Bongo hapo zamani: Nyerere alipoongoza kikao kilichoiua TAA na kuizaa TANU

Bongo hapo zamani: Nyerere alipoongoza kikao kilichoiua TAA na kuizaa TANU

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Bongo Hapo Zamani:
NYERERE ALIPOONGOZA KIKAO KILICHOIUA TAA NA KUZAA TANU

Kwenye kichumba kidogo kisichokuwa na hewa ya kutosha, Julius Nyerere alikaa kwenye kiti chenye meza. John Rupia alikaa kwenye kiti kingine.

Akina Sykes, mtu na nduguye, wakiwa na Dossa Aziz walihangaika na vilivyomo kwenye mikoba walioingia nayo kwenye chumba hicho.

Julius Nyerere akafungua kikao kwa kusema ametafakari sana kuhusu T.A.A. , lakini, imekuwa vigumu kukibadilisha kuwa Chama cha siasa.

Kwa kauli hiyo, ilimaanisha kuwa T. A. A ilishachimbiwa kaburi. Mwisho wa T. A. A ukawa hapo na T. A. N. U ikawa njiani kuzaliwa.

Siku ya tukio hilo ilikuwa Oktoba 10, 1953. Kikao kilikuwa ni cha T. A. A kwenye nyumba moja pale New Street ( Mtaa Mpya) ambao sasa unaitwa Mtaa Lumumba.

Haya yamo kwenye kitabu ninachokisoma sasa cha ‘ The Making of Tanganyika ‘ kilichoandikwa na mwanamama Judith Listowel.
Maggid,
Zanzibar.

Mwenyekiti Maggid,


Hayo hapo juu yanatokana na mahojiano kati ya Judith Listowel na Mwalimu Nyerere.

Nyumba hii ya New Street ambayo ilikuwa ofisi ya African Association ilijengwa kati ya mwaka wa 1929 hadi 1933 kwa kujitolea wanachama wenyewe kuja kufanya kazi za ujenzi kila Jumapili.

Abdu Sykes anaeleza kuwa yeye akiwa mtoto mdogo alikuwa akifuatana na baba yake kuja pale kila Jumapili.

Haikumpitikia kuwa iko siku yeye na mdogo wake watakuja kuwa viongozi wa chama hiki na watashiriki katika kuasisi TANU kudai uhuru wa Tanganyika.

Katika kitabu cha Abdul Sykes ipo picha ya ufunguzi wa ofisi hii na baadhi ya majina ya waliohudhuria sherehe hiyo iliyoongozwa na Gavanà Donald Cameron.

1572798246046.png

Katika hii picha waliokaa wa pili kushoto ni Ramadhani Mashado Plantan
Barabara ya United Nations wakati wa ukoloni ikiitwa Donald Cameron Road kwa heshima ya Gavana huyu.

Yeye ni kati ya watoto wa Chief Mohosh Mkuu wa Jeshi la Wazulu lililoingia Tanganyika na Herman von Wissman kuja kupigana na Abushiri bin Salim Al Harith na Mtwa Mkwawa.

Mohosh akajajulikana kwa jina la Affande Plantan Tanganyika wakati huu akiwa Mkuu wa Germany Constabulary.

Kaka yake, Thomas Plantan ndiye alikuwa Rais wa TAA aliyepinduliwa na Abdul Sykes na Dr. Vedasto Kyaruzi kuingia madarakani ili kugeuza TAA kiwe chama cha siasa kudai uhuru.

1572837852408.png

Thomas Plantan

Aliyekuwa akitia shinikizo la kumtoa Thomas Plantan alikuwa mdogo wake Abdillah Schneider Plantan.

Msimamo wa Schneider ilikuwa wakati umefika chama kiongozwe na vijana.

Listowel kawapa jina hawa vijana kawaita "Makerere Intellectuals."
Hawa akina Plantan na Sykes ni ndugu.

Dr. Kyaruzi kwenye mswada wake "The Muhaya Doctor," kaeleza mchango wa Schneider katika kuwaingiza vijana katika uongozi wa TAA.

Hizi koo mbili za Kizulu wazee wao wakitokea Mozambique zilikuwa na nguvu sana katika siasa za Dar es Salaam.

Schneider baada ya uhuru na Mufti Sheikh Hassan bin Ameir kutangaza kujiuzylu siasa ili ashughulike na suala la elimu kwq Waislam alianzisha taasisi inaitwa Daawat Islamiyya (Mwito Kwa Waislam) akiwa Mudir yaani Kiongozi Mkuu, Schneider akachaguliwa kuwa Katibu.

Mashado Plantan ni Mwafrika wa pili kuwa na gazeti "Zuhra," na ndiyo lilikuwa sauti ya TAA na TANU hadi TANU ilipoanzisha gazeti lake, ''Sauti ya TANU,'' mwaka wa 1956.

