Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Buchosa. Baraza la madiwani Halmashauri ya Buchosa Wilaya ya Sengerema mkoani limelaani kitendo cha ofisa afya kata ya Maisome, Robert Masubugu kutoza faini wananchi bila kuwapa risiti.
Wanaotozwa faini ni wale waliokutwa na makosa na kutokuwa na vyoo na mabafu.
Kauli hiyo imetolewa leo Jumanne Februari 9, 2021 baada ya diwani wa Maisome, Dauson Miyaga kulieleza baraza hilo kwamba kuna malalamiko ya wananchi kutozwa faini ya Sh50,000 kila mmoja na hawapewi risiti na kuzua maswali mengi kuhusu suala hilo.
“Fedha za Serikali zinapotea watu wanaweka mifukoni mwao tunapaswa kuliangalia suala hili kwa mapana na kuokoa fedha hizi," amesema Miyaga akibainisha kuwa kuna mazoea ya maofisa wa Serikali kufanya misako kwa wananchi na kutoza faini bila kutoa risiti.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Buchosa, Crispin Luanda amesema hajui lolote kuhusu suala hilo na kuwataka madiwani kumpatia muda ili afanye uchunguzi ili aweze kuchukua hatua stahiki.
Hivi Karibu kumekuwa na malalamiko ya baadhi ya watumishi hasa wa ngazi ya kata ya vijiji kutotoa risiti na baadhi kuendesha msako wa walioshindwa kujenga choo na bafu.
Ofisa afya wa Maisome, Robert Masubugu amesema hajawahi kutoza mtu yoyote fedha akiwa na makosa ya kutokuwa na choo wala bafu, kwamba anachofanya ni kutoa elimu ili jamii itambue umuhimu wa choo na bafu.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Buchosa, Idama Kibanzi amemwagiza mkurugenzi kuchunguza tuhuma hizo na ikibainika achukuliwe hatua za kinidhamu.
Wanaotozwa faini ni wale waliokutwa na makosa na kutokuwa na vyoo na mabafu.
Kauli hiyo imetolewa leo Jumanne Februari 9, 2021 baada ya diwani wa Maisome, Dauson Miyaga kulieleza baraza hilo kwamba kuna malalamiko ya wananchi kutozwa faini ya Sh50,000 kila mmoja na hawapewi risiti na kuzua maswali mengi kuhusu suala hilo.
“Fedha za Serikali zinapotea watu wanaweka mifukoni mwao tunapaswa kuliangalia suala hili kwa mapana na kuokoa fedha hizi," amesema Miyaga akibainisha kuwa kuna mazoea ya maofisa wa Serikali kufanya misako kwa wananchi na kutoza faini bila kutoa risiti.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Buchosa, Crispin Luanda amesema hajui lolote kuhusu suala hilo na kuwataka madiwani kumpatia muda ili afanye uchunguzi ili aweze kuchukua hatua stahiki.
Hivi Karibu kumekuwa na malalamiko ya baadhi ya watumishi hasa wa ngazi ya kata ya vijiji kutotoa risiti na baadhi kuendesha msako wa walioshindwa kujenga choo na bafu.
Ofisa afya wa Maisome, Robert Masubugu amesema hajawahi kutoza mtu yoyote fedha akiwa na makosa ya kutokuwa na choo wala bafu, kwamba anachofanya ni kutoa elimu ili jamii itambue umuhimu wa choo na bafu.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Buchosa, Idama Kibanzi amemwagiza mkurugenzi kuchunguza tuhuma hizo na ikibainika achukuliwe hatua za kinidhamu.