Baada ya kuridhika na Mahakama hiyo ilitoa dhamana kwa watuhumiwa wote saba kwa mashariti ya kuwasilisha mahakamani fedha taslimu kiasi cha shilingi milioni tatu kwa kila mmoja pamoja na kuwa wadhamini watatu ambao ni watumishi wa Serikali kwa kila mmoja akitoa kiasi kama hicho cha fedha mahakamani.
Watuhumiwa hao pamoja na Wadhamini wao, kwa pamoja wametakiwa kuwasilisha barua kutoka kwa Sheha wa Shehiya anayoishi pamoja na kivuli cha vitambulisho vya Zanzibar Mkazi na kwa wale wenye Hati za Kusafiria pia wawasilishe vivuli vya hati hizo Mahakamani.
Pamoja na masharti hayo ya jumla, lakini pia wadhamini wometakiwa wawe watumishi wa serikali na wawakilishe barua kutoka katika ofisi wanazozifanyia kazi na vivuli vya vitambulisho vyao vya kazi ili view kama kumbukumbu mahakamani.
Hata hivyo watuhumiwa wote wamerejeshwa rumande baada ya kushindwa kutekeleza masharti ya dhamana pamoja na kukabiliwa na kesi nyingine Mahakama Kuu ya Vuga, kesi ambayo dhamana yake imewekewa pingamizi kwa hati maalum ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar kwa sababu za kiusalama.