Yapo mengi.

Historia ya TAA, TANU na historia ya Julius Nyerere inahitaji utulivu kuieleza kwa pande zote za mazingira aliyoyakuta Dar es Salaam 1952 pale alipopokelewa ndani ya TAA na Abdulwahid Sykes.

Kinyume cha haya haitakuwa historia ya TANU kama TANU ilivyokuwa.

Listowel hakupata haya ninayokuelezeni kutoka kwa Abdul sababu ya Abdul kukataa kueleza historia kwa dhahiri yake nimeshaeleza hapa.
 
Sijaelewa hapo kwenye hitimisho, na sijabahatika kusoma ulichowahi kuandika ni kwa nini Abdul alikataa kutoa maelezo.

Kwa hiyo Bi Listowel alimuhoji Mwalimu kisha alipoenda kwa Abdul hakutoa ushirikiano?

Ni nani wengine zaidi ya Mwalimu waliopata kuhojiwa na Bi Listowel na maelezo kutumika kwenye kitabu chake?
 
Sijaelewa hapo kwenye hitimisho, na sijabahatika kusoma ulichowahi kuandika ni kwa nini Abdul alikataa kutoa maelezo.

Kwa hiyo Bi Listowel alimuhoji Mwalimu kisha alipoenda kwa Abdul hakutoa ushirikiano?

Ni nani wengine zaidi ya Mwalimu waliopata kuhojiwa na Bi Listowel na maelezo kutumika kwenye kitabu chake?
May Day,
Baada ya uhuru TANU iliamua kuandika historia yake wakati wenyewe wenye TANU wako hai ili wawe na historia ambayo wao wenyewe wanaikubali.

Fikra hii ilikuja katika mazungumzo kati ya Mwalimu Nyerere, Dossa Aziz, Mwalimu Kihere na Abdul Sykes.

Jukumu hili alipewa Abdul kwa kuwa yeye amekulia ndani ya chama cha TAA baba yake akiwa muasiai wa TAA na kiongozi na yeye mtoto akiwa kiongozi wa TAA na muasisi wa TANU.

Ikachukuliwa kuwa atakuwa anajua mengi.

Mwalimu Nyerere akamchagua Dr. Wilbard Klerruu amsaidie Abdul katika kazi ile ya kuandika historia ile.

Abdul alirejea katika ofisi yake TAA na akaanza kuandika akitumia nyaraka za TAA na TANU alizokuwanazo pamoja na mswada wa kitabu alichoandika baba yake kuhusu maisha yake kabla hajafa mwaka wa 1949.

Mradi huu ukaingia katika matatizo kuhusu historia yenyewe ya TANU kama hivi tunavyoshuhudia leo.

Abdul Sykes akajitoa katika mradi ule lakini Dr. Klerruu alikamilisha kazi ile ingawa kwa wakati ule hakikuchapwa kitabu.

Abdul alijitoa katika mradi ule kama njia ya kuepusha sintofahamu baina yake yeye na Nyerere kuhusu TANU.

Sasa Judith Listowel alipokuja kuonana na Abdul Sykes si kuwa Abdul hakutoa ushirikiano alimweleza historia ya TANU kama vile Nyerere alivyokuwa anapenda ielezwe.

Lakini inaelekea kuwa Listowel katika ''comparison of notes,'' na watu wengine walimwambia kuwa Abdul hakumweleza ukweli wa historia ya TANU.

Abdul hadi anaingia kaburini hakueleza mchango wake au wa baba yake au wa mdogo wake Ally katika TAA, TANU na uhuru wa Tanganyika na TANU ilipoandika historia yake kupitia Chuo Cha CCM Kivukoni, jina la Abdul halikuwamo katika kitabu.

Listowel alimhoji Dr. Vedasto Kyaruzi na Denis Pombeah.

Abdul na Ally Sykes walikuja kutambuliwa kuwa walitoa mchango katika uhuru wa Tanganyika baada ya miaka 50 na kutunukiwa Medali ya Mwenge wa Uhuru na Rais Kikwete katika Kumbukumbu ya Miaka ya 50 ya Uhuru wa Tanganyika mwaka wa 2011.

1572839778426.png

Medali ya Mwenge wa Uhuru ya Abdul Sykes aliyotunukiwa ''post humous''
 
Je kulikua na ugomvi binafsi baina yao? Je wewe Mzee Said Kwa nafasi yako unahisi nini kilisababisha hadi Abdul Sykes akajiweka pembeni? Hasa ukizingatia Nyerere alishamuamini na kumpatia msaidizi wa kuandika Historia ya Tanu
 
Asiposemwa Sykes wewe humezi mate
Njinjo,
Historia ya Abdul Sykes katika historia ya Tanganyika imekuwa mfano wa Rip Van Winkle mtu aliyelala usingizi kisha akaamka miaka mingi baadae na kukuta kila kitu kimebadilika.

