ephen_
JF-Expert Member
- Oct 28, 2022
- 14,949
- 54,485
"Based on a True Story "
SEHEMU YA 1
"Tina! twende baba yangu amekuja" Haya ni maneno ya rafiki yangu Emmy mchana ya Siku ya jumamosi ya mwisho wa mwezi.
"Mmh! Wewe nenda ukirudi utanikuta" nikamjibu
" Twende nikakutambulishe baba yangu hana shida, lazima ameniletea chakula na huku bwenini vyakula haviruhusiwi, twende Tina tukale"
Mimi ni nani nikatae kwenda kula ukizingatia wazazi wangu wapo mkoani huku hawawezi kuja.
..........................................................
Imepita miaka 12 tokea nilipoanza kuharibu maisha yangu, nimejaribu njia nyingi za kujitoa uhai lakini nimegonga mwamba. Sina jinsi zaidi ya kuchukua ushauri wa rafiki yangu kua nianze upya.
Nina miaka 27 kwasasa ila sio mbaya nikirudi nyumbani kwa baba na mama, nikiwa kwetu nitajihisi amani na utulivu zaidi. Bora nirudi ili mama na baba wanilee upya, safari hii nitasikiliza kila watakachoniambia.
Mama yangu alizoea sana kuniita 'mtukutu' yeye huniambia "Hivi Tina kwa tabia zako hizi wadogo zako unataka wajifunze nini? Kwanini hutaki kubadilika"
Haya maneno yananiudhi sana naona bora shule zifunguliwe niondoke nyumbani.
Nipo kidato cha pili shule ya bweni lakini kila ijumaa ya mwisho wa mwezi wenzangu wakienda usiku kujisomea Mimi natoroka narudi nyumbani mpaka jumapili ndio narudi shule.
Natoroka Siku hiyo kwasababu ni ngumu walimu kugundua sababu jumamosi ya kila mwisho wa mwezi ni visiting day.
MAMA: Leo tena umerudi nyumbani! Sasa kuna faida gani ya baba yako kulipa mamilioni wewe usome bweni, walimu wako wakigundua utafukuzwa shule. Baba yako ndiye anakudekeza wewe!
TINA: Hakuna madhara yoyote, kesho wazazi wanakuja kuwaona watoto wao hakuna kusoma, sasa Mimi nikija nyumbani kuna shida gani?
MAMA: Mimi hayo hayanihusu, muhimu ukifukuzwa shule ni kosa LA baba yako, yeye ndiye amekuza huo mchezo wako.
Baba yangu ni dereva wa malori ya mikoani, hana shida kuhusu Mimi kurudi nyumbani, huwa ananiambia anachotaka yeye ni kuniona nafaulu vizuri.
Nikijiangalia naona kabisa sina akili za darasani, nimeitwa sana mbele ya umati wa wanafunzi wenzangu kama 'best loser' kwenye mitihani ya mwisho wa mwezi, ni kawaida yangu kutofikisha wastani wa 50.
Nimemaliza mitihani ya kidato cha pili nipo nyumbani.
TINA: Hivi mama sina ndugu Dar es salaam niende kukaa kwake hii likizo?
MAMA: Kukaa kwenu hutaki? Nani ataweza kuishi na wewe na utukutu wako huo?
Mama yangu ananiona mtukutu kisa sipendi kutumwa, napenda kukaa kwenye TV tu, nikiwa nyumbani wadogo zangu wanakasirika nawatuma mpaka kazi zangu.
MAMA: Dar es Salaam utakaa mpaka utachoka mwenyewe, kidato cha tatu unaenda bweni huko, sababu ukiwa hapa karibu kila Siku unataka utoroke shule.
..........................................................
MATRON: Umesema unaitwa Tina! Basi subiri wenzako watoke darasani nikupe Emmy awe rafiki yako ana akili atakufaa na wewe ufaulu vizuri.
Sio ishara nzuri kidato cha pili kupata division 3.
Huyu ni matron kwenye shule yangu mpya niliyoamishiwa Dar as salaam.
