Bounou wa Sevilla, golikipa anayeijua vizuri saikolojia ya kudaka penati

Bounou wa Sevilla, golikipa anayeijua vizuri saikolojia ya kudaka penati

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Wengi wanaamini upigaji penati ni bahati zaidi ya ufundi ila mimi napingana na hiyo dhana. Nikiwa mtu niliyecheza mchezo huu wa football kwa kiwango kikubwa sana katika nafasi tofauti uwanjani na kuna wakati nikawa hadi kocha, nina uwezo wa kulizungumza hili kwa uhakika na kujiamini maana najua ninachozungumza.

Kuna vitu fulani vidogo tu ambavyo mpigaji penati ukivijua, kukosa penati itakuwa ni nadra sana. Vivyo hivyo ukiwa golikipa kuna vitu ukivifahamu chance ya kuzuia penati inaongezeka maradufu na vyote hivi vinahusiana na saikolojia.

Nimemshuhudia golikipa Yassine Bounou, maarufu kama Bono, mchezaji wa Sevilla na timu ya taifa ya Morocco kama mmoja wa magolikipa waliomasta saikolojia ya kudaka penati.

Bono niliona umahiri wake katika Kombe la Dunia la 2022 kule Qatar. Nilimuangalia kwa makini sana vitu alivyokuwa anavifanya wakati wa penati na ni vitu ambavyo siku zote naamini ndiyo mbinu za kudaka penati.

images - 2023-06-01T103538.212.jpeg
Katika picha hii hapa juu, Bono alidaka penati hii huku anacheka baada ya kumuhadaa mpigaji naye akaingia mazima.

Jana katika mechi ya fainali ya kombe la EUROPA kati ya AS Roma na Sevilla, nilimuona tena akifanya vitu hivyo hivyo na akaokoa penati 2 zilizoipa ubingwa Sevilla.

Kwenye upigaji au kudaka penati, trick ipo kwenye kupenya kwenye kichwa cha mchezaji wa upande wa pili na kucheza na akili yake ili kumuhadaa akili yake. Ni kitendo cha sekunde chache sana ila ukikipatia matokeo yake utayaona. Ukifanya hivi, utajua usimame vipi na ucheze vipi na mikono na mwili wako kiujumla.

Kama unataka kujua mbinu za udakaji penati, msome vizuri golikipa wa Sevilla na timu ya taifa ya Morocco, Bounou.
 
sasa umeongea kama kocha, mchambuzi, mshabiki wa bono? ongeza nyama sana sana kwenye upande wa hiyoo saikolojia.
 
Huwa sielewi mimi ndio mjinga au sielewi akili za watu wa mpira. Jamaa kadai ni fani yake ila anavyoeleza utadhani kasimuliwa leoleo yani kama kaokoteleza maelezo kidogo.
Huwezi ona mtu anajiita fundi mzoefu wa magari simply anakwambia "fanya service". Atakwambia mwaga oil, tumia oil husika, usifanye hiki, kama kuna tatizo fulani fanya hivi.

Kucheka kwa Bono kulimfanyaje adake penati?

"Kwenye upigaji au kudaka penati, trick ipo kwenye kupenya kwenye kichwa cha mchezaji wa upande wa pili na kucheza na akili yake ili kumuhadaa akili yake..."
ndio nini hapa? Mpigaji au kipa anapenyaje kwenye kichwa cha mwenzake, tricks zipi anatumia, sign zipi anaona.

Wewe ni kocha ila umeandika kama nabii, hana haja ya kujua sana atawasingizia waumini wawe na imani basi hata kama hamna logic
 
sasa umeongea kama kocha, mchambuzi, mshabiki wa bono? ongeza nyama sana sana kwenye upande wa hiyoo saikolojia.
Maneno mengi alafu ujaeleza namna bono anavyofanya!!!!

Angalieni mechi ya Kombe la Dunia kati ya Morocco na Spain, angalia kwa makini Bono tuvitu alikuwa anafanya kabla ya kila penati na jiulize vile vitu alivyokuwa anafanya vilikuwa na athari gani kwa mpigaji.
 
Huwa sielewi mimi ndio mjinga au sielewi akili za watu wa mpira. Jamaa kadai ni fani yake ila anavyoeleza utadhani kasimuliwa leoleo yani kama kaokoteleza maelezo kidogo.
Huwezi ona mtu anajiita fundi mzoefu wa magari simply anakwambia "fanya service". Atakwambia mwaga oil, tumia oil husika, usifanye hiki, kama kuna tatizo fulani fanya hivi.

Kucheka kwa Bono kulimfanyaje adake penati?

