Bongo Star Search (BSS) anzisheni program ya kupeleka vipaji American Got Talent (AGT)

Bongo Star Search (BSS) anzisheni program ya kupeleka vipaji American Got Talent (AGT)

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
7,899
Reaction score
10,415
Kwa:
Meneja wa Bongo Star Search (BSS)

Dar es Salaam, Tanzania

Yah: Kuanzisha Programu ya Kuwapeleka Washindi wa BSS Kushiriki Mashindano ya America’s Got Talent (AGT)

Natumai barua hii inakufikia ukiwa na afya njema na unaendelea vyema na juhudi za kukuza vipaji vya muziki na sanaa kupitia mashindano ya Bongo Star Search (BSS).

Ninapenda kutoa pongezi kwa juhudi zenu katika kuwawezesha vijana wenye vipaji Tanzania kupitia BSS. Mashindano haya yamekuwa chachu kubwa ya kukuza wasanii wapya na kuwapa nafasi ya kutambulika kitaifa. Hata hivyo, ili kuendeleza vipaji vya washindi zaidi ya mipaka ya Tanzania, napendekeza kuanzishwa kwa mpango wa kuwawezesha washindi wa kwanza wa BSS kushiriki katika mashindano makubwa ya kimataifa kama America’s Got Talent (AGT).

Kushiriki AGT kutawapa washindi wa BSS jukwaa pana zaidi la kimataifa, kuwafungulia milango ya fursa mpya, ikiwa ni pamoja na mikataba ya kazi, mafunzo ya hali ya juu, na uwezekano wa kukuza vipaji vyao kimataifa.

Ninaamini kuwa kwa pamoja tunaweza kuinua vipaji vya Watanzania hadi viwango vya kimataifa.
 
Kwa:
Meneja wa Bongo Star Search (BSS)

Dar es Salaam, Tanzania

Yah: Kuanzisha Programu ya Kuwapeleka Washindi wa BSS Kushiriki Mashindano ya America’s Got Talent (AGT)

Natumai barua hii inakufikia ukiwa na afya njema na unaendelea vyema na juhudi za kukuza vipaji vya muziki na sanaa kupitia mashindano ya Bongo Star Search (BSS).

Ninapenda kutoa pongezi kwa juhudi zenu katika kuwawezesha vijana wenye vipaji Tanzania kupitia BSS. Mashindano haya yamekuwa chachu kubwa ya kukuza wasanii wapya na kuwapa nafasi ya kutambulika kitaifa. Hata hivyo, ili kuendeleza vipaji vya washindi zaidi ya mipaka ya Tanzania, napendekeza kuanzishwa kwa mpango wa kuwawezesha washindi wa kwanza wa BSS kushiriki katika mashindano makubwa ya kimataifa kama America’s Got Talent (AGT).

Kushiriki AGT kutawapa washindi wa BSS jukwaa pana zaidi la kimataifa, kuwafungulia milango ya fursa mpya, ikiwa ni pamoja na mikataba ya kazi, mafunzo ya hali ya juu, na uwezekano wa kukuza vipaji vyao kimataifa.

Ninaamini kuwa kwa pamoja tunaweza kuinua vipaji vya Watanzania hadi viwango vya kimataifa.
Trump amesha wafukuza hamkomi tu

Endelezeni vya kwenu
 
Labda Sanaa zingine lkn sio kwenye uimbaji Bado Wana viwango vya chini sana.
Labda watz wapewe link kupitia wizara ya michezo watume sanaa zao huko, maana mtaani Pana vipaji hatari vinaoza tu.
Nikisema vipaji sisemi hivi vya hii miziki ya kipumbavu ya kufundisha watz ngono hapana.
 
Sasa wakienda America's Got Talent hiyo talent itakuwa ya America au ya Bongo?

Kwani Watanzania hawawezi kufanya vitu vyao vizuri vikatambulika kimataifa bila kufanywa na AGT?
 
Zile level hakuna wa kuweka mguu labda waende got talent za kiafrica Africa
 
Sasa wakienda America's Got Talent hiyo talent itakuwa ya America au ya Bongo?

Kwani Watanzania hawawezi kufanya vitu vyao vizuri vikatambulika kimataifa bila kufanywa na AGT?
Unaingia chekechea ukifaulu unaenda shule ya Msingi ukifaulu unaingia sekondari ukifaulu unaingia form five na six ukifaulu unaingia chuo kikuu.
 
Unaingia chekechea ukifaulu unaenda shule ya Msingi ukifaulu unaingia sekondari ukifaulu unaingia form five na six ukifaulu unaingia chuo kikuu.
Katika dunia ya leo watu wanataka authenticity, uki Americanize muziki wako hutaweza kushindana na wenyewe Wamarekani.

Ndiyo maana Afro-Pop imekuwa very successful, mpaka Wamarekani wenyewe wameikubali, bila kupitia America's Got Talent.

There is nothing that AGT can do that Youtube and a good African management can't do.

Kitu k8ng8ne, hivi Africa 8nash8ndwa kuungana na kuanzisha kitu chake kama America's Git Talent? Mbona Ulaya wana Eurovision Song Contest?

Huoni kwamba Waafrika kutaka kupitia AGT watakuwa wanawapa nguvu sana AGT, pengine bila sababu kubwa ya muhimu?
 
Sasa American got talent si ni ya America,waafrika wanaenda kufanya nini huko sasa.
 
Back
Top Bottom