Bosi wa mashuhushu wanaomlinda Obama alivyojiuzulu ni darasa kwa Idara yetu ya Usalama wa Taifa

Bosi wa mashuhushu wanaomlinda Obama alivyojiuzulu ni darasa kwa Idara yetu ya Usalama wa Taifa

Mkuu kiufupi nchi zote za Africa hakuna democracy, hivyo zinaendeshwa kibabe kupita maelezo.

Lakini miaka 50 ijayo tutaanza democracy. Na hii ni baada labda ya advancement ya technology inaweza iforce serikali kupractice democracy.

Lakini kwa sasa tuendelee tu kufa na tai shingoni.
 
Kwahyo unayoyaangalia YouTube ndio yanakuleta mbio kuja kuwambia nahuku waige,unadhani tiss wanaendelea kwa kufata movie,marekani yenyewe unayotolea mfano nao wanamatatzo ya kiintelligencia pamoja na kwamba wanahojiwa kwenye baraza la senet kama ulivyodai!.
 
Ameshaorodhesha Marekani hapo juu,wao wanamwita kwenye baraza la Seneti.
Kwahyo alichokiangalia YouTube ndio kimemleta mbio kuwashauri tiss waige!!,kwahyo marekani haina matatzo ya kiintelligencia pamoja na kwamba amejiuzulu huyo au pamoja na kwamba wanahojiwa seneti?
 
Mkuu kiufupi nchi zote za Africa hakuna democracy, hivyo zinaendeshwa kibabe kupita maelezo.

Lakini miaka 50 ijayo tutaanza democracy. Na hii ni baada labda ya advancement ya technology inaweza iforce serikali kupractice democracy.

Lakini kwa sasa tuendelee tu kufa na tai shingoni.
Mkuu umesema vema sana. Kwanza huo mfumo wa ajira za 'kurithishana' ndiyo uliokuja kuiharibu taasisi hii. Mfumo huu huu vile vile umeliharibu jeshi letu la polisi. Ndiyo maana utaona uadilifu hakuna tena kwani kijana anapewa kazi kwa manufaa ya mkubwa wake.
Pili, hakuna uwazi wa kuajiri watu wawe na vigezo gani ambavyo vitamfanya afit katika kazi husika, hivyo kutoa mwanya kwa mjomba kumleta mpwawe katika kazi na matokeo yake kutengeneza cheni ya kumtumikia 'bwana Fisadi' kuanzia baba.....mjomba mpaka mpwawe.
Tatu, weledi nao imekuwa shida. Hatupingi mtu kapata kazi kupitia kwa shangazi, mjomba nk maana waTz hawakawii kusema 'tunawivu na alichopata mwingine' sasa inshu huyo aliyopata kazi hiyo ana weledi mzuri wa hiyo kazi?

Kumbe mnataka kazi tiss si mngesema tu! kuliko kutoka povu.
 
Umeongelea "mifumo" halafu ukaongelea "mbinu".

Inaonesha wazi huelewi hiyo "mifumo" ni ipi na wala hilo neno lina maana ipi.

Kuna sita sita? Nne mbili? tatu tatu? Au?

Wacheni kuhororoja na kubwabwaja bila mpango.

Ukiona mtu anaelezea jambo halafu akataja "mfumo" au even worse akataja "mifumo" ujuwe huyo ni kilaza asiyeelewa anachokiandika bali anaandika na yeye awe yumo yumo tu.

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
tatizo lako kila kitu unajua wewe, anzisha blog yako ya kuelezea ufahamu wako juu ya kila jambo....
 
mtoa mada una mawazo mazuri ni vyema ukawaandikia barua ya ushauli ukiwa mtu huru kuliko kuweka jamvini
 
wacha uwoga hapa raisi ndio mkuu jemedari.wa majeshi
 
Evarist Chahali mwenyewe ni TISS maarufu kabisa, sa hivi kakimbili uscoch, ni mtoro anayewindwa sana na ex TISS wengi akiwamo membe
Vijana hawajui hilo kuwa jamaa nae ni ex intelligent officer
 
Evarist Chahali mwenyewe ni TISS maarufu kabisa, sa hivi kakimbili uscoch, ni mtoro anayewindwa sana na ex TISS wengi akiwamo membe
Ndio kusema wanashindwa kumpata?!
 
Idara ya usalama wa taifa wa tz ndio imara na shupavu na namba moja kwa Africa ikifuatiwa na SA.

Kuhusu kuhoji utendaj kazi wa idara hii me nadhani ni uendawazimu, Tiss ipo imara na Salama nchini ya mkurugenz wake Mh Othman na vijana wake.

Wakati mwingine tusijifanye much know kwa mambo msioyajua.
kauli za tangu mwaka 47.
 
bahati nzuri wahusika wakuu Nifah, UncleBen na Mussolin5 wamo humu humu hivyo ngoja na wao sasa waje waitetee hii hoja yako japo nakubaliana na wewe kwa 100% zote kwani hata hao majamaa tajwa hapo hunipiga mno mkwara na kuna siku mmoja wapo nilibishana nae humu akanitolea bastola nikawa kila niki type tu naiona. nilinywea mwenyewe mkuu!
kijana wa kinyarwanda upo?.
 
Mkuu kwa namna fulani nashindwa kukubaliana na baadhi ya hoja zako,
kwa mfano kwamba watendaji wakuu wa TISS waweze kuitwa bungeni..

hivi bunge unalolizungumzia ni hili hili au kuna lingine.

Kwa uwezo wa bunge letu lilivyo siamini kama lina uwezo huo, bunge letu linaendeshwa mno kisiasa, hawazingatii weledi wala nini, we angalia tu ile ishu ya escrow ilivyomalizwa kisiasa na sasa wale watuhumiwa karibu wote ndio wako bungeni na baadhi ni wenyeviti wa kamati za bunge.

hawa wabunge wa "naunga mkono hoja" sidhani kama wana ubavu wa kuwaita TISS na kuwahoji ki-weledi, bila kuingiza siasa za vyama..

hoja yao ina mashiko kabisa lakini si kwa bunge letu labda kwa miaka ijayo...
hivi bunge letu mnalionaje?
Kweli mkuu kwa bunge hili la waropokaji na wazushi hata mimi nakataa....sasa hivi bunge halina tofuati na vijiwe vya wahuni wa pale magomeni kwa jinsi wanavyozozana.....
 
Tiss wanapokea ushahidi moja moja toka kwa raia?.
Uliwai kuwapelekea ushahidi wakakwambia hawapokei? Kwanza unawajua? Unajua ofisi zao? Hebu kamilisha ushahidi wako halafu watakutafta uwape ili waufanyie kazi. Tunaheshimu mawazo yako hapa JF.
 
Si kila kinachofanyika Marekani kinafaa kuigwa Tanzania. Twende na mazingira yetu
 
Back
Top Bottom