Hatimaye yule mbabe wa masumbwi ya Uzito wa juu duniani Anthony Joshua kutoka nchini Uingereza,usiku wa jana kuamkia leo amepokea kipigo kikali kutoka kwa Bondia mwenye umbo kama "kitimoto" Mmexico Andy Ruiz mwenye makazi yake California, nchini Marekani. Pambano hilo lilipigwa katika ukumbi wa Madison Square Garden, Newyork. Joshua alionyesha uhai kidooogo katika raundi ya tatu alipomuangusha mpinzani wake kwa konde zito,naye Ruiz alijibu mapigo kwa nguvu zote na kumlambisha sakafu mara mbili Anthony Joshua katika raundi hiyo ya tatu.Kiukweli AJ hakuwaweza kuonyesha makali yake kama tunavyomfahamu,yaani alikuwa anapigana kama hataki hali iliyopelekea mpinzani wake kumsukumia makonde mengi ya uso.Raundi ya 7 ndio ilikuwa mbaya sana kwa AJ alilambishwa sakafu mara mbili tena na kwenda angle yake, ambapo mwamuzi alimuuliza kama yuko tayari kuendelea lakini alikataa na kuwa mwisho wa game. Nilikuwa nampa AJ 100% za ushindi lakini imekuwa kinyume na matarajio yangu. Pambano hili limenikumbusha pigano la mwaka 1990 kule Tokyo nchini Japan kati ya Mike "Iron" Tyson na James Douglas "Buster" hakika kwa wale wakongwe waliokuwa wakimfuatilia Tyson kwa kila pambano alilokuwa akicheza hawakuamini kilichotokea huko Japan,kiukweli Tyson alikuwa na mashabiki wengi sana duniani kwa hiyo alipopigwa na James Douglas wengi hawakuamini walibaki na simanzi na baadhi walitokwa machozi kwa Tyson kushindwa. Ndicho kilichomtokea AJ ambaye usiku wa jana kuamkia leo. Mara nyingi tumeona kila mchezo anaocheza AJ anashinda. Hatimaye historia ya 1990 imejirudia. Kwa hiyo AJ amepokonywa mikanda yote mitatu aliyokuwa anaihold.