Bongo lala Kajala ilikuwa lazima aachike na Harmonize

twende kazi

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
1,520
Reaction score
461
Kijana kampenda kweli yule dada, shida dada yule hana mipango anawaza kutumia pesa tu na si kuzitafuta.

Amepata fursa ya kuwa manager ili ajipatie kipato halali KUPITIA ubunifu wake na kujituma lakini maskini ya Mungu dada lile ni bongo lala kwake umeneja ulikuwa ni mzigo mzito sana.

Dada yule hakuwa na morali ya kuwa sehemu ya kuongeza kipato badala yake alikuwa na kiu ya kupunguza kipato tu. Na hili ni funzo kwa vijana wote unapotaka kuwa na mwanamke wa maisha yako usiangalie msambwanda tu, omba Mungu upate mwanamke mwenye akili.

Ukipata jitu linawaza kula bata na udangaji tu utaumia sana na utafifisha sana ndoto zako za kupata maisha bora.

Super Star Konde boy tuliza akili na kazi, saivi East Africa umemaliza nenda Africa sasa.
 
Penzi ni siti ya daladala anatoka mtu anaingia mtu haina kinyaa
 
Wakirudiana je? Mahusiano ya kibongo sio ya kuongelea au kuchagua upande.
 
"Akipendacho binti wahuni tunanunua ikifika mida ya *** asije akasumbua..Deka unahonga laki unaulizia chenji ,konde amehonga gari mbili tena zote range." - Rajabu
 
Hivi hili neno "Tunachokijua" kila uzi
Ni kitu gani tena huko Dasilamu?
 
Alitakiwa amzalishe ndio angetulia.
 
Hivi hili neno "Tunachokijua" kila uzi
Ni kitu gani tena huko Dasilamu?
Nadhani ni format ya thread inavyotakiwa kuwa, pale mwisho kwa sisi wahenga wa jumbo forum ilikuwa ukishaandika yako mwishoni lazima uweke ile "my take" ambayo nadhani ndo hiyo "tunachokijua"..sina uhakika though.
 
Hivi hilo jina baba levo analomuita Harmo lina maana gani?
 
Huwa sielewi Harmo anaimba nini siku izi...nyimbo za mwanzon alinikosha sanaa...mfn nyimbo kama bed room ilikaa poa sanaa due ilihamasisha mle 6*6....siku izI anaishia kukohoa tu hata simuelewi
 
Jamaa mapenzi yakamlemea mpaka akayaweka kwenye kazi. Penzi kitovu cha uzembe.
 
Ile kauli Yake " umri nao ni number tu" imeshapoteza maana Sasa😂
 
Kwahyo kwenye hii second break out ni Kajala ndio kaumia?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…