Bora nichukiwe na Wana Simba SC ila ukweli huu Mchungu uliochangia Kipigo Kitakatifu cha Mzulu na Mkaburu Kaizer Chiefs FC niuseme

Bora nichukiwe na Wana Simba SC ila ukweli huu Mchungu uliochangia Kipigo Kitakatifu cha Mzulu na Mkaburu Kaizer Chiefs FC niuseme

Simba kwa Mkapa watashinda 3-1 naa ndio tutakuwa tumetoka.
 
Kama Mwamamichezo Halisi ( japo sijifichi ni mwana Simba SC ) nianze kwa Kuwapongeza Kaizer Chiefs FC kwa Ushindi wa Goli Nne na niwape pia Pole Simba SC kwa Kufungwa Mchezo huu wa Kwanza leo.

Zifuatazo ni sababu zangu Binafsi za Kiuchambuzi Mimi Krav Maga kwanini Simba SC tumefungwa na Kaizer Chiefs FC ambazo hata hivyo sikulazimishi uziamini japo unatakiwa uziheshimu kama ambavyo nami naheshimu ( nitaheshimu ) zako.

1. KUBWETEKA KWA WACHEZAJI

Huitaji Akili Kubwa ama kuona au kugundua kuwa Mafanikio ya hivi karibuni ya Simba SC yamewapa Kiburi cha Kipuuzi Wachezaji wa Simba SC kiasi cha kuanza Kubweteka wakijiona ni akina FC Barcelona.

2. MIPIRA YA KROSI NI TATIZO SUGU KWA MABEKI WA SIMBA SC

Nilidhani baada ya mwaka Juzi Kufungwa Goli Tano Tano na AS Vita na Al Ahly kwa Mipira ya Krosi Simba SC ingejifunza na Kulifanyia Kazi Ila leo Makosa haya haya ya Kutokujua Kukaba Krosi yamesababisha Beki Shomari Kapombe asababishe Kufungwa Goli 3 huku Beki Mohammed Hussein Zimbwe nae akisababisha Goli 1 ( tena la Nne ) kwa Kumzawadia Pasi ya Upendo Adui na akafumua bonge la Shuti ( Muwa )

3. UZEE KWA MABEKI WA KATI WA SIMBA SC NA KUCHOKA KWAO UPESI

Ifike mahala sasa Simba SC ijifunze ama kutokupenda Kusajili au Kung'ang'ania Wachezaji Wakongwe ( Wazee ) huku wale Vijana na wenye Uwezo kama Beki Kijana ninayemkubali sana Ame Ibrahim na David Kameta Duchu tukiacha Kuwatumia. Leo akina Wawa na Onyango wamefanya Makosa makubwa mno na laiti yangetumiwa vyema na Washambuliaji wa Kaizer Chiefs FC huenda leo tungefungwa hata Magoli 7 au 8 pale Bondeni kwa Madiba.

4. KOCHA WA SIMBA SC KUKARIRI KIKOSI NA KUKOSA PLAN B YA HARAKA

Nikiri tu kuwa Kocha Mkuu wa Simba SC Didier Gomez kweli ni Tactician ila nae sasa ajifunze Kucheza Mechi zake Kimkakati na Kimazingira zaidi kuliko Kujiamini sana na kuingia Kichwa Kichwa tu.

5. VYOMBO VYA HABARI KUPENDA KUIPA SIFA SIMBA SC ZISIZOSTAHILI

Nilitegemea kuona Vyombo vingi vya Habari nchini Tanzania ( hasa vya Michezo ) vingekuwa vinaiambia Ukweli Simba SC kuhusu Klabu ya Kaizer Chiefs Matokeo yake Kutwa tu Magazeti na Watangazaji wa Vipindi vya Michezo Kazi yao ni Kuisifia tu Kinafiki Simba SC kwa kutokujua kuwa Wanawaharibu Wachezaji kupelekea kutokuwa na Ufanisi.

6. UBOVU WA LIGI YA TANZANIA. KUDEKEZWA SANA NA TFF HUKU MWILI KUTOKUWA TAYARI KIMCHEZO

Binafsi niliwashangaa mno Wapenzi na Mashabiki wa Simba SC walipokuwa wakiibeza Klabu ya Kaizer Chiefs kwakuwa iko nafasi ya Kenda ( Tisa ) katika Ligi Kuu yao.