Nilikuwa nacheka kimoyomoyo nilipokuwa namsoma Lady Judith Listowel anavyoeleza mkutano wa Mwalimu Nyerere, Abdul Sykes, Ally Sykes Dossa Aziz na John Rupia kuhusu kikao cha kuibadili TAA kuwa TANU.

Maggid Mjengwa akawa kachagua kipande hiki kukitafsiri na kuwawekea watu wasome waone jinsi Nyerere alivyounda TANU.

Kuna mtu alipatapo kuniuliza kwa nini namtaja sana Abdul katika historia ya TANU?

Jibu langu kwake lilikuwa je, unaweza kutaja siasa ya ujamaa au ujamaa vijijini bila kumtaja Nyerere?

Jibu lake likawa kuwa haiwezekani kuandika ujamaa Tanzania bila kutaja jina la Mwalimu Nyerere.

Nikamwambia unapotaja historia ya TANU na Nyerere wengi wanaijua ile historia rasmi.

Hapo mimi ndipo ninapoingia na historia ya TANU kama ninavyoifahamu na historia hii haiweze kukamilika bila kumtaja Abdul Sykes.

Nadhani kuna walichojifunza kipya katika bandiko langu hilo la ikiwa kuna mtu atasema alikuwa anajua historia hiyo niliyoeleza kumuongozea Maggid Mjengwa itakuwa vyema ajitokeze.

Abdul Sykes hakwepeki katika historia ya TANU, historia ya Nyerere na uhuru wa Tanganyika.

Nimeandika kitabu kizima cha maisha yake na kitabu kimebadili historia nzima ya uhuru wa Tanganyika.
 
Je kulikua na ugomvi binafsi baina yao? Je wewe Mzee Said Kwa nafasi yako unahisi nini kilisababisha hadi Abdul Sykes akajiweka pembeni? Hasa ukizingatia Nyerere alishamuamini na kumpatia msaidizi wa kuandika Historia ya Tanu
Nemo...
This is the magic of Abdul Sykes...
Huwezi kutosheka na yeye utataka kujua mengi zaidi na zaidi kuhusu mtu huyu.

Jonathan Glassman mmoja wa mabingwa wa African History alinibeba msobe msobe tena bila mwaliko rasmi kwenda Northwestern University, Evanston Chicago tukafanye mjadala baada ya kunisikia University of Iowa namzungumza Abdul Sykes katika historia ya Tanganyika.

1572844710594.png

Northwestern University, Chicago

Binadamu anapanga na Mungu anapanga.
Leo Abdul Sykes anatajwa katika historia ya uhuru wa Tanganyika kama vile yu hai.

Jopo la waandishi wa historia ya TANU wa Chuo Cha CCM Kivukoni walikataa kupokea "notes," za Abdul Sykes wakati wanaandika historia ya TANU.

Hivi ndivyo walivyomfuta Abdul Sykes katika historia ya TANU.

Hapajakuwa na ugomvi baina ya wazalendo hawa lakini uhuru ulikuja na changamoto mpya wengi hawakuzitegemea.

Moja ya changamoto ni hii ambayo tunajadili hapa kuhusu historia ya TANU.

Abdul hakuona sababu ya kuvutana kwenye historia ya TANU na ndiyo akajitoa katika uandishi wake.

Abdul alijua kuwa TANU was the ultimate prize na yeyote yule ambae jina lake litahusishwa na chama hicho hatoweza kufutika katika historia ya Tanganyika hadi kiama.

Hili si jambo dogo.
 
Je kulikua na ugomvi binafsi baina yao? Je wewe Mzee Said Kwa nafasi yako unahisi nini kilisababisha hadi Abdul Sykes akajiweka pembeni? Hasa ukizingatia Nyerere alishamuamini na kumpatia msaidizi wa kuandika Historia ya Tanu
Tatizo kubwa la Mwanahistoria wetu huyu Mzee said hayupo tayari kabisa kueleza mapungufu ya kina Sykes, labda kwa makusudi au hakujishughulisha kabisa kuangalia upande huo.

Yaani alimradi walihusika kwa hili ama lile basi wao walikuwa binaadamu wa kipekee kabisa kwake.

Lazima kuna jambo nyuma ya Mzeee Abdul kususa, na Dr Kleruu kuamua kuendelea na mradi bila ushiriki wa Mzee Abdul, na Mzee Said kamwe hawezi kukwambia jambo negative la the Sykes brothers.

