hivi wamegeuka wanasema biashara ya ndege faida yake inachukua muda mrefu, kwahiyo kwa miaka ya karibuni lazima hasara ipatikane kwanza, kwahiyo sio tatzo! Kwaufupi mim nachangayikiwa
 
Mwenye hoja anaweza andika paragraph moja na akaeleweka. Maneno meengi ugoro tuuu.
Hata shetani ana historia ya mamilioni ya miaka.
MAGUFULI NI SHETANI WA TANZANIA
Shetani tigo yako
 
Mkuu hilo bomba sio la kwanza lipo TAZAMA tumezaliwa lipo tuu toka Daslm mpaka Zambia ungewauliza hilo linachangia kiasi gani na linapitisha mapipa mangapi kwa saa ningekuelewa kidogo ili twende sawa...
 
Sitaki kumhukumu JPM analaana za watu wengi sina ndii maana Mungu hakutaka kumwacha amalize muda wake.Alotaka abudiwe kama Mungu ,asikosolewe,nk Prof Asad Mungu atampa maisha marefu yenye afya .Ndio tofauti ya mtu mwenye Roho safi na mbaya
 
Sasa Profesa Assad anahusikaje na ulichoandika hapo au ndio kuwashwa washwa kuko hivyo?
Hata mimi namshangaa sana.Huwezi mpambanisha Asad na Magufuli kila mmoja ana wigo wa taaaluma yake.

Asad anaongelea taaluma yake haongelei siasa kwanza siasa haijui.

Mkuu wetu aliyetangulia japo na yeye kiukweli hatuwezi sema alikuwa ni mwanasiasa ila alikuwa amebobea kwenye utendaji na uwezo wa kutoa maamuzi magumu kuliko maraisi wote waliopita kwa hapa nampa ngongole shida inakuja hayo maamuzi yana implication yake in future itakuwaje.

Kumlinganisha aliyetangulia na Asad ni sawa kushindanisha mafuta na maji kuwa vyote ni vimiminika ni kipi kama kikijazwa kwenye pipa kitakuwa kizito zaidi kumbe unashindwa kujua vyote ndio ni vimiminika lakini vina density tofauti hata vikijaa kwenye pipa uzito wake utakuwa tofauti.

Kuna usemi unasema beautlul one are not yet born yaani wema au vizuri bado havijazaliwa.Abraham Lincolin alitokea kuwa raisi bora sana Marekani lakini waliomfuatia wapo walikuja kuwa wazuri pia.Kila mmoja duniani anakumbukwa kwa mabaya na mazuri yake that is nature.

Mtanguliaji ana mazuri tena mengi tu lazima tumpe credit zake ila naye kama binadamu mwenye nyama na damu ana mapungufu yake.Aliyofanya mazuri tuyaendeleze aliyofanya mabaya tuyasahihishe hata kama ni kimya kimya ila kwa mtandao na uwazi wa sasa hivyi ni vigumu sana kuyaficha pembe la ng'ombe halifichiki.

Baba wa Taifa angefariki leo na utandawazi huu lazima tu ungesikia mengi
 
Ndg umenena ukweli kila binadam ana mazuri na mabaya yake. RIP JPM.
Hata mimi namshangaa sana.Huwezi mpambanisha Asad na Magufuli kila mmoja ana wigo wa taaaluma yake.

Asad anaongelea taaluma yake haongelei siasa kwanza siasa haijui.

Mkuu wetu aliyetangulia japo na yeye kiukweli hatuwezi sema alikuwa ni mwanasiasa ila alikuwa amebobea kwenye utendaji na uwezo wa kutoa maamuzi magumu kuliko maraisi wote waliopita kwa hapa nampa ngongole shida inakuja hayo maamuzi yana implication yake in future itakuwaje.

Kumlinganisha aliyetangulia na Asad ni sawa kushindanisha mafuta na maji kuwa vyote ni vimiminika ni kipi kama kikijazwa kwenye pipa kitakuwa kizito zaidi kumbe unashindwa kujua vyote ndio ni vimiminika lakini vina density tofauti hata vikijaa kwenye pipa uzito wake utakuwa tofauti.

Kuna usemi unasema beautlul one are not yet born yaani wema au vizuri bado havijazaliwa.Abraham Lincolin alitokea kuwa raisi bora sana Marekani lakini waliomfuatia wapo walikuja kuwa wazuri pia.Kila mmoja duniani anakumbukwa kwa mabaya na mazuri yake that is nature.

Mtanguliaji ana mazuri tena mengi tu lazima tumpe credit zake ila naye kama binadamu mwenye nyama na damu ana mapungufu yake.Aliyofanya mazuri tuyaendeleze aliyofanya mabaya tuyasahihishe hata kama ni kimya kimya ila kwa mtandao na uwazi wa sasa hivyi ni vigumu sana kuyaficha pembe la ng'ombe halifichiki.

Baba wa Taifa angefariki leo na utandawazi huu lazima tu ungesikia mengi
 
MSISHANGAE SANA WAKUU HAWA NDIO WASEMAO TANGU VYAMA VYA WAPINZANI VIANZE WAMEIFANYIA NCHI HII NA WAKAJIKUTA WAMEWAZA SAWA SAWA POLENI SANA DARASA LA SABA MNATUSUMBUA SANA.
 
Back
Top Bottom