Watu wa Simba SC walisahau kuwa Kaizer Chiefs FC wapo katika Moja ya Ligi Kuu bora barani Afrika ambayo ni Professional League wakati yetu hapa ya VPL ni Semi - Amateur kwa sasa.

Pia sasa imefika wakati TFF kuambiwa ukweli juu ya kupenda Kuidekeza Simba SC na Kuisikiliza kwa kila walitakalo wakati kumbe hapo wanakuwa hawaijengi Klabu bali wanazidi tu Kuibomoa.

Sikuona sababu ya Simba SC kukaa karibia Siku 9 au 11 kutokucheza Mechi yoyote ile ya Kimashindano ( hasa Ligi Kuu ) kwa Kisingizio kuwa wana Mechi za Champions League na hawataki Wachezaji wao ( wetu ) Kuumizwa.

Cha Kushangaza Kaizer Chiefs FC ndani ya Siku hizo hizo ambazo Simba SC ilidekezwa na TFF kwa Kusikilizwa na kutokucheza Mechi yoyote ile ya Ligi Kuu ya VPL wao Kaizer Chiefs wameweza Kucheza Mechi zao Mbili za Ligi Kuu yao Kubwa ya PSL.

Kwangu Mimi Krav Maga naamini mojawapo ya sababu Kubwa ya Simba SC yangu kupokea Kipigo Kitakatifu ni Wachezaji kutokuwa na Match Fitness tofauti na Wenzao ( Kaizer Chiefs FC ) ambao kuendelea Kwao kucheza Mechi zao za Ligi Kuu zimewasaidia Kuwaimarisha Kimwili, Kiufundi na Kimchezo.

Simba SC wangeacha Kudekadeka na TFF nayo kukubali Kuidekeza ingecheza Michezo yake Miwili ya Ligi Kuu VPL dhidi ya Watani zao Yanga SC na Coastal Union FC ingekuwa Faida Kwao ya kukijua Kikosi na kukifanyia marekebisho ili isifungwe Kifedheha na Kaizer Chiefs FC kama ilivyotokea leo ( jana ) pale Soccer City ( FNB Stadium )

7. SIMBA SC HAINA KIKOSI CHA MICHUANO YA NUSU FAINALI YA CL BALI INA CHA KUCHEZA VPL, ASFC NA CHA KUISHIA TU ROBO FAINALI YA CL

Ili ujue ( mjue ) kuwa Simba SC ina Wachezaji tu wa Kuifikisha hapo Robo Fainali CL na siyo Nusu Fainali CL angalieni jinsi Wachezaji mahiri wa Simba SC ambao Kutwa huwa tunawaimba walivyokuwa outshined kwa kila Kitu na Wachezaji wa Kaizer Chiefs FC ambao wanaonyesha kuwa wameandaliwa vyema na katika Misingi hasa ya Soka.

Sasa ni wakati wa Simba SC kupitia Mwekezaji wake Mo Dewji kufikiria Kusajili Wachezaji wa Viwango vikubwa vya Kucheza hatua ya Nusu Fainali ya CL na siyo hawa tulionao ambao uwezo wao ni wa kutufikisha tu kila mara katika hatua za Robo Fainali CL.

Kuna Wachezaji wa Kigeni mahiri mno Walisajiliwa kwa Mbwembwe zote na Simba SC kuja Kuongeza Nguvu kama akina Junior Lukosa na Peter Maduhwa ila sijajua wamepotelea wapi, wameitia Hasara Kiasi gani Simba SC yetu na kwanini Kutoweka Kwao wana Simba SC hatukuambiwa pia.

Hata hivyo nihitimishe tu kwa kusema kuwa japokuwa Simba SC leo ( jana ) imefungwa Goli Nne kwa Bila ila ikijipanga vyema na kuwa na Mikakati ya Ushindi ya ndani na nje ya Uwanja Krav Maga nina uhakika Jumamosi ijayo Kaizer Chiefs FC anafungwa hata Goli Sita kwa Sifuri Uwanja wa Machinjio wa Benjamin Mkapa Temeke Mkoani Dar es Salaam.