Binafsi sikubaliani sana na mambo kadhaa anayosisitiza Mzee Said kuhusu TANU ilivyoasisiwa, na uzuri ni kwamba Mzee Said mwenyewe alishaninanga ya kuwa sijui lolote kuhusu historia ya TANU, na wala mimi sijamkatalia kwa hilo...ni kweli sijui maana sikuwepo wakati huo, ila huwa najitahidi sana kuunganisha dots kwa kila ninaloelezwa/kusoma, na nikiona dots zinakataa kuungana basi nitatikisa kichwa tu.

Huenda Mzee Abdul alieleza baadhi ya mambo ambayo yaliyosa 'uzito' (najaribu kutumia neno lisilokosea Mtu heshima) ambapo ilipelekea kalamu ya Dr Kleruu kupata kigugumizi, jambo lililomghafirisha Mzee Abdul na kuamua kususia.

Ila Mzee Said yeye ni kama anailazimisha jamii kwamba Mzee Abdul/Sykes brothers walikuwa 'parfect' na kila wanachosema ni sahihi 100% na tukubaliane nao tu.
 
Tatizo kubwa la Mwanahistoria wetu huyu Mzee said hayupo tayari kabisa kueleza mapungufu ya kina Sykes, labda kwa makusudi au hakujishughulisha kabisa kuangalia upande huo.

Yaani alimradi walihusika kwa hili ama lile basi wao walikuwa binaadamu wa kipekee kabisa kwake.

Lazima kuna jambo nyuma ya Mzeee Abdul kususa, na Dr Kleruu kuamua kuendelea na mradi bila ushiriki wa Mzee Abdul, na Mzee Said kamwe hawezi kukwambia jambo negative la the Sykes brothers.

Binafsi sikubaliani sana na mambo kadhaa anayosisitiza Mzee Said kuhusu TANU ilivyoasisiwa, na uzuri ni kwamba Mzee Said mwenyewe alishaninanga ya kuwa sijui lolote kuhusu historia ya TANU, na wala mimi sijamkatalia kwa hilo...ni kweli sijui maana sikuwepo wakati huo, ila huwa najitahidi sana kuunganisha dots kwa kila ninaloelezwa/kusoma, na nikiona dots zinakataa kuungana basi nitatikisa kichwa tu.

Huenda Mzee Abdul alieleza baadhi ya mambo ambayo yaliyosa 'uzito' (najaribu kutumia neno lisilokosea Mtu heshima) ambapo ilipelekea kalamu ya Dr Kleruu kupata kigugumizi, jambo lililomghafirisha Mzee Abdul na kuamua kususia.

Ila Mzee Said yeye ni kama anailazimisha jamii kwamba Mzee Abdul/Sykes brothers walikuwa 'perfect' na kila wanachosema ni sahihi 100% na tukubaliane nao tu.
May Day,
Napenda kwanza kabisa kukugusia kuhusu vipi tunaweza kufanya mjadala wa maana na wenye heshima baina yetu na mjadala huu ukawa na tija kwetu sote pamoja na hawa wanaotusikiliza.

Jiepushe na lugha mfano wa hii, ''mwanahistoria wetu huyu,'' ''kususa.'' na mfano wa haya.
Hii ni lugha ya kejeli.

Mimi si mwanahistoria wa yeyote awaye yule.

Abdul Sykes hakususa ila alijitoa katika ule mradi kwa sababu ilimdhihirikia kuwa historia iliyokuwa inatakiwa kuandikwa si historia ya kweli ya TANU kama yeye anavyoijua.

Hapa nitapenda kuwafahamisha wasomaji wetu kuwa katika wale waasisi tisa wa African Association mwaka wa 1929 - Kleist Sykes, Cecil Matola, Ibrahim Hamisi, Zibe Kidasi, Rawson Watts, Mzee bin Sudi, Suleiman Majisu, Ali Said Mpima, Raikes Kusi, katika hawa ni Kleist peke yake ndiye aliyenyanyua kalamu kuandika maisha yake na hivi ndivyo ndani ya mswada wake huu tukapata majina ya waasisi hawa na historia nzima ya African Association, vinginevyo leo tusingeijua historia hii.

Mswada huu alikuwanao Abdul Sykes baada ya kifo cha baba yake mwaka wa 1949 na mwaka wa 1968 alimpa binti yake Aisha ''Daisy,'' Sykes wakati huo mwanafunzi University of East Africa, Dar es Salaam na akiwa mwanafunzi wa historia chini ya John Iliffe.

Mswada huu ukatolewa hadharani kama ''seminar paper,'' mwaka wa 1968 na uko Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, East Africana.

Mwaka wa 1973 hii ''seminar paper,'' ikachapwa kama sura ndani ya kitabu, ''Modern Tanzanians,'' kitabu kilichohaririwa na John Iliffe (Daisy Sykes Buruku, ‘The Townsman: Kleist Sykes’, in Iliffe (ed) Modern Tanzanians, Nairobi, 1973, pp. 95 -114).

