Breaking News:- Viongozi wa Uamsho wapewa dhamana

Breaking News:- Viongozi wa Uamsho wapewa dhamana

Baada ya kuridhika na Mahakama hiyo ilitoa dhamana kwa watuhumiwa wote saba kwa mashariti ya kuwasilisha mahakamani fedha taslimu kiasi cha shilingi milioni tatu kwa kila mmoja pamoja na kuwa wadhamini watatu ambao ni watumishi wa Serikali kwa kila mmoja akitoa kiasi kama hicho cha fedha mahakamani.

Watuhumiwa hao pamoja na Wadhamini wao, kwa pamoja wametakiwa kuwasilisha barua kutoka kwa Sheha wa Shehiya anayoishi pamoja na kivuli cha vitambulisho vya Zanzibar Mkazi na kwa wale wenye Hati za Kusafiria pia wawasilishe vivuli vya hati hizo Mahakamani.

Pamoja na masharti hayo ya jumla, lakini pia wadhamini wometakiwa wawe watumishi wa serikali na wawakilishe barua kutoka katika ofisi wanazozifanyia kazi na vivuli vya vitambulisho vyao vya kazi ili view kama kumbukumbu mahakamani.

Hata hivyo watuhumiwa wote wamerejeshwa rumande baada ya kushindwa kutekeleza masharti ya dhamana pamoja na kukabiliwa na kesi nyingine Mahakama Kuu ya Vuga, kesi ambayo dhamana yake imewekewa pingamizi kwa hati maalum ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar kwa sababu za kiusalama.
Kuna kila dalili za akina Farida na wenzake kuozea rumande. Ila ni kwa nia njema tu...
 
Jela makazi ya wakorofi! Gvt has to be careful na hili zigo la Udini TZ!

Zigo naona ni akili yako uliyoitune kuwa kila aliye gerezani ni mkorofi, pia zigo ni akili yako kwa kuteelewa nini udini. Na hapo ndio huwa tatizo, tulio wengi huwa tunakimbilia kuandika juu ya udini bila kuweka wazi Nani mdini, kivipi amekuwa mdini, na nini chanzo cha yeye kuwa mdini.
 
Back
Top Bottom