Brother James
JF-Expert Member
- Feb 21, 2012
- 233
- 172
Kwa heshima ya Mwl. Nyerere, Benki Kuu ya Tanzania(BOT) wametoa fursa kwa watanzania wanne (4) kwa ngazi ya undergraduate na watanzania wawili (2) kwa ngazi ya postgraduate/Masters kuwasomesha bure (scholarships) endapo watakidhi vigezo walivyoweka. Scholarships hizi wamezipa jina la Mwl. Julius K. Nyerere Memorial Scholarship Fund.
Deadline ya kuomba kwa undergraduate ni tarehe 12/09/2014 na deadline kwa postgraduate ni 29/10/2014
KWA MAELEZO YA KINA JUU YA SCHOLARSHIPS HIZI SOMA HAPO CHINI. VIAMBATISHO(ATTACHMENTS) ZA UJUMBE HUU NI FORMS ZA KUOMBEA SCHOLARSHIPS HIZI PAMOJA NA RECOMMENDATION FORM kwa ajili ya waombaji wa Postgraduate. NIWATAKIE MAFANIKIO MEMA WOTE WENYE SIFA:
UTANGULIZI:
Scholarships hizi kwa mara ya kwanza zimetolewa mwaka wa masomo 2013/2014 na walengwa walikuwa ni wasichana waliofanya vizuri (A-Level) katika masomo ya sayansi na Hisabati kupewa fursa ya kusomeshwa bure (kwenye fani za sayansi na hisabati) katika vyuo vikuu vya kitanzania na kulipwa fedha za chakula ma malazi pamoja na laptop moja kwa kila scholar. Pia walifikiria kutoa ufadhili mdogo kwa wanafunzi watakao soma fani za Economics,IT, Accounting & Finance. Pia wakafikiria kutoa ufadhili kwa level ya Masters katika fani tajwa hapo juu japo kwa uchache.
LENGO KUU LA UFADHILI/SCHOLARSHIP
BOT wamenuia kuwainua kielimu wanawake hususani katika masomo ya sayansi na Hisabati husasani katika ngazi ya Shahada/degree na Shahada ya Uzamili/Master na kwa uchache kutoa motisha kwa wanaume wachache waliofanya vizuri zaidi katika masomo/fani tajwa. Scholarships hizi hufadhili malipo yote yahusuyo gharama za kielimu kwa mtu aliyepewa ufadhili huu ikiwa ni pamoja na gharama za udahili wa chuoni, chakula, malazi, practicals, ada, laptop moja, na gharama nyinginezo zoote.
MGAWANYO WA UFADHILI HUU
1.UNDERGRADUATE:
(i) Scholarship mbili (2) ni kwa wadada waliofaulu vizuri (A-level) katika masomo ya sayansi na Hisabati na ambao
wamejiandaa kusomea masomo ya sayansi na Hisabati ngazi ya degree
(ii) Scholarship mbili (2) ni kwa ajili ya wavulana na wasichana waliofanya vizuri katika masomo yao ya A-level na
wana sifa za kujiunga katika vyuo vikuu kusoma fani za Economics, Accounting, Finance na IT.
SIFA ZA WAOMBAJI WA (i)
a. Wawe watanzania waliohitimu A-level mwaka 2014 na wenye ufaulu wa daraja la kwanza na wapate alama "A'
katika somo moja wapo kati ya Hisabati na Sayansi (Chemistry, Physics, Biology)
b. Wawe na ufaulu mzuri katika cheti cha O-level na wawe wameomba/dahiliwa katika vyuo vikuu vya Tanzania kwa
mwaka wa masomo 2014/15 hususani ktk fani za Hisabati na sayansi tu.
SIFA ZA WAOMBAJI WA (ii)
a. Wawe watanzania waliohitimu A-level mwaka 2014 na wenye ufaulu wa daraja la kwanza na wapate alama "A'
katika somo moja wapo kati ya Hisabati, Commerce, Economics, Acounting na Sayansi (Chemistry, Physics, Biology)
b. Wawe na ufaulu mzuri katika cheti cha O-level na wawe wameomba/dahiliwa katika vyuo vikuu vya Tanzania kwa
mwaka wa masomo 2014/15 hususani ktk fani za IT, Economics, Accounting & Finance
2. POSTGRADUATE/MASTERS
i. Ngazi hii, waombaji wote (wanaume na wanawake) wanasifa za kuomba ufadhili bora wawe watanzania tu
ii. Waombaji wote wawe na first class na upper second class wenye ufaulu wa chini kabisa 4.0 GPA katika degree zao wa kwanza na wawe wamehitimu kati ya mwaka 2013 na 2014 tu.
iii. Waombaji wawe wamedahiliwa kusoma katika vyuo vikuu vya nchini Tanzania na wawe wamedahiliwa kusomea fani zifuatazo; IT, Mathematucs, Science, Economics & Acconting.
