Bongo Tambarare?

Bongo Tambarare?

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
uchafu2.jpg

GARBAGE is piling up at Manzese Flyover Bridge in Dar es Salaam and city authorities seem not to care. Our Staff Photographer Bernard Rwebangira captured this ugly scene.
 
Hii picha nimeitoa kule kwa Michuzi. Nimeiangalia mara kibao na kuanza kujiuliza maswali kem kem. Moja ya maswali niliyojiuliza ni nani abebe lawama za uchafu huu?

Ni viongozi wetu (wa ngazi zote)? Ni wananchi watupao takataka ovyo ovyo? Au ni Ndivyo Miafrika Tulivyo? Nimefikiria weee...nimewaza weeee...sipati jibu hadi nikaanza kuona kizunguzungu!

Nina uhakika kabisa hapo karibu na huo uchafu kunatoa harufu. Lakini hebu mwangalie huyo dogo alivyominya hap utadhani yupo bustanini akipunga upepo. Mwenzio wala haonyeshi kukerwa na huo uchafu.

Halafu mcheki huyo jamaa aliyebeba sijui ungo (labda njegere, karanga, korosho, who knows what) huo. Hapo ukimsimamisha mwenzio atakuuzia bila hata ya kuonyesha kukereka na uchafu huo...

Why us jamani? Yaani hata usafi unatushinda? Yaani kuweka mazingira unayoishi katika hali ya usafi na yenyewe yanahitaji uwe na akili kama Einstein? Good Lord!!!

uchafu.JPG
 
Mods naomba muunganishe hii na thread ya "Lawama zimwendee nani?"
 
hii inatia aibu nchi yetu,mamlaka zinazohusika ziwajibishwa kwa ili
 
Hii picha nimeitoa kule kwa Michuzi. Nimeiangalia mara kibao na kuanza kujiuliza maswali kem kem. Moja ya maswali niliyojiuliza ni nani abebe lawama za uchafu huu?

Ni viongozi wetu (wa ngazi zote)? Ni wananchi watupao takataka ovyo ovyo? Au ni Ndivyo Miafrika Tulivyo? Nimefikiria weee...nimewaza weeee...sipati jibu hadi nikaanza kuona kizunguzungu!

Nina uhakika kabisa hapo karibu na huo uchafu kunatoa harufu. Lakini hebu mwangalie huyo dogo alivyominya hap utadhani yupo bustanini akipunga upepo. Mwenzio wala haonyeshi kukerwa na huo uchafu.

Halafu mcheki huyo jamaa aliyebeba sijui ungo (labda njegere, karanga, korosho, who knows what) huo. Hapo ukimsimamisha mwenzio atakuuzia bila hata ya kuonyesha kukereka na uchafu huo...

Why us jamani? Yaani hata usafi unatushinda? Yaani kuweka mazingira unayoishi katika hali ya usafi na yenyewe yanahitaji uwe na akili kama Einstein? Good Lord!!!

uchafu.JPG

Wananchi nao wanaboronga big time. Nimesoma kwenye shule zenye maji na makaratasi ya kutosha na bado watu wakienda kwenye 18 wanatumia mawe yenye size ya kichwa cha mtu. Vyoo vikiziba wanagoma.
 
kwa hili mkuu hakuna haja ya pesa ya kigeni,uzembe wa mamlaka husika ,wanapeana tenda za kusafisha jiji kiujanjaujanja .kampuni haina uwezo wowote ule matokeo yake ndio hay sasa, kututia aibu,kuaribu mazingira kwa hewa isiyo salama, maradhi kibao ya mlipuko.

utakuta kampuni iliyopewa tenda ina gari moja bovu kabisa,unajiuliza ilipataje tenda.

Naomba sana PPRA mtusaidia kwenye hizi zabuni.
 
Utasikia tu maskini...hatuna pesa ya kigeni!

Wakati huo huo tunaagiza mashangingi 1,000 na bei ya shangingi moja ni kati ya milioni 100 na milioni 150!!!

Ingetia moyo sana katika sherehe za miaka 32 ya CCM Kikwete na uongozi wa juu wa CCM kuwahamasisha na kushiriki katika kusafisha uchafu uliokithiri katika miji yetu mbali mbali ikiwemo Dar.
 
Wakati huo huo tunaagiza mashangingi 1,000 na bei ya shangingi moja ni kati ya milioni 100 na milioni 150!!!

Ingetia moyo sana katika sherehe za miaka 32 ya CCM Kikwete na uongozi wa juu wa CCM kuwahamasisha na kushiriki katika kusafisha uchafu uliokithiri katika miji yetu mbali mbali ikiwemo Dar.

...bro BaK, si unakumbuka Lowassa alipoingia madarakani (u-pm) ilipita safisha safisha ya nguvu, na mabustani yakaanza kupendeza?

uchafu upo ndani ya mioyo yetu. Fikiria hata Cherrie Blair alivyoshangazwa na poor sanitation inayopelekea magonjwa ya mlipuko kama Kipindupindu, halafu mijitu inakenua meno ikitanguliza lame excuses.

