BRELA yatangaza bei mpya za Usajili wa Makampuni na Majina ya Biashara kuanzia tarehe 1, Julai, 2015

BRELA yatangaza bei mpya za Usajili wa Makampuni na Majina ya Biashara kuanzia tarehe 1, Julai, 2015

MeinKempf

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2013
Posts
11,093
Reaction score
7,229
BRELA wametangaza bei mpya elekezi kwa ajili ya kusajili makampuni na biashara ambazo zitaanza kutumika kuanzia tarehe 01 July,2015.

=========

BRELA.png

TAARIFA KWA UMMA


Kufuatia Mangazo ya Serikali Namba 126 na 127 ya tarehe 25 Aprili 2014, ada mbalimbali zinazotozwa chini ya Sheria ya Makampuni (Sura 212) na Sheria ya Kuandikisha Majina ya Biashara (Sura 213) zimebadilika. Ada hizi mpya zitaanza kutumika rasmi kuanzia tarehe 1 Julai 2015, na zitakuwa kama ifuatavyo:-

Bonyeza hapa chini kusoma Taarifa hii kwa kirefu;

View attachment 269644010-bei-mpya-za-usajili-makampuni-na-majina-ya-biashara-ambazo-zitaanza-kutumika-kuanzia-.docx
 
Hebu tudokezeni hizo bei kwa ufupi, wengine sim hazifungui hiyo link
 

Brela.JPG

Kufuatia Mangazo ya Serikali Namba 126 na 127 ya tarehe 25 Aprili 2014, ada mbalimbali zinazotozwa chini ya Sheria ya Makampuni (Sura 212) na Sheria ya Kuandikisha Majina ya Biashara (Sura 213) zimebadilika. Ada hizi mpya zitaanza kutumika rasmi kuanzia tarehe 1 Julai 2015, na zitakuwa kama ifuatavyo:-

A: Sheria ya Makampuni (Sura 212)

1. Kampuni ambayo mtaji wake ni :
(a) Zaidi ya Tsh. 20,000/= lakini hauzidi Tsh. 1,000,000/= 95,000/=
(b) Zaidi ya Tsh. 1,000,000/= lakini hauzidi Tsh 5,000,000/= 175,000/=
(c) Zaidi ya Tsh. 5,000,000/= lakini hauzidi Tsh 20,000,000/= 260,000/=
(d) Zaidi ya Tsh. 20,000,000/= lakini hauzidi Tsh 50,000,000/= 290,000/=
(e) Zaidi ya Tsh. 50,000,000/= 440,000/=

2. Kwa usajili wa kampuni isiyokuwa na mtaji 300,000/=

3. Kutunziwa jina la kampuni 50,000/=

4. Kubadilisha jina la kampuni 22,000/=

5. Msajili kupokea au kusajili waraka wowote unaotakiwa kisheria kupelekwa kwake 22,000/=

6. Ada ya kuchelewa kupeleka waraka wowote unaotakiwa kisheria kupelekwa kwa Msajili (kwa mwezi au sehemu ya mwezi) 22,000/=

7. Kuwasilisha Mizania ya kampuni 22,000/=

8. Kuthibitisha waraka wowote, kwa kila ukurasa 3,000/=

9. Kufanya upekuzi kwenye jalada lolote 3,000/=

10. Kupata taarifa za kampuni kwa maandishi,kila jalada 22,000/=

11. Kusajili Hati ya Dhamana (Charge) iliyowekwa na kampuni 22,000/=

12. Kupata nakala ya Cheti cha usajili wa kampuni 4,000/=

13. Ada zinazolipwa na kampuni zinazoandikishwa chini ya sehemu ya XII ya Sheria :

(a) Kusajili katiba au waraka wowote unaotambulika kama ndio Katiba ya kampuni yao $ 750.00

(b) Kusajili au kuwasilisha waraka wowote unaopaswa Kuwasilishwa kwa Msajili chini ya sehemu ya XII ya sheria, Isipokuwa mahesabu ya kampuni $ 220.00

(c) Kuwasilisha Mahesabu ya Kampuni $ 220.00

(d) Ada ya kuchelewesha kuwasilisha kwa Msajili waraka wowote Unaopaswa kuwasilishwa kwake (kwa mwezi au sehemu ya mwezi) $ 25.00

B: Sheria ya Kuandikisha Majina ya Biashara (Sura 213)

1. i. Ada ya usajili wa Jina la Biashara 15,000/=
ii. Ada ya mabadiliko ya taarifa zilizosajiliwa 15,000/=
iii. Upekuzi kwenye daftari la Majina ya Biashara 2,000/=
iv. Ada ya kupata nakala ya nyaraka ambayo haijathibitishwa kwa kila ukurasa au sehemu ya ukurasa 3,000/=
v. Kuthibitisha nyaraka ya aina yoyote 4,000/=
vi. Ada ya kufuta jina la biashara 10,000/=
vii. Ada ya kupata nakala ya cheti cha usajili 15,000/=
viii. Malipo ya kuchelewa kuwasilisha nyaraka katika muda
uliopangwa, kwa kila mwezi au sehemu ya mwezi 1,000/=
ix. Ada ya utunzaji wa jalada kwa mwaka 5,000/=

2.

(i) Ushuru wa stempu hutozwa katika kila nakala ya cheti cha usajili wa Jina la Biashara kitakachoombwa 500/=

Imetolewa na
Msajili Makampuni / Majina ya Biashara
Simu: (+255-22)2181344 / 2180141 / 2180048 / 218004
 
Duuuhh. ....
Ongezeko la gharama ya usajili wa jina la biashara kutoka sh 6,000/= hadi sh 15,000/=???
 
tatizo ni mfumo wa ulipaji urahisishwe uwe benki moja kwa moja vinginevyo rushwa itakuwa kubwa sana eneo hili.
 
Inamaana unaweza ukaanzisha kampuni kwa mtaji wa tsh 20,000? Hapo sijaelewa.
 
Hivi nikitaka kusajili kampuni mwenyew nila kutumia middleman ni sh ngapi? Ni sole proprietor. Na inachukua muda gn?
 
Duh! Baada ya jamaa kuhamishia ofisi zao kwenye jengo jipya la ushirika ndio wameamua kutafutia hela ya kodi huku?
 
Nakuhusu tin kma hujapata ofisi bado unafanyaje? Maana wanahitaji mkataba was pango kma umepanga kwa ajili ya shufhuli zako
 
Back
Top Bottom