Safari yangu ya urafiki na Emmy ilianza kwa kuunganishwa na Matron.
.........................
Basi Mimi na Emmy tukaongozana mpaka kwenye bustani waliopo wazazi.
Nikatambulishwa na Emmy kwa baba yake, nashkuru Mungu baba wa watu hakuonesha kutofurahishwa na uwepo wangu pale.
Emmy akafungua mifuko iliyoletwa, jicho langu likatua kwenye chakula ninachokipenda 'Chips kuku' japo kulikua na mazagazaga mengine
Nilikula nikafurahi.
Kitu kilichonishangaza ni baba Emmy wakati anaondoka akanipa elfu 30.
Nikapokea huku siamini macho yangu
"Jamani huyu baba ana roho nzuri sana" nikajisemea
"Sinilikuambia Tina! Baba yangu hana neno"
Elfu 30 nilipewa mbele ya kila Mtu aliyekuwepo pale, Tina nae alipewa kibunda ambacho baadae nilijua ilikua ni laki 1.
Baada ya Mimi kupewa ile hela, mapenzi yangu kwa Emmy yaliongezeka urafiki ulinoga sana ukizingatia baba alitupa nasaha wakati anaondoka "Watoto wangu msome kwa bidii" hivyo tulikua tunasoma kwa kushirikiana na Emmy wangu.
Nikapata utamaduni mpya kila mwisho wa mwezi baba Emmy akija na Mimi nipo! Chips kuku zikaanza kuletwa mbili, shower gel 2, dawa za mswaki 2 kila kitu kinaletwa kwa pair.
Yote Tisa, kumi nililetewa mpaka dictionary bila kusahau kila mwisho wa mwezi elfu 30 yangu ipo palepale.
Ila nina siri ambayo naona nimfiche Emmy JINSI BABA YAKE ANAVYONIANGALIA..!
Sehemu ya 2: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya 3: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya 4: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya 5: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya 6: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya 7: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya 8: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya mwisho: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
SEHEMU YA 1
"Tina! twende baba yangu amekuja" Haya ni maneno ya rafiki yangu Emmy mchana ya Siku ya jumamosi ya mwisho wa mwezi.
"Mmh! Wewe nenda ukirudi utanikuta" nikamjibu
" Twende nikakutambulishe baba yangu hana shida, lazima ameniletea chakula na huku bwenini vyakula haviruhusiwi, twende Tina tukale"
Mimi ni nani nikatae kwenda kula ukizingatia wazazi wangu wapo mkoani huku hawawezi kuja.
..........................................................
Imepita miaka 12 tokea nilipoanza kuharibu maisha yangu, nimejaribu njia nyingi za kujitoa uhai lakini nimegonga mwamba. Sina jinsi zaidi ya kuchukua ushauri wa rafiki yangu kua nianze upya.
Nina miaka 27 kwasasa ila sio mbaya nikirudi nyumbani kwa baba na mama, nikiwa kwetu nitajihisi amani na utulivu zaidi. Bora nirudi ili mama na baba wanilee upya, safari hii nitasikiliza kila watakachoniambia.
Mama yangu alizoea sana kuniita 'mtukutu' yeye huniambia "Hivi Tina kwa tabia zako hizi wadogo zako unataka wajifunze nini? Kwanini hutaki kubadilika"
Haya maneno yananiudhi sana naona bora shule zifunguliwe niondoke nyumbani.
Nipo kidato cha pili shule ya bweni lakini kila ijumaa ya mwisho wa mwezi wenzangu wakienda usiku kujisomea Mimi natoroka narudi nyumbani mpaka jumapili ndio narudi shule.
Natoroka Siku hiyo kwasababu ni ngumu walimu kugundua sababu jumamosi ya kila mwisho wa mwezi ni visiting day.
MAMA: Leo tena umerudi nyumbani! Sasa kuna faida gani ya baba yako kulipa mamilioni wewe usome bweni, walimu wako wakigundua utafukuzwa shule. Baba yako ndiye anakudekeza wewe!