Ikiwa TANU asili yake ni TAA hakuna njia ambayo tunaweza kukwepa mswada huu katika utafiti wa historia ya TANU.

Mswada huu ni moja ya nyaraka ambazo Abdul alitumia katika kuandika historia ya TANU pamoja na nyaraka nyingine ambazo zilikuwa mikononi kwake kutoka kwa baba yake kama secretary wa African Association na nyaraka zake mwenyewe pia kama secretary wa TAA 1950 na kaimu president 1951 baada ya Dr. Vedasto Kyaruzi kupewa uhamisho kwenda Kingolwira kisha Nzega.

Baada ya yeye kujitoa katika ule mradi wa kuandika historia ya TANU na kumwacha Dr. Wilbard Klerruu, ni wazi Klerruu hakuwa na moja alijualo kuhusu historia ya TANU na harakati za kudai uhuru wa Tanganyika kumzidi Abdul Sykes.

Nataka msomaji ajiulize Dr. Klerruu ikiwa aliendelea na mradi ule atakuwa anaandika historia ile kwa kutumia vyanzo vipi?

Nyaraka hizi zilihifadhiwa kwa zaidi ya miaka 30 na hakuna mtafiti yeyote aliyepata fursa ya kuziona hadi mimi nilipofunguliwa nyaraka hizi na Ally Sykes mwaka wa 1985 na kuniruhusu kuzitumia kuandika kitabu cha maisha ya kaka yake na katika maisha yake nikaeleza historia ya TANU kama nilivyoisoma katika nyaraka zile.

May Day,
Naona unatumia neno, ''Mzee Abdul,'' kutumia neno ''Mzee,''unaweza kumpotezea msomaji fikra ya kuona hali halisi ya Abdul Sykes.

Wakati Abdul anachukua uongozi wa TAA mwaka wa 1950 alikuwa na umri wa miaka 26 na amefariki mwaka wa 1968 akiwa na miaka 44.

Tunaweza kusema bado alikuwa kijana.
Umezungumza kuhusu upungufu wa Sykes.

Hakuna binadamu aliyekamilika kwani ukamilifu ni wake Allah peke yake.
Kama upo upungufu una haki ya kuueleza.

Ukweli ni kuwa hakuna mtu aneijua historia ya TANU kunishinda na nalisema hili kwa shingo kutoa na kwa kinywa kipana.

Kila aliyekuja na historia ya TANU ambayo siyo, kuanzia Dr. Vedasto Kyaruzi hadi Pius Msekwa nimewajibu kuwasahihisha na wahariri wa magazeti ya kuheshimika wamechapa makala zangu achilia mbali kuwa nimesahihisha kitabu cha Chuo Cha CCM Kivukoni kilichoandika historia ya TANU.

1572906014361.png

Leo hii si mimi tu peke yangu ninaejua sababu ya Abdul kujitoa katika mradi ule wa kuandika historia ya TANU.

Mwaka wa 1981 wakati Chuo Cha CCM Kivukoni wanaandika historia ya TANU, mmoja wa wanajopo lile la waandishi jina lake Hassan Upeka alileta katika jopo ''notes,'' alizopata kuandika kutokana na mahojiano na Abdul Sykes kuhusu historia ya TANU, Mwenyekiti wa jopo lile alikataa kupokea zile ''notes,'' kwa kusema kuwa historia inayoandikwa haina uhusiano wowote na Abdulwahid Sykes.

May Day,
Kabla ya kuandika maisha ya Abdul Sykes wengi hamkujua historia yake na mchango wake si kwa TAA na TANU bali hata kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Kwa kumrejesha Abdul Sykes katika historia ya TANU, Abdul kaja na wenzake wengi waliosahaulika, wazalendo ambao wamefanya makubwa katika historia ya uhuru wa Tanganyika.


HISTORIA YA TANU ABUBAKAR ULOTU.jpg
SYKES BOOK ALL EDITIONS.jpg
 
Tatizo kubwa la Mwanahistoria wetu huyu Mzee said hayupo tayari kabisa kueleza mapungufu ya kina Sykes, labda kwa makusudi au hakujishughulisha kabisa kuangalia upande huo.

Yaani alimradi walihusika kwa hili ama lile basi wao walikuwa binaadamu wa kipekee kabisa kwake.

Lazima kuna jambo nyuma ya Mzeee Abdul kususa, na Dr Kleruu kuamua kuendelea na mradi bila ushiriki wa Mzee Abdul, na Mzee Said kamwe hawezi kukwambia jambo negative la the Sykes brothers.

Binafsi sikubaliani sana na mambo kadhaa anayosisitiza Mzee Said kuhusu TANU ilivyoasisiwa, na uzuri ni kwamba Mzee Said mwenyewe alishaninanga ya kuwa sijui lolote kuhusu historia ya TANU, na wala mimi sijamkatalia kwa hilo...ni kweli sijui maana sikuwepo wakati huo, ila huwa najitahidi sana kuunganisha dots kwa kila ninaloelezwa/kusoma, na nikiona dots zinakataa kuungana basi nitatikisa kichwa tu.

