GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
Watu sita wamefariki dunia na wengine tisa kujeruhiwa katika ajali ya gari, linalofanya safari zake kati ya Kemondo na Bukoba Mjini, ajali hiyo imetokea maeneo ya Rwamishanye Bukoba..( dakika 14 zilizopita )
Chanzo: Habari Leo Online
--UPDATE--
Watu nane wamefariki dunia na wengine sita wanapatiwa matibabu katika Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera baada ya gari walilokuwa wanasafiria kukatika mfumo wa breki kabla ya kutumbukia shimoni.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Kagera, Revocatus Malim basi hilo dogo linalofanya safari zake Kemondo na Manispaa ya Bukoba limepata ajali katika barabara ya Uganda, Mtaa wa Rwamishenye.
Ameeleza kuwa gari hilo aina ya Toyota Hiace lenye namba za usajili T471DCG lilikuwa linatokea Kemondo na kwenda Bukoba Mjini jana.
Alisema kuwa Polisi wanamshikilia dereva wa gari hilo, Ismaili Rashid.
-----
Siku zingine Watani zangu muwe mnajitahidi tu kabda ya Kusafiri muwe mnahakikisha kuwa mmeshatambika katika hiyo Migomba yenu na hizo Ndizi.
Chanzo: Habari Leo Online
--UPDATE--
Watu nane wamefariki dunia na wengine sita wanapatiwa matibabu katika Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera baada ya gari walilokuwa wanasafiria kukatika mfumo wa breki kabla ya kutumbukia shimoni.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Kagera, Revocatus Malim basi hilo dogo linalofanya safari zake Kemondo na Manispaa ya Bukoba limepata ajali katika barabara ya Uganda, Mtaa wa Rwamishenye.
Ameeleza kuwa gari hilo aina ya Toyota Hiace lenye namba za usajili T471DCG lilikuwa linatokea Kemondo na kwenda Bukoba Mjini jana.
Alisema kuwa Polisi wanamshikilia dereva wa gari hilo, Ismaili Rashid.
-----
Siku zingine Watani zangu muwe mnajitahidi tu kabda ya Kusafiri muwe mnahakikisha kuwa mmeshatambika katika hiyo Migomba yenu na hizo Ndizi.