Bongo Movie mnakera, kwanini hambadiliki?

Bongo Movie mnakera, kwanini hambadiliki?

Siku moja ray kaigiza maisha ya kijijini lakini pamba anazopiga sasa, yan mpaka nikajihisi naangalia maigizo yale ya jukwaani, enzi zile
 
Waigizaji wa Bongo hawaishi vituko. Angalia huyo jambazi alivua viatu na kwenda kuvamia!
3c650f52319611e3a98422000aa80fc9_7.jpg
 
Hivi badogo kuna bongo movie...? Nilishaga sahau mimi ni mwendesha wa series tu.
 
Mimi najiulizaga scripts wanaandika au maneno wanatunga palepale?
Maana wanaongea kama wanawaza, haileti hisia, hawavai uhusika, ukiangalia ni kama watu wanaongea tu

Kurefusha movie kingine, mtu yupo beach tutututururuuu mziki tu unaenda dakika 10, jamani loh

Mavazi bado sana

Mtu anaact kijijini maisha magumu, ameshonea weaving linang'aa


I think its time wainvest kwenye tasnia yao, wafanye vitu kiprofession zaidi, wakuwe to other levels
 
Movie mbaya alafu mnatulazimisha tununue....Shenz type!!! hata mtupe bure hizo cd zenu tutawapa watoto wetu wazichezee kama toy
 
Mimi najiulizaga scripts wanaandika au maneno wanatunga palepale?
Maana wanaongea kama wanawaza, haileti hisia, hawavai uhusika, ukiangalia ni kama watu wanaongea tu

Kurefusha movie kingine, mtu yupo beach tutututururuuu mziki tu unaenda dakika 10, jamani loh

Mavazi bado sana

Mtu anaact kijijini maisha magumu, ameshonea weaving linang'aa


I think its time wainvest kwenye tasnia yao, wafanye vitu kiprofession zaidi, wakuwe to other levels
Mwingine yuko home pengine ni weekend unamuona amevaa suti.
 
umenikera wewe,badala ya kuwafundisha cha kufanya wewe unawasimanga mkuu!
Tumewafundisha sana!
Humu JF kuna akina bongo movie kadhaa, Kuna @Cloud112, na Batuli. Walishapewa maoni haya waziwazi, kama hawazingatii tufanyeje sasa? Ni kuacha kuangalia movie zao
 
Mtu anakumbuka ten years ago ukutani kuna picha ya prezidaa sizonje[emoji23][emoji23]
 
Mabadiliko yanatakiwa, Tunahitaji vipaji vipya na serikali au mashirika binafsi yasaidie kuwekeza kwenye tasnia hiyo.

Na isiwe tu kipaji cha kuzaliwa nacho bali pia wasomee ili wafanye vitu vyenye akili.
 
Nilishaacha zamani sikuhizi naangalia live concert za wasanii wa kongo kina koffi werra fally ferre brigade jb karmapa wemba
moja masaa mawili na nusu
 
Kuna kipindi fulani miaka ya 2010 hadi 2013 nilikuwa naziona ktk DSTV chanel...south Africa.. . Basi kuna nimekaa na wa south africa fulani gheto...picha linaanza.. Likaja bonge la movie tittle... Tukasema hili movie....baada ya pch kuendelea NIKAANZA KUONA AIBU MM SASA... poor acting...broken english written... Broken english spoken.... Yaani wale wasouth wakawa wanauliza... HAWA wanaandika english gani?mbn siwaelewi?hatujakaa sawa WATCH PART 2.... Ehhh... Tukabadili SEHEM INGINE......HAIKUPITA muda wakazitoa bongo movie ktk program za MOVIE MAGIC.. Dstv...in South Africa...MAANA ILIKUWA NI AIBU TUPU... Sasa hazipo tena.... Dstv
 
Mi kwenye kuchanganya lugha tu ndio huwa wananiboa sana. Kiswanglish aaaarg kero tupu.
 
SABABU ZILIZONIFANYA NISIANGALIE BONGO MOVIE TENA!!
1.Wachawi wanakamatwa na Mgambo
2.Majeruhi na maiti zinabebwa kwa mikono mitupu
3.Jini anavuka barabara anaangalia kulia na kushoto anaangalia usalama kwanza
4.Risasi inachukua Dakika kumfiki mpigwaji
5.Mtu yupo na demu wake supermarket wanachukua nusu saa nzima wakati movie ina saa moja na nusu
6.Mtu akipigwa ngumi anaangalia pakuangukia kwa usalama wake
7.Milio ya Risasi kama unawasha njiti za kiberiti
8.Kahaba lazima avute sigara
9.Jambazi lazima livae koti refu na miwani meusi
10.Mganga wa kienyeji lazima awe porini,mchafu,halafu anaongea kwa ukali!
11.Kwenye subtitle mgeni anaitwa New People
12.Hospitalini wapo wao tu
13.Jambazi anavua viatu akavamia kwenye nyumba
14.Mtanga na Serengo lazima wawe walinzi
15.Jini lazima awe mwanamke
16.JB anavaa shati moja kwenye movie sita
17.Tukio linaonywshwa lilitokea mwaka 1977 halafu ukutani kuna picha ya Rais wa sasa Magu
18.Familia ya kitajiri lazima waongee kizungu Dadii!!..Mamii!!
19.Tajiri lazima amuoe maskini
20.Gereza ni nyumba ya mtu yenye madirisha ya chuma
21.Kila anayetoa habari za maisha yake ya nyuma lazma anyanyue uso juu
22.Mapenzi yanaanza pale mwanamke anapoalibikiwa na gari afu mwanaume anatokea kusaidia
23.Mlinzi wa getini lazima awe hana akili nzuri
24.Kitu pekee kinachoharibika ni Glass tu
25.jambazi laziwa awe na sura mbaya na awe ananuna muda wote
26.Movie inaanza mtoto mweusi kichwani kipilipili cha nguvu, akiwa mkubwa ni mweupe na nyele za kiarabu
Nolog Off bongo movie
Malizia na ww.
 
Back
Top Bottom