Huenda Mzee Abdul alieleza baadhi ya mambo ambayo yaliyosa 'uzito' (najaribu kutumia neno lisilokosea Mtu heshima) ambapo ilipelekea kalamu ya Dr Kleruu kupata kigugumizi, jambo lililomghafirisha Mzee Abdul na kuamua kususia.

Ila Mzee Said yeye ni kama anailazimisha jamii kwamba Mzee Abdul/Sykes brothers walikuwa 'parfect' na kila wanachosema ni sahihi 100% na tukubaliane nao tu.
Haya yanafanana na ya bunge la katiba 2014.Watu walipewa dhamana ya kuliendesha bunge wakalivuruga na waliokuwa tayari kutenda haki wakakataa kushiriki kuvuruga haki,viongozi walichowaambia raia ikawa ni tofauti na mchakato wa katiba ukauwawq kibudu na Samwel Sitta ,Mungu amsamehe hakujua atendalo.
 
Haya yanafanana na ya bunge la katiba 2014.Watu walipewa dhamana ya kuliendesha bunge wakalivuruga na waliokuwa tayari kutenda haki wakakataa kushiriki kuvuruga haki,viongozi walichowaambia raia ikawa ni tofauti na mchakato wa katiba ukauwawq kibudu na Samwel Sitta ,Mungu amsamehe hakujua atendalo.

Mzee Said

Umewahi kupata vitisho katika kuandika Historia ya TANU
 
Njinjo,
Historia ya Abdul Sykes katika historia ya Tanganyika imekuwa mfano wa Rip Van Winkle mtu aliyelala usingizi kisha akaamka miaka mingi baadae na kukuta kila kitu kimebadilika.

Nilikuwa nacheka kimoyomoyo nilipokuwa namsoma Lady Judith Listowel anavyoeleza mkutano wa Mwalimu Nyerere, Abdul Sykes, Ally Sykes Dossa Aziz na John Rupia kuhusu kikao cha kuibadili TAA kuwa TANU.

Maggid Mjengwa akawa kachagua kipande hiki kukitafsiri na kuwawekea watu wasome waone jinsi Nyerere alivyounda TANU.

Kuna mtu alipatapo kuniuliza kwa nini namtaja sana Abdul katika historia ya TANU?

Jibu langu kwake lilikuwa je, unaweza kutaja siasa ya ujamaa au ujamaa vijijini bila kumtaja Nyerere?

Jibu lake likawa kuwa haiwezekani kuandika ujamaa Tanzania bila kutaja jina la Mwalimu Nyerere.

Nikamwambia unapotaja historia ya TANU na Nyerere wengi wanaijua ile historia rasmi.

Hapo mimi ndipo ninapoingia na historia ya TANU kama ninavyoifahamu na historia hii haiweze kukamilika bila kumtaja Abdul Sykes.

Nadhani kuna walichojifunza kipya katika bandiko langu hilo la ikiwa kuna mtu atasema alikuwa anajua historia hiyo niliyoeleza kumuongozea Maggid Mjengwa itakuwa vyema ajitokeze.

Abdul Sykes hakwepeki katika historia ya TANU, historia ya Nyerere na uhuru wa Tanganyika.

Nimeandika kitabu kizima cha maisha yake na kitabu kimebadili historia nzima ya uhuru wa Tanganyika.
Mzee wangu,
Kwa msingi ya hoja yako sidhani kwamba unataka kusema kwamba Nyerere alimtoa Sykes katika historia ya TANU na wala sifikiri kwamba unataka kusema kwamba kulikuwa na POWER strugle kati ya SYKES na NYERERE..

Binafsi nafikiri unachotaka ni kutaka kuweka kumbukumbu sawa kwamba SYKES alikuwa na mchango mkubwa sana katika kuhakikisha Nyerere anakubalika ndani ya MZIZIMA pamoja na UKRISTO wake na kwamba SYKES kwa hekima kabisa alichagua kutokutaka kujiweka juu kama shujaa wa historia baada ya kumkabidhi Nyerere nafasi ya kuwa shujaa wa Watanganyika.

Kwa maana hio basi sidhani kama kuna tatizo kama Historia ya Uhuru wa Tanganyika na TANU itabaki kama ilivyo kwa sasa kama sehemu ya kuhakikisha kwamba Nyerere anaendelea kuwa shujaa wa uhuru na SYKES anabaki kuwa sehemu ya mashujaa wengi ambao wamo pembeni ya Historia kama ambavyo tunafahamu.Endelea kutuhabarisha ili tufahamu zaidi.
 
