Bulb zako za LED zimeungua? Usitupe, suluhisho limepatikana!

Bulb zako za LED zimeungua? Usitupe, suluhisho limepatikana!

Sikia mkuu, ikiwezekana wewe zinunue mbovu, zenye hitilafu, tengeneza, rekebisha, kisha uza tena(sambaza kwenye maduka ya vifaa vya umeme)
Unanunua yale mabovu kwa mafungu, mfano taa 10 kwa elfu 1, kila moja hapo umeinunua kwa 100, rekebisha weka buku lako la ufundi na 400 kama usafiri, we wasambazie wauzaji kwa 1500, ye akiuza elfu 2 sawa, na kama zinakuwa zinatoka we hata ukiwauzia kwa buku buku tu bado itakuwa vema kuliko kukaa kusubiri wateja walete taa zao mbovu.
Kwanza kuna watu wapo mbali sana, mfano we unaweza ukawa chanika mie tegeta, ngumu kukuletea taa zangu 2 uzitengeneze, sababu ya nauli, muda na kitu chenyewe kipya nakipata kwa bei chee,
Ila wewe ukikusanya mbovu utazipata za watu wa tegeta, mbezi, kigamboni, kisha we unarelebisha unasambaza wananunua,
Hapo unakuwa umemtengenezea wa tegeta kwa namna nyingine
umeandika kirahisi sana,biashara kwa maandishi kwenye karatasini rahisi sana..kwa ushauri wako huu si ajabu ukamponza kwenda jela au akapoteza pesa nyingi kujinasua kwenye msala kwa kutokuwa na leseni ya hiyo biashara au kulipa kodi TRA..kwanza kununua taa mbovu na kuzitengeneza ni vizuri..maboksi ya hizo taa atayapata wapi baada ya kuzitengeneza maana alienda kuuza kwa wenye maduka lazima hizo taa ziwe kwenye kibox na kwa vile alikusanya taa nyingi za LED bila shaka zitakuwa za kampuni tofauti tofauti na hiyo ni gharama nyingine ya maboksi..na mwisho taa used iliyotumika zaidi ya miezi 6 tena iliyopauka kwa vumbi,mvua na jua kimuonekano haiwezi kuwa sawa na mpya..je,wenye maduka na wateja wao wataziamini na kuzinunua hizo taa zilizopauka kwa vumbi na jua alafu waache mpya.!
 
Back
Top Bottom