Kutokana na Hali ya Hewa ya Baridi Kali la Afrika Kusini nawashauri Simba SC hii Mechi yao ya marudiano ichezwe Saa 9 Alasiri ili iwe Changamoto Kwao Kimchezo na Faida Kwetu.

Kikubwa tu tuvumilieni Kuchekwa na Watani zetu wakubwa Yanga SC kwani ndiyo mpira na Utani huo ila nasi sasa tujitahidi kuyafanyia Kazi mapungufu yetu yote ya Kimchezo kusudi Mchezo wa marejeano Simba SC tupindue Matokeo kwa Ushindi kisha nasi tuendelee Kuwaacha Kimafanikio huku wakiendelea tu kupoteza Alama ( points ) kama kwa Namungo FC leo ( jana ) na watukabidhi mapema Ubingwa wetu wa Nne mfululizo wa VPL.

Tumefungwa, lakini tusikate tamaa pia.
Umenena ukweli kabisa.
Point ya 5 haswa. Mchambuzi au mwandishi akiusema ukweli anaonekana ni wa Yanga. Tukumbuke mashambulizi kwa Shafii Dauda aliposema Simba ni underdog. Alipigwa sana mawe. Wachache tunatambua hilo la Shafii lilifanya Simba waamke na kufanya kweli uwanjani.
Sasa kila mchambuzi anaisifia Simba na wanabweteka. Wengine wanalipwa ili wamwage misifa ya uongo. Imewaingia wachezaji wanajiona wako juu sana.

Na point ya 6 ni muhimu sana. TFF wanawapa nafasi ya kupumzika kujiandaa na mechi za kimataifa namwisho wanakosa mechi fitness. Baadaye viporo vitafululiza na ni mbaya maana watakosa recovery time.
 
Ndo maana daily mnaitwa takataka. Mbna hayo hukuyasema wakati simba anashinda? Alafu kufungwa sio jambo geni na ukizingatia bado tuna mechi ya nyumbani. Hata Simba ikitolewa hakutaifanya yanga ibebe ubingwa zaidi mtaendelea na majungu mnyama anasonga.
 
Yani sikujua au kufuatilia sawasawa uwanja gani mechi ya Simba na kcfc itachezwa,nilivyoona ule uwanja tu jinsi ulivyo na kutazama kikosi chetu kinavyoingia uwanjani dhahiri kabisa niliona hofu usoni kwa tshabalala,kapombe na bwalya...tujipange sawasawa mechi ya pili lolote kwenye mpira linaweza kutokea tu,ila Cha msingi ni kujipanga sawasawa michuano ya mwakani Mana huwa inafarijisha sana tukiona timu yetu inazoea zoea kuingia ktk hatua nzuri za mashindano,keep it up...
 
Popoma wenzako wanafungua kampuni mpya we unafungua id mpya kila siku
 
Ndo maana daily mnaitwa takataka. Mbna hayo hukuyasema wakati simba anashinda? Alafu kufungwa sio jambo geni na ukizingatia bado tuna mechi ya nyumbani. Hata Simba ikitolewa hakutaifanya yanga ibebe ubingwa zaidi mtaendelea na majungu mnyama anasonga.
Sijazidi Takataka za aliyekuleta duniani.
 
Kwa mara ya kwanza jana nimeshuhudia Kagere, Boco na Mugalu wakicheza kwa pamoja. Na nnadhani isije kutokea tena mpaka wanastaafu soka.
 
Yaani kikosivni cha kuishia Robo fainali
Ila unategemea kipindue matokeo ya goli 4 kiingie nusu fainali [emoji23][emoji23]

Si kila mtu achambue mpira bana wengine tubaki mashabiki tu ingependeza zaidi
 
Mikia mwisho wao ni Vodacom PL. Huko kwingine hawapawezi kabisa

Umeeleza sababu za msingi mleta mada
 
Kwa mtizamo wangu naona benchi la ufundi la Kaizer lililizidi mbinu kwa mbali sana benchi la ufundi la Simba kama ifuatavyo:-

