Pre GE2025 Boniface Jacob kurejesha fomu ya kugombea Uenyekiti wa Kanda ya Pwani tarehe 05/09/2024 kwa Maandamano

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426

Meya zamani wa Kinondoni na Ubungo, ambaye ametangaza kugombea Uenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, amepanga kurejesha fomu ya kugombea uongozi huo kwa Maandamano.

Leo aliitwa Polisi Kanda Maalum ili kueleza kwanini anarejesha fomu kwa maandamano, baada ya Ufafanuzi Polisi wameahidi kuyalinda.

Maandamano hayo kabambe yataanzia Manzese, Yatapita Tandale na Kuingia Mwananyamala na Hatimaye yataishia Kinondoni Zilipo Ofisi za Kanda ya Pwani.

Soma Pia: Meya wa Zamani wa Ubungo na Kinondoni Boniface Jackob, atangaza nia kugombea Uenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Pwani

Wote Mnakaribishwa.
 
Wajinga wengi watapoteza muda kutembea kutoka Manzese hadi Ufipa halafu baadae kulalamika maisha magumu.
 
Mwamba namkubali... Ningekuwa napiga kura angepata. Hata hivyo tukutane mwakani kwenye ubunge. Una kura yangu
 
Mzee wa fitna sio?🀣

vip shekhe atarudisha lini fomu? au ataanza kukiona cha moto mapema kabla ya hapo?πŸ’
 
Mungu baba Ibariki CHADEMA
 
Maandamano bila kibali ni kosa la kisheria
 
Kwani unaitaka fomu yenyewe,kama hivyo nawe uchukue ya ujumbe wa nyumba 10.Hiyo mwachie yeye ni yake na chama chake.
mtoa hoja ambae ni mpigadebe wa boni anadai mungwana anaweza sana fitna za ndani ya chama nadhani alimaanisha pamoja na kusambaza mkwanja kama ilivyotokea Nyasa,

Lakini pia mtoa hoja akaja kumuhadaa yule shekhe ambae nae amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo nyeti ya ubosi wa kanda,

nataka tu kufahamu,
Je, shekhe nae anazijua fitna au atafedheheshwa Zaidi ya msigwa?πŸ’
 
Mlimfedhehesha kwa kumbebesha mabango au kwa namna ipi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…