Bulembo: Polepole ni Unyasi kaletwa CCM na kokoro, V8 ameijulia CCM, Bashiru alitoka CUF. Nataka Mdahalo na Polepole

Kwani CCM ni ya baba yako tu,mtu yeyote anaweza kuingia CCM na kutoka huyu Bulembo ni tapeli tu wa mjini,kwanza alipe hela ya kukodisha choo pale ilipokuwa stand ya mabasi Mwenge ,juu ndio kilikuwa kiofisi chake, ngumbaru anataka apambane na wasomi na huyu huyu alivyo mnafiki ndie alikuwa kimbelembele enzi za mwendazake,leo kaanza kujikomba kwa mama, tahadhari kwa mama watu wa sampuli hii ndio hao hao watakusaliti na kukusimanga ukisha toka madarakani, Bulembo anaishi mjini kwa kutumia maneno, arudishe na shule zetu za jumuia ya wazazi (TAPA)
 
Kwa kuwa Bulembo ni fisadi lazima awachukie akina Polepole,Bashiru na wengineo wapya kwa kuwa hawa ndio waliokata mizizi ya kufisadi mali za chama baada ya mwendazake kuunda tume chini ya Bashiru kuhakiki mali za chama na kuangalia njia za kuziba mianya ili chama kijijengee uwezo wa kujitegemea na Bashiru bila kupepesa macho ripoti yake ilionyesha ufisadi mkubwa wa kujiuzia au kuuza mali za chama chini ya akina marope,mzee wa vipusa /meno ya tembo/bulembo na wengineo hawa waliuza mali za chama ikiwemo mitambo, shule vituo vya runinga n.k. Ni hekima na busara tu za mwendazake ambazo ziliwafanya hawa wakora wasiwe wageni wa serikali. Hizi kelele zote hizi ni'' KURUDI KWA WEZI''
 
C
CCM chama cha ajabu Sana ,that's kijina ukiwa ccm lazima ujipime Mara mbili ,au ukapimwe mirembe, kwamba ndani ya ccm mwanachama wa mda mrefu Basi haki yako ni kubwa kuliko Wanachama wengine, upumbavu mtupu ndani ya Chama Wanachama wote lazima kua na haki sawa Mbele ya katiba
 
Walikuwa wakimuogopa aseme ukwel bhana
 
Wewe unae soma comment tambua kuwa Bulembo Hana jipya
 
Mkubwa waache hao mbwa walane wenyewe kwa wenyewe
 
Bulembo ni mwizi mkubwa. kazi yake ilikuwa kuosha vyoo, kajiunga na siasa Leo ni tajiri mkubwa kwa kuuza mali za CCM. Huyu alitakiwa kuwa gerezani. Awamu ya nne iliyokuwa imejaa wahuni haikumufunga kama wahunu wengine. Akaja kutimuliwa awamu ya tano, iliyokuwa ikisafisha wahuni serikalini na CCM. Kwa sasa anajipendekeza kwa Mama, mama hajuwi record zake za wizi. Huyu ni mwizi mkubwa mama. Asikudanganye na tuhuma za uwongo kwa PolePole kuficha maovu yake. huyu ni mwizi aliuza shule za wazazi wa CCM. Angetakiwa awe jela kifungo cha maisha. Hafai kabisa serikalini hata kufunguwa mdomo wake. Kweli wahuni bado wako. Lazima tusimame na PolePole kufukuza wahuni.
 
Huyu Bulembo alifaa awe Jela,kahusika sana kuuza mali za Jumuiya ya wazazi.
CCM yenyewe ingekuwa jela kwa kupora mali za Watanzania na kuzimiliki kiharamu kama zake. CCM imeipora hadi Katiba ya nchi na kuihatamia kama kuku na kuwaona wananchi kama vifaranga wake.

CCM imejengwa kwenye misingi ya dhuluma na yeyote anayejiunga na CCM ni kwamba anakubaliana na sera ya dhulma. Uporaji, utekaji, utesaji, wizi, rushwa na ufisadi ni sifa zilizoiganda CCM kama kupe.

CCM iko tayari hata kuua kulinda uovu wao. CCM ni manyanga'au na hofu kubwa ya manyang'au ni pale mzoga unapokaribia kuisha, hapo watatafunana wao kwa wao na ole wako ukutwe na damu mdomoni!

Hakuna mwana CCM asiye na hizo sifa, period!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…