JINSI YA KUOMBA UFADHILI
i. Form za kuombea zinapatikana kwenye website hii: Bank of Tanzania (BOT): Home Page : Benki Kuu ya Tanzania (nime iambatanisha kwenye ujumbe huu)
ii. Ukisha ijaza itume kwenye anuani ifuatayo:
THE CHAIRPERSON
SCHOLARSHIP AWARD COMMITTEE
MWL. JULIUS K. NYERERE MEMORIAL SCHOLARSHIP FUND
BANK OF TANZANIA
2 MIRAMBO STREET
P.O. BOX 11884
DAR ES SALAAM
*****MWISHO
Deadline ya kuomba kwa undergraduate ni tarehe 12/09/2014 na deadline kwa postgraduate ni 29/10/2014
KWA MAELEZO YA KINA JUU YA SCHOLARSHIPS HIZI SOMA HAPO CHINI. VIAMBATISHO(ATTACHMENTS) ZA UJUMBE HUU NI FORMS ZA KUOMBEA SCHOLARSHIPS HIZI PAMOJA NA RECOMMENDATION FORM kwa ajili ya waombaji wa Postgraduate. NIWATAKIE MAFANIKIO MEMA WOTE WENYE SIFA:
UTANGULIZI:
Scholarships hizi kwa mara ya kwanza zimetolewa mwaka wa masomo 2013/2014 na walengwa walikuwa ni wasichana waliofanya vizuri (A-Level) katika masomo ya sayansi na Hisabati kupewa fursa ya kusomeshwa bure (kwenye fani za sayansi na hisabati) katika vyuo vikuu vya kitanzania na kulipwa fedha za chakula ma malazi pamoja na laptop moja kwa kila scholar. Pia walifikiria kutoa ufadhili mdogo kwa wanafunzi watakao soma fani za Economics,IT, Accounting & Finance. Pia wakafikiria kutoa ufadhili kwa level ya Masters katika fani tajwa hapo juu japo kwa uchache.
LENGO KUU LA UFADHILI/SCHOLARSHIP
BOT wamenuia kuwainua kielimu wanawake hususani katika masomo ya sayansi na Hisabati husasani katika ngazi ya Shahada/degree na Shahada ya Uzamili/Master na kwa uchache kutoa motisha kwa wanaume wachache waliofanya vizuri zaidi katika masomo/fani tajwa. Scholarships hizi hufadhili malipo yote yahusuyo gharama za kielimu kwa mtu aliyepewa ufadhili huu ikiwa ni pamoja na gharama za udahili wa chuoni, chakula, malazi, practicals, ada, laptop moja, na gharama nyinginezo zoote.
MGAWANYO WA UFADHILI HUU
1.UNDERGRADUATE:
(i) Scholarship mbili (2) ni kwa wadada waliofaulu vizuri (A-level) katika masomo ya sayansi na Hisabati na ambao
wamejiandaa kusomea masomo ya sayansi na Hisabati ngazi ya degree
(ii) Scholarship mbili (2) ni kwa ajili ya wavulana na wasichana waliofanya vizuri katika masomo yao ya A-level na
wana sifa za kujiunga katika vyuo vikuu kusoma fani za Economics, Accounting, Finance na IT.
SIFA ZA WAOMBAJI WA (i)
a. Wawe watanzania waliohitimu A-level mwaka 2014 na wenye ufaulu wa daraja la kwanza na wapate alama "A'
katika somo moja wapo kati ya Hisabati na Sayansi (Chemistry, Physics, Biology)
b. Wawe na ufaulu mzuri katika cheti cha O-level na wawe wameomba/dahiliwa katika vyuo vikuu vya Tanzania kwa
mwaka wa masomo 2014/15 hususani ktk fani za Hisabati na sayansi tu.
SIFA ZA WAOMBAJI WA (ii)
a. Wawe watanzania waliohitimu A-level mwaka 2014 na wenye ufaulu wa daraja la kwanza na wapate alama "A'
katika somo moja wapo kati ya Hisabati, Commerce, Economics, Acounting na Sayansi (Chemistry, Physics, Biology)
b. Wawe na ufaulu mzuri katika cheti cha O-level na wawe wameomba/dahiliwa katika vyuo vikuu vya Tanzania kwa
mwaka wa masomo 2014/15 hususani ktk fani za IT, Economics, Accounting & Finance
2. POSTGRADUATE/MASTERS
i. Ngazi hii, waombaji wote (wanaume na wanawake) wanasifa za kuomba ufadhili bora wawe watanzania tu
ii. Waombaji wote wawe na first class na upper second class wenye ufaulu wa chini kabisa 4.0 GPA katika degree zao wa kwanza na wawe wamehitimu kati ya mwaka 2013 na 2014 tu.
iii. Waombaji wawe wamedahiliwa kusoma katika vyuo vikuu vya nchini Tanzania na wawe wamedahiliwa kusomea fani zifuatazo; IT, Mathematucs, Science, Economics & Acconting.
JINSI YA KUOMBA UFADHILI
i. Form za kuombea zinapatikana kwenye website hii: Bank of Tanzania (BOT): Home Page : Benki Kuu ya Tanzania (nime iambatanisha kwenye ujumbe huu)
ii. Ukisha ijaza itume kwenye anuani ifuatayo:
THE CHAIRPERSON
SCHOLARSHIP AWARD COMMITTEE
MWL. JULIUS K. NYERERE MEMORIAL SCHOLARSHIP FUND
BANK OF TANZANIA
2 MIRAMBO STREET
P.O. BOX 11884
DAR ES SALAAM
*****MWISHO