1. Simba waliidharau sana Kaizer baada ya kuaminishwa na takwimu za waandishi hapa bongo kuwa Kaizer ipo nafasi za chini sana kwenye ligi yao, Kaizer wamefunga magoli machache na kufungwa mengi kwenye CL hivyo basi wanafungika kirahisi na hawafungi sana, wamepita tu kwa bahati kwenye kundi lao licha ya kulingana na Horoya na pia wachezaji wao tegemeo Biliati na kipa tegemeo Itumilenge ni majeruhi. Matokeo yake viongozi wa Simba na benchi la ufundi wakiongozwa na Gomez wakaingiza hizo propaganda kichwani mwao wakaanza kucheza vipasi vyao vifupi wakafunguka jamaa wakastukiza wakawapiga kimoja lakini Simba hawakushtuka wakaendelea kuona tu wanawamudu Kaizer na watasawazisha akili kuja kuwakaa sawa sawa tayari half time ubao unasoma 2 - 0
2. Kaizer ni wazuri lakini hawakutii ubora wa Al Haly. Vipi Al Haly kafunga moja lakini Kaizer kafunga nne? Je tatizo nini? Tatizo lilianzia kwenye benchi la ufundi kujiamini badala ya kucheza kama walivyocheza Misri na Kongo kwao wakafikiri wanacheza na Dodoma Jiji. Laiti kama Simba wangejilinda na kushambulia kwa kushtukiza na kumuacha Mugalu mbele peke yake na wote kurudi nyuma kama walivyofanya Kongo na Misri nina uhakika mechi ingeisha kwa kupoteza kwa goli moja na si zaidi. Hivi benchi la ufundi lilifikiria nini kuanza na viungo Bwalya na Mkude kwenye mechi ya kugongana kiasi kile wakati kwenye benchi una Muzamiru na Nyoni? Siku zote Bwalya na Mkude ni wapiga pasi wazuri sana lakini ikifika kwenye kugongana kama anavyofanya Lwanga hutawaona kabisa. Kwa hiyo inaonyesha kabisa Simba walijiandaa zaidi kwenda mbele kutafuta magoli badala ya kujiandaa kujilinda kwanza.
3. Urefu na maumbo ya wachezaji wa Kaizer ilikuwa tatizo kwa wachezaji wengi wa Simba. Hili ni funzo kwa benchi la ufundi la Simba siku zijazo kuwa wakati wa usajili pamoja na uwezo binafsi wa wachezaji lakini wakati mwingine unatakiwa uwe na wachezaji wawili watatu wababe warefu wenye miili kama Lwanga kwa ajili ya mechi kama ya jana na hapa kwenye ligi yetu wanapokutana na timu kama Prison. Kuna mchezaji beki wa pembeni kushoto mrefu alikuwa Namungo na sasa yupo Ruvu kama sikosei anaitwa Charles Manyama wakimsajili naamini Simba haitajuta. Kwani kwa mijitu kama ya Kaizer au Prison atawafaa sana. Na tatizo lingine ligi yetu inazibana sana timu zetu kuwa na wachezaji 10 tu wa kigeni hivyo basi Simba inatakiwa ifanye kazi kweli kweli kupata wachezaji bora wa ndani na hao wachache 10 wa kigeni ambao ni bora kabisa. Ni wakati sasa kwa benchi la ufundi laSimba lianze kuwafundisha wachezaji mpira kucheza mpira wa nguvu pale inapobidi bna sio kutegemea aina moja tu ya mpira laini laini. Na ili ucheze mpira wa nguvu ni lazima uwe na mijitu hasa iliyokamilika kama wachezaji wa Kaizer.
4. Kwenye mechi ya jana nalipongeza sana benchi la Kaizer kwa sababu waliwapa Simba kitanzi wakajinyonga wenyewe. Kaizer sio kama hawajui kucheza pasi fupi fupi wanajua sana na ndio mchezo wao. Wao waliwaacha Simba wacheze vipasi vyao vifupi (eti biriani) wao Kaizer wakawa wanawasubiri halafu wanapiga mipira mirefu (counter attack). Kiufupi Kaizer waliamua kucheza "direct football". Kwa mtu ambaye hazifahamu Simba na Kaizer angefikiri kuwa Kaizer ndio ipo ugenini na Simba ndio mwenyeji. Lakini ni lini benchi la ufundi litastuka na kumtumia mtu kama Ndemla (anaozea benchi) kwenye mechi kama hizi ambazo Simba inaishia katikati na kushindwa kuvusha mpira mbele? Ukiacha Chuji ambaye ameshastaafu nadhani kwa Tanzania amebaki Ndemla tu peke yake anayeweza kupiga pasi mita zaidi ya 30 kwa usahihi. Kama yupo mwingine naomba kujulishwa.
5. Mabeki wote wa pembeni na wakati walikosa utulivu. Hili siwezi kulisemea sana kwa sababu sijajua lilisababishwa na nini. Kapombe, Husein, Wawa na Onyango walifanya makosa sana walikosa kabisa utulivu ambao walikuwa nao katika mechi zilizopita za CL. Walikumbwa na kitu gani wote kwa pamoja tena katika mechi moja wao ndio wanajua kwani sio kawaida.
6. Viungo wakati na pembeni walikuwa wanachelewesha sana kupeleka mipira mbele kwa haraka. Badala yake walikuwa wanapiga pasi nyingi sana zisizo na malengo wala faida kwa timu. Pale ambapo wanapoamua kupeleka mpira mbele unakuta tayari Kaizer wameshajipanga watu zaidi ya saba kwenye eneo lao la kujilinda wanawasubiri Simba. Na hili ni tatizo sana kwa Simba hata kwenye ligi ya hapa nyumbani. Simba wapo taratibu sana kutoka katikati ya uwanja kwenda eneo la adui na hii huwa inampa adui muda mwingi sana wa kujipanga jinsi ya kuwazuia Simba sema tu kwenye ligi yetu hapa timu zinazoweza kutumuia hayo mapungufu ni chache sana.
7. Benchi la ufundi liwakumbushe mafowadi na viungo washambuliaji wa Simba kuwa sio mara zote lazima wapige pasi mpaka wamkute kipa. Shuti la maana nililoliana ni la Miquisone lililopaa na la Boko ambalo kipa alidaka. Katika akili ya kawaida kabisa Simba wamefika kwenye kumi na nane jamaa wamejaaa wakawa wanajaribu kupiga "one two" mara ya kwanza, pili, tatu, nne jamaa wanaokoa hivi bado tu benchi la ufundi lipo tu wamekaa badala ya kuwakumbusha wajaribu kupiga walau unaweza kukuta kipa yupo "off timing" au hata ikatokea mpira ukamgonga beki ukaenda wavuni.

