Bongo Movies Imekumbwa Na Msiba, Staa Mmoja Ajitoa Uhai Mwenyewe

Bongo Movies Imekumbwa Na Msiba, Staa Mmoja Ajitoa Uhai Mwenyewe

Ibrahim300

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2010
Posts
390
Reaction score
68
MSANII Victor Peter kutoka Bongo Movie afariki dunia kwa kujinyonga katika gesti moja iliyotambulika kwa jina la SAFARI JUNIOUR ilioko maeneo ya Kisosora huko mkoani Tanga.

Hapo pichani ni mwili wa marehemu ulivyokuwa ukipakiwa katika gari kupelekwa katika hospitali ya mkoa wa Tanga Bombo,

Chanzo cha habari kiliieleza kuwa msanii huyo alikuwa katika harakati zake za kushoot filamu yake mpya ambayo alicheza kama muhusika mkuu katika filamu hiyo.
Kilichowashangaza wenzake ni kwamba filamu iliisha jana Jumatatu 27/01/2014 na story ilimalizikia Vicktor kufa kwakujinyonga matokeo yake leo alfajiri Victor akakutwa amejinyonga kweli na kuiaga dunia, Mpaka sasa chanzo cha kifo chake bado hakijatambulika
====================================


B.jpg

victor2.jpg

Marehemu Victor Peter enzi za uhai wake.

MSANII Victor Peter kutoka Bongo Movie amefariki dunia usiku wa jana kuamkia leo 28/01/2014 kwa kujinyonga katika gest moja iliyotambulika kwa jina la SAFARI JUNIOUR ilioko maeneo ya Kisosora huko mkoani Tanga.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya mkoa wa Tanga Bombo, mmoja kati ya wasanii walioshirikishwa na marehemu katika filamu yake ya
mwisho kabla ya kujinyonga huku filamu yake ya kwanza ikiwa bado haijatoka na kuingia sokoni yenye jina la CHOZI.

Msanii huyo aliyetambulika kwa jina la usanii Koba alisema kwamba siku moja kabla ya tukio Victor alifanya nao Shuting ya filamu iliotambulika kwa jina OUR FAMILY ambayo ilikuwa ndio filamu ya marehemu Vicktor ya pili tangu ajikite katika tasnia ya filamu Bongo Movie,

MSEMAJI


Cha kushangaza ni kwamba filamu hiyo muhusika mkuu alikuwa ni marehemu Vicktor na katika filamu hiyo alicheza kwamba kuna msiba baba yake kafa na yeye mwenyewe mwisho wa filamu Picha yake hiyo mnayoiona hapo juu ilipigwa Ex na muhusika aliyecheza kama mdogo wake, Matokeo yake alivyomaliza kushut aliondoka na wasanii kadhaa wakaelekea katika ATM iliokwepo maeneo ya mjini kutoa hela ili awalipe wasanii walihusika katika kazi yake,

KABLA YA TUKIO

Kwa bahati mbaya ATM machine ikagomagoma kwa tatizo kidogo la kimtandao katika kusubiria mtandao ukae sawa marehemu Vicktor alibadilika na kuonekana kama amechanganyikiwa na kuonekana hayuko sawa, Basi kwa bahati nzuri baada ya mda mchache ATM ilikaa vizuri na yeye mwenyewe ile hali ikatulia akatoa hela wakaelekea Hospitali ya Ngamiani huko mkoani Tanga,
Kufika Ngamiani daktari akatoa tamko kwamba apelekwe Hospitali kuu Bombo.

UCHUNGUZI

Kufika Bombo akapimwa kila kitu na kukutwa mzima hana tatizo lolote lile ikabidi warudi Gest walikofikia huko maeneo ya Kisosora, Marehemu akawalipa wasanii wote na kuwauliza kuwa kuna mtu anaemdai? Wakamjibu hakuna. Kila msanii akaingia chumbani kwake na kuendelea na zake, Kwa wakati ule marehemu aliingia chumbani kwake na kwakuwa ni Self Contain si rahisi kumuona mtu akitoka nje hovyo hovyo.

TUKIO

Asubuhi yakuamkia jumanne 28/01/2014 Wasanii wenzake walimgongea mlango wakaona kimya wakapatwa na wasiwasi ikabidi wamuite mwenye Gest na kusimulia hali halisi mwenye Gest akachukua jukumu la kwenda kutoa taarifa kwa mwenye kiti wa Serikali za mitaa mwenye kiti akatoa taarifa Polisi, Gari ya Polisi ikatia timu katika eneo la tukio na kuvunja mlango wakakuta mwili wa marehemu Victor ukiwa umening'inia kama unavyoonekana hapo pichani alitumia mkanda wake mwenyewe wa kiunoni kujinyongea. Vicktor kajinyonga na kuiaga dunia.

Chanzo:masainyotambofu
 
Mwenye picha yake atuwekee mana wengine hatumfahamu ati
 
Huyo marehemu alikuwa anatafuta umaarufu, aya tushamjua rest in peace
 
Vifo vimefululiza sana kwa wasanii, Mungu azidi kuwatia wepesi wote walioondokewa na wapendwa wao.
 
Sio kila msanii wa bongo muvi ni msanii wa bongo muvi.
 
Kumbe nami ni bongo movie aisee rip brother
 
Huyo marehemu alikuwa anatafuta umaarufu, aya tushamjua rest in peace
Khaaa!!!
Afu nakutafuta ujue.
Ingia kwa kijiwe mshenzi ukamuone kaka yako kafumwa live na gasho
 
Huyo marehemu alikuwa anatafuta umaarufu, aya tushamjua rest in peace

Ndugu si vyema kuleta mizaha kwenye misiba.....watu wana majonzi ya kuondokewa na mpendwa wao........

Uungwana ni vitendo....
 
Chanzo cha kifo chake si "kujinyonga" ama?
 
Back
Top Bottom