TINA: Hakuna madhara yoyote, kesho wazazi wanakuja kuwaona watoto wao hakuna kusoma, sasa Mimi nikija nyumbani kuna shida gani?
MAMA: Mimi hayo hayanihusu, muhimu ukifukuzwa shule ni kosa LA baba yako, yeye ndiye amekuza huo mchezo wako.
Baba yangu ni dereva wa malori ya mikoani, hana shida kuhusu Mimi kurudi nyumbani, huwa ananiambia anachotaka yeye ni kuniona nafaulu vizuri.
Nikijiangalia naona kabisa sina akili za darasani, nimeitwa sana mbele ya umati wa wanafunzi wenzangu kama 'best loser' kwenye mitihani ya mwisho wa mwezi, ni kawaida yangu kutofikisha wastani wa 50.
Nimemaliza mitihani ya kidato cha pili nipo nyumbani.
TINA: Hivi mama sina ndugu Dar es salaam niende kukaa kwake hii likizo?
MAMA: Kukaa kwenu hutaki? Nani ataweza kuishi na wewe na utukutu wako huo?
Mama yangu ananiona mtukutu kisa sipendi kutumwa, napenda kukaa kwenye TV tu, nikiwa nyumbani wadogo zangu wanakasirika nawatuma mpaka kazi zangu.
MAMA: Dar es Salaam utakaa mpaka utachoka mwenyewe, kidato cha tatu unaenda bweni huko, sababu ukiwa hapa karibu kila Siku unataka utoroke shule.
..........................................................
MATRON: Umesema unaitwa Tina! Basi subiri wenzako watoke darasani nikupe Emmy awe rafiki yako ana akili atakufaa na wewe ufaulu vizuri.
Sio ishara nzuri kidato cha pili kupata division 3.
Huyu ni matron kwenye shule yangu mpya niliyoamishiwa Dar as salaam.
Safari yangu ya urafiki na Emmy ilianza kwa kuunganishwa na Matron.
.........................
Basi Mimi na Emmy tukaongozana mpaka kwenye bustani waliopo wazazi.
Nikatambulishwa na Emmy kwa baba yake, nashkuru Mungu baba wa watu hakuonesha kutofurahishwa na uwepo wangu pale.
Emmy akafungua mifuko iliyoletwa, jicho langu likatua kwenye chakula ninachokipenda 'Chips kuku' japo kulikua na mazagazaga mengine
Nilikula nikafurahi.
Kitu kilichonishangaza ni baba Emmy wakati anaondoka akanipa elfu 30.
Nikapokea huku siamini macho yangu
"Jamani huyu baba ana roho nzuri sana" nikajisemea
"Sinilikuambia Tina! Baba yangu hana neno"
Elfu 30 nilipewa mbele ya kila Mtu aliyekuwepo pale, Tina nae alipewa kibunda ambacho baadae nilijua ilikua ni laki 1.
Baada ya Mimi kupewa ile hela, mapenzi yangu kwa Emmy yaliongezeka urafiki ulinoga sana ukizingatia baba alitupa nasaha wakati anaondoka "Watoto wangu msome kwa bidii" hivyo tulikua tunasoma kwa kushirikiana na Emmy wangu.
Nikapata utamaduni mpya kila mwisho wa mwezi baba Emmy akija na Mimi nipo! Chips kuku zikaanza kuletwa mbili, shower gel 2, dawa za mswaki 2 kila kitu kinaletwa kwa pair.
Yote Tisa, kumi nililetewa mpaka dictionary bila kusahau kila mwisho wa mwezi elfu 30 yangu ipo palepale.
Ila nina siri ambayo naona nimfiche Emmy JINSI BABA YAKE ANAVYONIANGALIA..!
Sehemu ya 2: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya 3: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya 4: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya 5: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya 6: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya 7: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya 8: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya
Sehemu ya mwisho: Bora nirudi kwa wazazi wangu wanifunze upya