Mwisho nawapongeza Simba kwa kufika hatua hii. Kwa kweli wanahitaji pongezi sana. Tusiwabeze kwa kilichotokea bali tuwape moyo na ushauri mzuri utakaowasaidia mbeleni. Kwani walianza kupigwa tano tano Misri na Kongo lakini mwaka huu tumeona As Vita kapigwa nje ndani na Al Haly kafa hapa taifa. Nina imani mwakani wakijipanga wakajiimarisha zaidi na kufanya usajili mzuri watafika zaidi ya robo fainali. Mungu ibariki Simba Mungu ibariki Tanzania
 
Kama Mwamamichezo Halisi ( japo sijifichi ni mwana Simba SC ) nianze kwa Kuwapongeza Kaizer Chiefs FC kwa Ushindi wa Goli Nne na niwape pia Pole Simba SC kwa Kufungwa Mchezo huu wa Kwanza leo.

Zifuatazo ni sababu zangu Binafsi za Kiuchambuzi Mimi Krav Maga kwanini Simba SC tumefungwa na Kaizer Chiefs FC ambazo hata hivyo sikulazimishi uziamini japo unatakiwa uziheshimu kama ambavyo nami naheshimu ( nitaheshimu ) zako.

1. KUBWETEKA KWA WACHEZAJI

Huitaji Akili Kubwa ama kuona au kugundua kuwa Mafanikio ya hivi karibuni ya Simba SC yamewapa Kiburi cha Kipuuzi Wachezaji wa Simba SC kiasi cha kuanza Kubweteka wakijiona ni akina FC Barcelona.

