Mwishokambi
JF-Expert Member
- Nov 23, 2020
- 390
- 1,425
Juzi bondia Abdallah Pazi maarufu Dullah Mbabe alipata fursa ya kuandaliwa pambano na bondia chipukizi wa Masasi aitwae Ramadhan Migwede, Dullah alifanikiwa kushinda pambano hilo kwa knockout ya raundi ya 7 kati ya raundi 8 za pambano hilo.
Pamoja na kushinda, bondia Migwede alimmudu sana Dullah, alipelekeshana nae mwanzo mwisho hadi raundi ya saba ndipo Migwede aliposalimu amri kwa kubamizwa ngumi ya kichwa moja akaanguka chini na ndipo shughuli ilipokwisha.Kiukweli bondia Migwede ni chipukizi na Dullah yuko mikoa kusini ku promote ngumi baada ya kutoka Tunduru lakini pambano hili angedhalilika kama angefanya masihara maana Migwede alijitahidi sana kumkabili Dullah, changamoto kwake ilikuwa ni kukosa uzoefu.
Namshauri Dullah, pamoja na kuwa ndondo zinamuingizia kipato lkn kuna siku atamvagaa mbeba viazi ulingoni atamchukulia poa, ataumia, watu wanajua ngumi wanakosa promotion tu, halafu Dullah aongeze mazoezi, amekosa kabisa mbinu na fitness za kupambana, ukiliangalia pambano hilo kwenye YouTube huwezi amini kama anayepigana ni Dullah Mbabe.
Pamoja na kushinda, bondia Migwede alimmudu sana Dullah, alipelekeshana nae mwanzo mwisho hadi raundi ya saba ndipo Migwede aliposalimu amri kwa kubamizwa ngumi ya kichwa moja akaanguka chini na ndipo shughuli ilipokwisha.Kiukweli bondia Migwede ni chipukizi na Dullah yuko mikoa kusini ku promote ngumi baada ya kutoka Tunduru lakini pambano hili angedhalilika kama angefanya masihara maana Migwede alijitahidi sana kumkabili Dullah, changamoto kwake ilikuwa ni kukosa uzoefu.
Namshauri Dullah, pamoja na kuwa ndondo zinamuingizia kipato lkn kuna siku atamvagaa mbeba viazi ulingoni atamchukulia poa, ataumia, watu wanajua ngumi wanakosa promotion tu, halafu Dullah aongeze mazoezi, amekosa kabisa mbinu na fitness za kupambana, ukiliangalia pambano hilo kwenye YouTube huwezi amini kama anayepigana ni Dullah Mbabe.