"Kwenye upigaji au kudaka penati, trick ipo kwenye kupenya kwenye kichwa cha mchezaji wa upande wa pili na kucheza na akili yake ili kumuhadaa akili yake..."
ndio nini hapa? Mpigaji au kipa anapenyaje kwenye kichwa cha mwenzake, tricks zipi anatumia, sign zipi anaona.

Wewe ni kocha ila umeandika kama nabii, hana haja ya kujua sana atawasingizia waumini wawe na imani basi hata kama hamna logic
Hapa hatupo uwanjani kusema naweza kukuonyesha hizo mbinu kwa urahisi. Ndiyo maana nimesisitiza kaangalie udakaji wake wa penati uone nini utaweza kupata. Usipende kuwa mtu wa kutafuniwa na kumezewa kila kitu.
 
Angalieni mechi ya Kombe la Dunia kati ya Morocco na Spain, angalia kwa makini Bono tuvitu alikuwa anafanya kabla ya kila penati na jiulize vile vitu alivyokuwa anafanya vilikuwa na athari gani kwa mpigaji.

Ungepaswa useme hivyo vitu ni vitu gani, wengine mabando ya kuangangalia hizo video hawana!
Huu uzi utatukanwa bure...!!!
 
Hapa hatupo uwanjani kusema naweza kukuonyesha hizo mbinu kwa urahisi. Ndiyo maana nimesisitiza kaangalie udakaji wake wa penati uone nini utaweza kupata. Usipende kuwa mtu wa kutafuniwa na kumezewa kila kitu.
Hakukuwa na haja ya kujiita kocha na hujui kueleza unachotakiwa, ndivyo unafundisha wachezaji hivi? Si bora ungesema wewe ni mtazamaji wa mpira kama wengine na ukaelekeza watu wakatazame wenyewe kama wewe.

Ni sawa na daktari aje humu kufafanua namna ya kuepuka magonjwa ya moyo kisha atwambie nendeni mkasome msitafuniwe.
 
Huwa sielewi mimi ndio mjinga au sielewi akili za watu wa mpira. Jamaa kadai ni fani yake ila anavyoeleza utadhani kasimuliwa leoleo yani kama kaokoteleza maelezo kidogo.
Huwezi ona mtu anajiita fundi mzoefu wa magari simply anakwambia "fanya service". Atakwambia mwaga oil, tumia oil husika, usifanye hiki, kama kuna tatizo fulani fanya hivi.

Kucheka kwa Bono kulimfanyaje adake penati?

"Kwenye upigaji au kudaka penati, trick ipo kwenye kupenya kwenye kichwa cha mchezaji wa upande wa pili na kucheza na akili yake ili kumuhadaa akili yake..."
ndio nini hapa? Mpigaji au kipa anapenyaje kwenye kichwa cha mwenzake, tricks zipi anatumia, sign zipi anaona.

Wewe ni kocha ila umeandika kama nabii, hana haja ya kujua sana atawasingizia waumini wawe na imani basi hata kama hamna logic
Naungana na wewe. Mleta mada kaanza vizuri Sana kashindwa kumalizia. Mfano penati ya Kwanza iliyozuiwa na Bono ingetosha kueleza ujanja wake lakini hajasema lolote. Kipa kamhadaa mpigaji kwamba anakwenda kushoto kwake moja Kwa moja kumbe hakawenda mzima akawa na uwezo wa kurudi Kati ambapo mpigaji aliamini tayari kipa amehama. Kama penati husika Ingepigwa kulia Kwa kipa hiyo anayosema kipa aingie kwenye akili ya mpigaji isingefanya kazi.
 
Ungepaswa useme hivyo vitu ni vitu gani, wengine mabando ya kuangangalia hizo video hawana!
Huu uzi utatukanwa bure...!!!
Mtu akija kunitukana kisa hicho atakuwa amepungukiwa na akili. NITADIRII NAYE!
 
Hakukuwa na haja ya kujiita kocha na hujui kueleza unachotakiwa, ndivyo unafundisha wachezaji hivi? Si bora ungesema wewe ni mtazamaji wa mpira kama wengine na ukaelekeza watu wakatazame wenyewe kama wewe.

Ni sawa na daktari aje humu kufafanua namna ya kuepuka magonjwa ya moyo kisha atwambie nendeni mkasome msitafuniwe.
Mnapenda kukomalia mambo yasiyo na msingi mnasahau mada husika. Sasa kujitambukisha kama kocha au mtazamaji kungebadili nini kuhusu nilichosema zaidi tu ya mtazamo wako kuhusu mimi?
 
Back
Top Bottom