Vhagar
JF-Expert Member
- Jun 8, 2015
- 20,550
- 39,949
BRIGHTON YA ENGLAND YAONGOZA MBIO ZA KUMSAJILI MBWANA SAMATTA
Timu ya Brighton inaongoza mbio za Usajili za timu kutoka Ligi Kuu ya England ambazo zimeonyesha nia ya kumsajili Nyota wa Kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta anayechezea klabu ya Genk ya Ubelgiji
Seagulls, na timu kongwe ya Aston Villa iliyopanda Daraja msimu huu,Leicester, Watford na Burnley zote zina mmezea mate nyota huyo mwenye thamani ya kiaisi cha Pauni milioni 12- ili kumsajili.
Samatta,mwenye umri wa miaka 26 imefahamika ana shauku ya kuhamia kwneye Ligi kuu ya England baada ya kuwa na msimu mzuri kwenye Ligi Kuu ya Ubelgiji.
Amefunga magoli 23 na kuisaidia Genk kutwaa taji la Ligi Kuu pamoja na Tuzo Binafsi ya Kiatu cha Ebony.
Samatta atakiongoza kikosi cha Tanzania kwenye michuano ya Afcon baadaye mwezi huu,ni mara ya Kwanza kwa nchi yake kufuzu kwenye michuano hiyo tokea mwaka 1980.
Chanzo ya habari hii:The Sun la Uingereza .
Copy & paste.
Timu ya Brighton inaongoza mbio za Usajili za timu kutoka Ligi Kuu ya England ambazo zimeonyesha nia ya kumsajili Nyota wa Kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta anayechezea klabu ya Genk ya Ubelgiji
Seagulls, na timu kongwe ya Aston Villa iliyopanda Daraja msimu huu,Leicester, Watford na Burnley zote zina mmezea mate nyota huyo mwenye thamani ya kiaisi cha Pauni milioni 12- ili kumsajili.
Samatta,mwenye umri wa miaka 26 imefahamika ana shauku ya kuhamia kwneye Ligi kuu ya England baada ya kuwa na msimu mzuri kwenye Ligi Kuu ya Ubelgiji.
Amefunga magoli 23 na kuisaidia Genk kutwaa taji la Ligi Kuu pamoja na Tuzo Binafsi ya Kiatu cha Ebony.
Samatta atakiongoza kikosi cha Tanzania kwenye michuano ya Afcon baadaye mwezi huu,ni mara ya Kwanza kwa nchi yake kufuzu kwenye michuano hiyo tokea mwaka 1980.
Chanzo ya habari hii:The Sun la Uingereza .
Copy & paste.