Uchaguzi 2020 Bora CHADEMA mngesitisha uzinduzi wa kampeni kufuatilia hujuma za wagombea wenu kuenguliwa

Uchaguzi 2020 Bora CHADEMA mngesitisha uzinduzi wa kampeni kufuatilia hujuma za wagombea wenu kuenguliwa

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
69F599F6-0D53-4A31-8DFB-8384CFA7797A.jpeg


Baada ya kumsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara,kamanda Bensoni Kigaila, nimepoteza hata hamu ya kufuatilia uzinduzi wa kampeni kwani kwa idadi ya wagombea wa ubunge wa CHADEMA walioenguliwa mpaka sasa, naweza kusema inatisha huku msemaji mwenyewe akiweka wazi kuwa idadi ya wanaogombea udiwani ndio kubwa zaidi na angesema aiongelee, basi angetumia muda mrefu sana.

Mazingira haya kwangu mimi yananiondolea kabisa hata ile hamu ya kufuatilia huo uzinduzi kwani naona hawa mabwana kwa sasa ni kama wanatuchora tu.

Ushauri wangu ni bora kupambana kwanza juu ya hili kabla hamjaendelea na huo uzinduzi kwani hai-make sense kufanya uzinduzi huku wagombea ubunge zaidi ya 50(kwa maelezo ya Kigaila) kwa tiketi ya CHADEMA wakiwa katika hatihati ya kukosa nafasi ya kuwa wagombea huku idadi ya wagombea udiwani nchi nzima ikiwa ni kubwa zaidi.

Ni bora uongozi wa CHADEMA Taifa mkalipa uzito jambo hili vinginevyo mtavunja moyo wenzenu ambao wako katika hatihati ya kukosa haki yao ya kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa.

Napata wasiwasi kuwa huenda hata huo uzinduzi nao ukahujumiwa kama wagombea wetu walivyohujumiwa.

Hata hivyo, naungana na Bensoni Kigaila kwa aliyoyasema na kwakweli ametoa onyo kali kuhusu hujuma hizi na ninaona kuna giza nene huko mbeleni iwapo busara itakosekana hasa kwa wenye mamlaka.

Tuombe Mungu kwani "tone" ya Kigaila haikuwa ya mchezo na ni wazi wamedhamiria kudai/kutafuta haki kwa gharama yoyote.
 
Kuna team tayari imeundwa kushughulikia hilo tatizo mkuu ondoa shaka
Team hiyo itafanya nini kuunda tume mpya ?!

Sijawahi kusikia team inatengua matokeo ya tume.

Mara zote nimesikia maamuzi ya tume ni final na asiyekubali anashauriwa kwenda mahakamani.

Walipaswa wawe walisha rekebisha matatizo yote kabla ya matokeo, badala ya kuunda team baada ya matokeo.
 
Kweli kabisa hatuwezi kukubali yatokee yaliyotokea mwaka jana kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa. Jamani wagombe 60 wa ubunge wa CDM wameondolewa pamoja na wagombea 600 wa udiwani pia, hatuwezi kuendelea namna hiii!

Lazima tusimamishe mambo mpaka haki irejeshwe la sivyo nafikiri ni afadhali kugomea uchaguzi na kufanya kingine hadi kieleweke. Hakuna mgombea hata mmoja wa ccm ubunge au udiwani aliyeondolewa.
 
Wataachaje kampeni wakt wameshachukua ela za mabeberu kwa kuwadanganya kuwa wanakubalika na watashinda uchaguzi?

Inashangaza sana chama ambacho kinajinasibu kuwa kitashinda uchaguzi sasa unajiuliza inamaana chadema na usomi wao wanashindwa kujua huwezi kuunda serikali usipokuwa na wabunge wa kutosha au nia yao ni kupata Urais tu?

Lissu ameshawadanganya mabeberu kuwa watashinda na ukweli Chadema wanajua kabisa hawana ubavu wa kushinda uchaguzi ndo maana kutwa Lissu anafanya visa ili tu mabeberu waone anaonewa kuwekewe vikwazo kwa taarifa yake tutawangalia tu wala hatumgusi ataguswa na box la kura pale atakapopata chini ya 5%

Chadema wamewekeza nguvu nying kwa nafasi ya Urais wameshindwa kujua wanatakiwa kuwa na wabunge wengi ambapo hata wasipopata urais wanaweza kubadili mambo mengi kikatiba kupitia wabunge wao


 
Back
Top Bottom