BSS ina uchawi gani?mbona wengi hawafanikiwi?

BSS ina uchawi gani?mbona wengi hawafanikiwi?

Safi
Kwanza ni jambo la kujiridhisha kuwa si BSS tuu bali hata huko nje shows kama za the voice, SA idols, xfactors, na Got talents za nchi nyingi, ni watu wachache sana walio shinda mashindano ya aina hii wame make ki muzik.
Kwanini!!?
1. Lengo la mashindano, waandaji huwa wanaandaa kwa ajili ya faida yao na kupata wadhamini, na mara nyingi wakisha maliza shindano hawawekezi kwa nguvu kubwa kwani kuna shindano la mwakani inabidi waandae tena, hawana time na wewe
Pia washindanaji lengo lao kubwa zaidi ni kupata yale mamilioni tuu, wakisha pewa kuna msemo unasema easy come easy go
2. Mashabiki wa mashindano, askudanganye mtu, watanzania wanao fuatilia BSS ni chini ya milioni 10, wanao piga kura ni chini ya laki moja, kwa hiyo kama msanii ukishinda unakuwa hujapata fan base kubwa bado isipo kuwa ki portion kidooogoo cha wale walio angalia na wakajisumbua hata kupiga kura,,na wengi wanai piga kura huwa wanaanza kwanza kukuonea huruma ya kimaisha mfano unakumbuka Jumaanne Idd kwa hiyo Raymond akitoa wimbo mmoja uka hit anapata fan base kubwa kuliko wewe mshindi
3. Mziki ni zaidi ya kukopi nyimbo za watu, angalia yule mshindi wa mwaka jana kayumba alishnda kwa kuimba imba taarab za kina isha mashauz sasa je akitoka BSS ana uweza huo mziki!!? Mpaka yeye mwenyewe hajui afanyeje yaani

*sababu ni nyingi lakini kikubwa ni wasanii wajiamini wajue uwezo wao ni zaid ya kuimba BSS, ndio maana mara nyingi unakuta wanao fanikiwa ndio wale walio shika u tano, au ukumi, kwa kuwa it takes more than to win BSS ili kuwa msanii

Sor gazeti refu kidogo
Nilitaka kuja na hii hoja kwamba sio BSS tu watu wengi wanaopitia kwenye aina ya haya mashindano huwa hawafanikiwa asee ni wachache mnoo saivi namsubiri huyu aloimba na Akon sijui kama anaweza ku-make
 
bss hata haina maana yoyote! me sioni maana yake! kukariri mistari tu nakuiimba jukwaani hata me naweza japo sina nia wala sina wazo lakuwa msanii
 
Waungwana leo kwenye pita pita yangu nilikutana na miongoni mwa washiriki wa BSS aliyekuwa miongoni mwa waliofanya vizuri (jina kapuni) akiwa kachoka sana mpaka nikamuonea huruma, sasa nikawa najiuliza hivi hili shindano lina manufaa gani? Kwa nini washiriki wengi hawafanikiwi na majina yao hufifia baada ya muda mfupi?


Tuchukulie mfano mtu kama Jumanne Idd mpaka leo hajulikani halipo alkadharika Walter Chilambo, Kayumba , AngelMarry Kato , Steven Lupenza, Nasibu Fonabo nk ni miongoni mwa vijana ambao wana uwezo mkubwa sana wa kuimba lakini cha ajabu hawafanikiwi kulinganisha na washiriki wengine kama vile Harmonize ingawa alitoka mapema na kuonekana si chochote leo hii katudhihirishia kwamba yeye ana uwezo gani


Si harmonize tu pia nina mdogo wangu nisingependa kumtaja jina kwa sababu zangu binafsi ,naye pia alitolewa kwa maneno ya shombo na Salma Jabir kwa kuambiwa hajui kuimba bora akafuge kuku ndio kazi anayoiweza lakini leo hii ni msanii mkubwa tu

Hawa ni baadhi ya washiriki wa bss ambao washapotea kwenye ramani ya mziki


View attachment 412876huyu ni kayumba junior



View attachment 412878huyu ni Nasibu Fonabo



View attachment 412879huyu ni Favolii


View attachment 412880huyu ni Stev Lupenza







View attachment 412881Emmy Wimbo

View attachment 412882




View attachment 412883Angermarry Kato


View attachment 412887Frida Amani AKA queen fifi



Ujue muda mwingine mpaka nawaza, hivi hawa vijana wanafataga mpunga tu au? Maana huwa siwaoni kabisa shindano likiisha ,maana hupotea maziiiiiiima

Kama wengi wao wamefanikiwa kupata ' Mishuga Dadi ' na wengine kupata ' Mishuga Mami ' ulikuwa unataka wapate mafanikio gani tena mengine Mkuu? Kwani kwako Wewe hayo siyo mafanikio?
 
Walio shida chali kifo cha mende.
Walio shindwa wanafanya vzur mpaka kesho.

Maajabu ya bss
 
Back
Top Bottom