2. MIPIRA YA KROSI NI TATIZO SUGU KWA MABEKI WA SIMBA SC

Nilidhani baada ya mwaka Juzi Kufungwa Goli Tano Tano na AS Vita na Al Ahly kwa Mipira ya Krosi Simba SC ingejifunza na Kulifanyia Kazi Ila leo Makosa haya haya ya Kutokujua Kukaba Krosi yamesababisha Beki Shomari Kapombe asababishe Kufungwa Goli 3 huku Beki Mohammed Hussein Zimbwe nae akisababisha Goli 1 ( tena la Nne ) kwa Kumzawadia Pasi ya Upendo Adui na akafumua bonge la Shuti ( Muwa )

3. UZEE KWA MABEKI WA KATI WA SIMBA SC NA KUCHOKA KWAO UPESI

Ifike mahala sasa Simba SC ijifunze ama kutokupenda Kusajili au Kung'ang'ania Wachezaji Wakongwe ( Wazee ) huku wale Vijana na wenye Uwezo kama Beki Kijana ninayemkubali sana Ame Ibrahim na David Kameta Duchu tukiacha Kuwatumia. Leo akina Wawa na Onyango wamefanya Makosa makubwa mno na laiti yangetumiwa vyema na Washambuliaji wa Kaizer Chiefs FC huenda leo tungefungwa hata Magoli 7 au 8 pale Bondeni kwa Madiba.

4. KOCHA WA SIMBA SC KUKARIRI KIKOSI NA KUKOSA PLAN B YA HARAKA

Nikiri tu kuwa Kocha Mkuu wa Simba SC Didier Gomez kweli ni Tactician ila nae sasa ajifunze Kucheza Mechi zake Kimkakati na Kimazingira zaidi kuliko Kujiamini sana na kuingia Kichwa Kichwa tu.

5. VYOMBO VYA HABARI KUPENDA KUIPA SIFA SIMBA SC ZISIZOSTAHILI

Nilitegemea kuona Vyombo vingi vya Habari nchini Tanzania ( hasa vya Michezo ) vingekuwa vinaiambia Ukweli Simba SC kuhusu Klabu ya Kaizer Chiefs Matokeo yake Kutwa tu Magazeti na Watangazaji wa Vipindi vya Michezo Kazi yao ni Kuisifia tu Kinafiki Simba SC kwa kutokujua kuwa Wanawaharibu Wachezaji kupelekea kutokuwa na Ufanisi.

6. UBOVU WA LIGI YA TANZANIA. KUDEKEZWA SANA NA TFF HUKU MWILI KUTOKUWA TAYARI KIMCHEZO

Binafsi niliwashangaa mno Wapenzi na Mashabiki wa Simba SC walipokuwa wakiibeza Klabu ya Kaizer Chiefs kwakuwa iko nafasi ya Kenda ( Tisa ) katika Ligi Kuu yao.

Watu wa Simba SC walisahau kuwa Kaizer Chiefs FC wapo katika Moja ya Ligi Kuu bora barani Afrika ambayo ni Professional League wakati yetu hapa ya VPL ni Semi - Amateur kwa sasa.

Pia sasa imefika wakati TFF kuambiwa ukweli juu ya kupenda Kuidekeza Simba SC na Kuisikiliza kwa kila walitakalo wakati kumbe hapo wanakuwa hawaijengi Klabu bali wanazidi tu Kuibomoa.

Sikuona sababu ya Simba SC kukaa karibia Siku 9 au 11 kutokucheza Mechi yoyote ile ya Kimashindano ( hasa Ligi Kuu ) kwa Kisingizio kuwa wana Mechi za Champions League na hawataki Wachezaji wao ( wetu ) Kuumizwa.

Cha Kushangaza Kaizer Chiefs FC ndani ya Siku hizo hizo ambazo Simba SC ilidekezwa na TFF kwa Kusikilizwa na kutokucheza Mechi yoyote ile ya Ligi Kuu ya VPL wao Kaizer Chiefs wameweza Kucheza Mechi zao Mbili za Ligi Kuu yao Kubwa ya PSL.

Kwangu Mimi Krav Maga naamini mojawapo ya sababu Kubwa ya Simba SC yangu kupokea Kipigo Kitakatifu ni Wachezaji kutokuwa na Match Fitness tofauti na Wenzao ( Kaizer Chiefs FC ) ambao kuendelea Kwao kucheza Mechi zao za Ligi Kuu zimewasaidia Kuwaimarisha Kimwili, Kiufundi na Kimchezo.