Mzee wangu,
Kwa msingi ya hoja yako sidhani kwamba unataka kusema kwamba Nyerere alimtoa Sykes katika historia ya TANU na wala sifikiri kwamba unataka kusema kwamba kulikuwa na POWER strugle kati ya SYKES na NYERERE..

Binafsi nafikiri unachotaka ni kutaka kuweka kumbukumbu sawa kwamba SYKES alikuwa na mchango mkubwa sana katika kuhakikisha Nyerere anakubalika ndani ya MZIZIMA pamoja na UKRISTO wake na kwamba SYKES kwa hekima kabisa alichagua kutokutaka kujiweka juu kama shujaa wa historia baada ya kumkabidhi Nyerere nafasi ya kuwa shujaa wa Watanganyika.

Kwa maana hio basi sidhani kama kuna tatizo kama Historia ya Uhuru wa Tanganyika na TANU itabaki kama ilivyo kwa sasa kama sehemu ya kuhakikisha kwamba Nyerere anaendelea kuwa shujaa wa uhuru na SYKES anabaki kuwa sehemu ya mashujaa wengi ambao wamo pembeni ya Historia kama ambavyo tunafahamu.Endelea kutuhabarisha ili tufahamu zaidi.
Ondoza,
Lakini Abdul Sykes hayuko katika historia ya uhuru wa Tanganyika hatajwi popote.

Jopo la Chuo cha CCM Kivukoni la waandishi wa historia ya TANU walikataa kumtia kwenye historia ya TANU.

Hakuna aliyejua mchango wake hadi mimi nilipoandika kitabu cha maisha yake mwaka wa 1998.

Historia ya TANU haipo tena kama ilivyokuwa zamani.

Kitabu cha Abdul Sykes kimebadilisha historia nzima ya TANU, Nyerere na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kleist Sykes katibu muasisi wa African Association 1929 ametiwa ndani ya Dictionary of African Biography (DAB)Oxford University Press New York, 2011, yeye na wanae kama watu walioleta mabadiliko makubwa katika mwamko wa Waafrika wa Tanganyika kujikomboa na ukoloni.

Huu ulikuwa mradi wa Harvard na Oxford University Press New York.

Hizi ni volume sita za historia ya Waafrika wazalendo barani Afrika.

Nimeshiriki katika mradi huu kama mwandishi na mshauri.

Unaweza wewe kutamani historia ibakie kama ilivyotakiwa lakini elimu sifa yake moja kubwa ni kuongezeka kila uchao.

Leo ni muhali mkubwa Abdul Sykes na wale wote aliokuwanao wakati wa kupigania uhuru kuwa pembeni ya historia hii wawe Kamachumu kama Ali Migeyo au Mwanza na Siha kama Paul Bomani na Chief David Kidaha Makwaia.
 
Ondoza,
Lakini Abdul Sykes hayuko katika historia ya uhuru wa Tanganyika hatajwi popote.

Jopo la Chuo cha CCM Kivukoni la waandishi wa historia ya TANU walikataa kumtia kwenye historia ya TANU.

Hakuna aliyejua mchango wake hadi mimi nilipoandika kitabu cha maisha yake.

Historia ya TANU haipo tena kama ilivyokuwa zamani.

Kitabu cha Abdul Sykes kimebadilisha historia nzima ya TANU, Nyerere na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kleist Sykes katibu muasisi wa African Association 1929 ametiwa ndani ya Dictionary of African Biography (DAB)Oxford University Press New York, 2011, yeye na wanae kama watu walioleta mabadiliko makubwa katika mwamko wa Waafrika wa Tanganyika kujikomboa na ukoloni.

Huu ulikuwa mradi wa Harvard na Oxford University Press New York.

Hizi ni volume sita za historia ya Waafrika wazalendo barani Afrika.

Nimeshiriki katika mradi huu kama mwandishi na mshauri.
Ni vyema kama uliandika historia yake,na ni vyema zaidi kama unaendelea kuhamasisha ili na yeye akumbukwe katika harakati hizo.Jambo la muhimu kama mwanazuoni ni kuhakikisha suala hili linaibua mjadala wa kisomi na sio wa kiitikadi kwani katika uandishi wa historia ile inawezekana kabisa kulikuwa na masuala ambayo yalipelekea omission hio ingawa naamini kabisa hakukuwa na POWER STRUGLE.

Hivyo basi nikushukuru kwa ulilofanya,ningependa iwapo ungenipatia Jina kamili la kitabu hicho kwani napenda kufahamu zaidi na huenda nikahamasika kuchimba zaidi kuhusu historia adhimu ya Taifa Letu.Asante
 
Ni vyema kama uliandika historia yake,na ni vyema zaidi kama unaendelea kuhamasisha ili na yeye akumbukwe katika harakati hizo.Jambo la muhimu kama mwanazuoni ni kuhakikisha suala hili linaibua mjadala wa kisomi na sio wa kiitikadi kwani katika uandishi wa historia ile inawezekana kabisa kulikuwa na masuala ambayo yalipelekea omission hio ingawa naamini kabisa hakukuwa na POWER STRUGLE.