Hivi kweli panahitajika mpaka aje Kikwete ndio sie wananchi tutanawa mikono kabla ya kula, au kuchemsha maji kabla ya kunywa, ama kufukua mitaro ilozibwa na mifuko ya plastiki tunayoitupa wenyewe wananchi ilhali tunajua plastiki haiozi?

Kwakweli maendeleo yatakuwa magumu sana kufikiwa iwapo tutabakia tunailaumu serikali itufanyie kila kitu, wakati tumepewa akili ya kufikiria tukichimba shimo, tunaweza zichoma hizo taka!
 
utakuta kampuni iliyopewa tenda ina gari moja bovu kabisa,unajiuliza ilipataje tenda.

Ni kampuni ya mnene mmoja ndani ya chama na serikali ambaye ni lazima apate tenda hiyo hata kama anajua fika hana kampuni yenye uwezo wowote wa kubeba taka. Matokeo yake uchafu unarundikana na kukithiri. Malaria, magonjwa ya kuhara pamoja kipindupindu yanaendelea kuwaua Watanzania miaka nenda miaka rudi.
 
Jamani ukweli ni kwamba jiji la Dar lote linanuka, tofauti ni kwamba concentration ya harufu inatofautiana kutoka eneo moja kwenda jingine lakini mji mzima unanuka balaa. Shida moja ni kwamba wakazi wengi washa zoea 'acclimatize' na hali hiyo ya harufu.

Sielewi viongozi wa Dar ''Meya, et al'' wanamatatizo gani kwani ukienda Arusha na Moshi mambo swari kabisa. Mji upo clean hata gardens zipogreen zinamwagiliwa maji vizuri kabisa. Vile vile Meya wa Morogoro Prof. Ishengoma nae sina budi kumpongeza kaiweka Morogoro vizuri garderns safi inapendeza kwa keli. Dar siku zote mpaka watu wapige kelele sana ndio mtu awajibike unawezakuta bomba la maji machafu limefumka linatema harufu balaa katikati ya mji lakini hakuna anaeshtuka. Kama serikali hihi imeweza kupambana na machinga kariakoo inashindwa vipi kupambana na uchafu Dar?
 
Poverty is no excuse for this kind of filthyness... this is pathetic

When are people going to take responsibilty and be held accountable. If people who continually fail at their jobs this country will go nowhere

😡
 
Uongozi wa jiji la Dar es Salaam wote ni mbovu, kuanzia Mkuu wa Mkoa mpaka kwa Ma meya wake! Kwa kifupi Dar panazidi kuchukiza kila kukicha! Mitaro ya maji machafu inatiririka, ujenzi holela kati kati ya mji kunajengwa maghorofa kila siku wakati miundombinu haipo kuya-support. Mfano Mafuta House (BWM Towers) pale Azikiwa, umeme wa TANESCO hautoshi kuliendesha. Wanatumia jenereta. Pia kuna mtu kaniambia Citibank pia wanatumia jenereta kwenye jengo lao kwa kuwa umeme hautoshi. Transforma ni zile zile za miaka nenda rudi wakati majengo yameongezeka na matumizi pia.

Hakuna plan zozote kila kitu kinakwenda shaghala bhagala tu!
 
...bro BaK, si unakumbuka Lowassa alipoingia madarakani (u-pm) ilipita safisha safisha ya nguvu, na mabustani yakaanza kupendeza?

uchafu upo ndani ya mioyo yetu. Fikiria hata Cherrie Blair alivyoshangazwa na poor sanitation inayopelekea magonjwa ya mlipuko kama Kipindupindu, halafu mijitu inakenua meno ikitanguliza lame excuses.

Hivi kweli panahitajika mpaka aje Kikwete ndio sie wananchi tutanawa mikono kabla ya kula, au kuchemsha maji kabla ya kunywa, ama kufukua mitaro ilozibwa na mifuko ya plastiki tunayoitupa wenyewe wananchi ilhali tunajua plastiki haiozi?

Kwakweli maendeleo yatakuwa magumu sana kufikiwa iwapo tutabakia tunailaumu serikali itufanyie kila kitu, wakati tumepewa akili ya kufikiria tukichimba shimo, tunaweza zichoma hizo taka!

Serikali itaendelea kulaumiwa tu katika hili. Unakumbuka walipiga marufuku mifuko ya plasitic lakini mpaka leo bado inauzwa kama kawaida. Matokeo yake mamlaka zinazohusika kufuatilia hao wanaouza mifuko ya plastic ndizo zinaneeemeka kwa rushwa!

Seriakali gani inatoa maagizo halafu hayafuatwi na inakaa kimya?
 
Back
Top Bottom