Simba SC wangeacha Kudekadeka na TFF nayo kukubali Kuidekeza ingecheza Michezo yake Miwili ya Ligi Kuu VPL dhidi ya Watani zao Yanga SC na Coastal Union FC ingekuwa Faida Kwao ya kukijua Kikosi na kukifanyia marekebisho ili isifungwe Kifedheha na Kaizer Chiefs FC kama ilivyotokea leo ( jana ) pale Soccer City ( FNB Stadium )

7. SIMBA SC HAINA KIKOSI CHA MICHUANO YA NUSU FAINALI YA CL BALI INA CHA KUCHEZA VPL, ASFC NA CHA KUISHIA TU ROBO FAINALI YA CL

Ili ujue ( mjue ) kuwa Simba SC ina Wachezaji tu wa Kuifikisha hapo Robo Fainali CL na siyo Nusu Fainali CL angalieni jinsi Wachezaji mahiri wa Simba SC ambao Kutwa huwa tunawaimba walivyokuwa outshined kwa kila Kitu na Wachezaji wa Kaizer Chiefs FC ambao wanaonyesha kuwa wameandaliwa vyema na katika Misingi hasa ya Soka.

Sasa ni wakati wa Simba SC kupitia Mwekezaji wake Mo Dewji kufikiria Kusajili Wachezaji wa Viwango vikubwa vya Kucheza hatua ya Nusu Fainali ya CL na siyo hawa tulionao ambao uwezo wao ni wa kutufikisha tu kila mara katika hatua za Robo Fainali CL.

Kuna Wachezaji wa Kigeni mahiri mno Walisajiliwa kwa Mbwembwe zote na Simba SC kuja Kuongeza Nguvu kama akina Junior Lukosa na Peter Maduhwa ila sijajua wamepotelea wapi, wameitia Hasara Kiasi gani Simba SC yetu na kwanini Kutoweka Kwao wana Simba SC hatukuambiwa pia.

Hata hivyo nihitimishe tu kwa kusema kuwa japokuwa Simba SC leo ( jana ) imefungwa Goli Nne kwa Bila ila ikijipanga vyema na kuwa na Mikakati ya Ushindi ya ndani na nje ya Uwanja Krav Maga nina uhakika Jumamosi ijayo Kaizer Chiefs FC anafungwa hata Goli Sita kwa Sifuri Uwanja wa Machinjio wa Benjamin Mkapa Temeke Mkoani Dar es Salaam.

Kutokana na Hali ya Hewa ya Baridi Kali la Afrika Kusini nawashauri Simba SC hii Mechi yao ya marudiano ichezwe Saa 9 Alasiri ili iwe Changamoto Kwao Kimchezo na Faida Kwetu.

Kikubwa tu tuvumilieni Kuchekwa na Watani zetu wakubwa Yanga SC kwani ndiyo mpira na Utani huo ila nasi sasa tujitahidi kuyafanyia Kazi mapungufu yetu yote ya Kimchezo kusudi Mchezo wa marejeano Simba SC tupindue Matokeo kwa Ushindi kisha nasi tuendelee Kuwaacha Kimafanikio huku wakiendelea tu kupoteza Alama ( points ) kama kwa Namungo FC leo ( jana ) na watukabidhi mapema Ubingwa wetu wa Nne mfululizo wa VPL.

Tumefungwa, lakini tusikate tamaa pia.
Mkuu salut hata Mimi ni shabiki wa Simba lakini potelea mbali wanilaumu lakini huo ndo ukweli japo unauma
 
Mi Nadhani laana ilianzia kwa Manara kuwaita watu takataka, ile ni laana au kufuru kubwa
 
Simba SC wangeacha Kudekadeka na TFF nayo kukubali Kuidekeza ingecheza Michezo yake Miwili ya Ligi Kuu VPL dhidi ya Watani zao Yanga SC na Coastal Union FC ingekuwa Faida Kwao ya kukijua Kikosi na kukifanyia marekebisho ili isifungwe Kifedheha na Kaizer Chiefs FC kama ilivyotokea leo ( jana ) pale Soccer City ( FNB Stadium )
🎯💯
 
Back
Top Bottom