BRELA mnafanya vizuri ila boresheni utendaji kazi wenu

BRELA mnafanya vizuri ila boresheni utendaji kazi wenu

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
37,630
Reaction score
47,434
Napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza sana BRELA kwa maboresho katika utendaji kazi wenu mmekuwa active mno.

Baada ya pongezi nije kwenye hoja ya msingi ambayo imenifanya kuandika waraka huu ikiwa ni namna mnavyodeal na applications za registration ya makampuni.

Binafsi nimevutiwa na utaratibu mpya wa online registration umesaidia mno, Ila umekuja na changamoto zake.

1. Application kushughulikiwa na zaidi ya mtu mmoja.

Hili ni tatizo kubwa Sana na linapelekea ucheleweshwaji wa usajili kwa wakati.

Unapotuma application anayeipokea na kuifanyia kazi sio Yule Yule hii inapelekea mwendelezo kuwa wa kusua sua, huyu atakuambia lete hiki au rekebisha hiki, ukituma marekebisho anakuja mwingine kukuambia mengine ambayo wa Jana hakukuambia hivyo unaweza jikuta unapigwa Dana Dana hata miezi kadhaa.

2. Hakuna vigezo rasmi katika usajili.

Unakuta maombi ya Jana yamewekewa vigezo vyake.

Ukituma mengine kesho watakwambia vigezo vingine.

Kila Mara kumekuwa na vigezo mbali mbali ambavyo vinaleta usumbufu usiokuwa wa lazima kwa watumiaji wa mfumo.

Napendekeza yafuatayo:

1. Mgawanyo wa kazi,

Kwamba maombi yakishatumwa Basi aliyeanza kuyashughulikia aendelee nayo mpaka usajili utakapokamilika.

2. Vigezo vitavyofahamika na wadau.

Kwamba kwa kila category kuwe na vigezo Rasmi ambavyo kila mtu atapaswa kutimiza.

Au kunapokuwa na kigezo kipya taarifa zitolewe kwa wakati katika website yenu ili kila mtu ajue na avifuate kabla ya kupeleka maombi yake.

Otherwise kwa jinsi Mambo yanavyokwenda mdau anaishia kugombana na anaowahudumia au kushawishika kuwa mtoa Rushwa. Haipendezi kabisa.

Niishie kwa kuwapongeza kwa kazi nzuri mnayofanya na kuwaomba myafanyie marekebisho hayo niliyoyaainisha.

Kazi njema.
 
Mkuu umenena sahihi Sana.

Hiyo namba moja ndo napambana nao saizi
 
Brela malalamiko yamekuwa mengi mjirekebishe.
 
Sijui kwasasa ila BRELA hii ishu yao ya kusajili mrandaoni wamejitahidi sana. Nilisajili hadi kupata cheti ni mimi na kompyuta tu. Pia ukiwapigia simu hawazingui.
 
Sijui kwasasa ila BRELA hii ishu yao ya kusajili mrandaoni wamejitahidi sana. Nilisajili hadi kupata cheti ni mimi na kompyuta tu. Pia ukiwapigia simu hawazingui.
Hao utendaji wao upo kama homa za msimu mkuu, sisi tunaodeal nao mara kwa mara tunafahamu.

Kuna watu kazi zao ziko pending hata miezi miwili you can't imagine.

Mfumo ni mzuri ila wauboreshe.
 
Sijui kwasasa ila BRELA hii ishu yao ya kusajili mrandaoni wamejitahidi sana. Nilisajili hadi kupata cheti ni mimi na kompyuta tu. Pia ukiwapigia simu hawazingui.
Kiongozi mpya wa Brela anauadui mkubwa na staff usikute ni uhujumu tu wa uchumi maana ni jamaa arrogant sana sijui kabla alitokea wapi japo Nahisi ni TRA au BoT. Ni jamaa boguz to the maximum nililazimika kuomba tuonane baada ya kushindwa kupata usajili wa kampuni yetu ikabidi nitoe kidogodogo kwa jamaa Anaitwa Tulizo jamaa yng wa shinyanga. Ni wahuni wale aisee
 
Kiongozi mpya wa Brela anauadui mkubwa na staff usikute ni uhujumu tu wa uchumi maana ni jamaa arrogant sana sijui kabla alitokea wapi japo Nahisi ni TRA au BoT. Ni jamaa boguz to the maximum nililazimika kuomba tuonane baada ya kushindwa kupata usajili wa kampuni yetu ikabidi nitoe kidogodogo kwa jamaa Anaitwa Tulizo jamaa yng wa shinyanga. Ni wahuni wale aisee
Huku nje tunasubiri huduma kumbe wahusika wananuniana huko ndani na mambo hayaendi, aisee bongo mpaka tufikie malengo itachukua mda Sana.
 
Back
Top Bottom