Hivyo basi nikushukuru kwa ulilofanya,ningependa iwapo ungenipatia Jina kamili la kitabu hicho kwani napenda kufahamu zaidi na huenda nikahamasika kuchimba zaidi kuhusu historia adhimu ya Taifa Letu.Asante
Ondoza

tapatalk_jpeg_1571891272846.jpeg
 
Mzee Said

Umewahi kupata vitisho katika kuandika Historia ya TANU
Nemo...
Hili swali uliloniuliza la mimi kutishwa kwa ajili ya kuandika historia ya TANU kila mara watu huniuliza.

Hapa Majlis imetokea mara nyingi tutakuwa tunafanya mjadala na mtu na kwa hakika ni tabu sana kwangu mimi mtu kunishinda kuhusu historia hii na sababu ni kuwa waliounda TANU mimi ni mzao wao kwa hiyo nimeishi kwenye nyumba za waliopigania uhuru na walioona kila kitu kwa macho yao wenyewe.

Historia ya babu yangu Salum Abdallah nimeihadithia mara kadhaa hapa jinsi alivyopambana na Waingereza katika migomo mitatu aliyoongoza akiwa mfanyakazi wa Tanganyika Railways 1947, 1949 na 1960 na vipi alikuwa akihudhuria mikutano ya siri ya kuunda TANU Tabora, Western Province 1953 na akawa mmoja wa waasisi wa TANU 1954 na 1955 akawa rais muasisi wa Tanganyika Railways African Union (TRAU).

Kwa ajili hii nawashinda wengi kwa hoja na ushahidi na wapo wanaostahamili na wapo wale mara wananiita gaidi ambae serikali inastahili kuniweka jela.

Watu kama hawa wengi wao hutoa vitisho vya kila aina kwa maneno.

Sababu kubwa ya wao kusema hivi wanaona majina mengi katika harakati hizi ni ya Waislam na wao hawapendi jambo hili.

Kwao wao hii ni historia mpya ambayo hawajapatapo kusomeshwa shule wala mahali popote pale.

Miaka hii ya karibuni vitisho naweza kusema vimetoweka kabisa ila mara moja moja yanakuwapo matusi kwa ajili ya ghadhabu na taharuki.

Akili zao zinakataa kuamini ukweli wanaousikia kutoka kwangu ingawa sehemu ya akili inamwambia kuwa huu hauwezi kuwa uongo.
 
Nemo...
Hili swali uliloniuliza la mimi kutishwa kwa ajili ya kuandika historia ya TANU kila mara watu huniuliza.

Hapa Majlis imetokea mara nyingi tutakuwa tunafanya mjadala na mtu na kwa hakika ni tabu sana kwangu mimi mtu kunishinda kuhusu historia hii na sababu ni kuwa waliounda TANU mimi ni mzao wao kwa hiyo nimeishi kwenye nyumba za waliopigania uhuru na walioona kila kitu kwa macho yao wenyewe.

Historia ya babu yangu Salum Abdallah nimeihadithia mara kadhaa hapa jinsi alivyopambana na Waingereza katika migomo mitatu aliyoongoza akiwa mfanyakazi wa Tanganyika Railways 1947, 1949 na 1960 na vipi alikuwa akihudhuria mikutano ya siri ya kuunda TANU Tabora, Western Province 1953 na akawa mmoja wa waasisi wa TANU 1954 na 1955 akawa rais muasisi wa Tanganyika Railways African Union (TRAU).

Kwa ajili hii nawashinda wengi kwa hoja na ushahidi na wapo wanaostahamili na wapo wale mara wananiita gaidi ambae serikali inastahili kuniweka jela.

Watu kama hawa wengi wao hutoa vitisho vya kila aina kwa maneno.

Sababu kubwa ya wao kusema hivi wanona majina mengi katika harakati hizi ni ya Waislam na wao hawapendi jambo hili.

Kwao wao hii ni historia mpya ambayo hawajapatapo kusomeshwa shule wala mahali popote pale.

Miaka hii karibuni vitisho naweza kusema vimetoweka kabisa ila mara moja moja yanakuwapo matusi kwa ajili ya ghadhabu na taharuki.

Akili zao zinakataa kuamini ukweli wanaousikia kutoka kwangu ingawa sehemu ya akili inamwambia kuwa huu hauwezi kuwa uongo.

Kusema ukweli hata mimi ni mfuatiliaji mzuri wa historia unayotupatia, kuna vitu nisingevisikia sehemu yoyote ila kwako, kila la heri
 
Back
Top Bottom