Uchaguzi 2020 Bulendu: Kanuni na Sheria za Uchaguzi zimetungwa kuwa Muathirika wa kanuni hana Haki ya kudai haki inayovunjwa. Tunatengeneza Magaidi wenyewe

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2012
Posts
4,572
Reaction score
26,885
Kanuni na maelekezo yanayosimamia uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 baadhi yana ukakasi mwingi na kama dhana ya uadilifu kwa baadi ya watu haitaheshimika itasababisha uchaguzi huu kuwa na malalamiko mengi na hasa siku ya kupiga kura, kuhesabu na kutoa matokeo, maeneo ambayo yanashida kwa jicho langu ni yafatayo.

1. Kama kutakuwa na uhaba wa fomu za matokeo, mawakala hawatapatiwa nakala hizo za matokeo(Ubunge, Udiwani, Urais), nachojiuliza kwanini fomu zisitoshe? Tume ihakikishe kunakuwa hakuna uhaba wa fomu za matokeo ili kila wakala apewe nakala yake,hii ya kusema "kama kutakuwa na uhaba, mawakala hawatapewa nakala ya matokeo, inaweza kusababisha malalamiko yasiyo na msingi.

2. Nakala ya fomu ya kiapo (fomu namba 6) kutotumika kwa ajili ya utambulisho wa mawakala, na pia wakala aliyeapa hatapewa nakala ya fomu hizo baada ya kuapa, hii si sawa kwa mtazamo wangu.

Kwa nini si sawa,unaweza kuta mgombea ameandaa mawakala wake, wanafika asubuhi kwenye kituo wanakuta watu wengine washaingia na wasimamizi wamewatambua halafu mawakala halali walioapa wanawekwa pembeni,hii inaweza kuleta malalamiko yasiyo na ulazima,ni vizuri tume ikatumia fomu namba sita kuwatambulisha mawakala na wawe ni wale waliotambulishwa na vyama vyao ama wagombea na siyo vinginevyo.

3. Waandishi wa habari kutotambulika kama kundi linaloruhusiwa kuingia kwenye chumba cha kupigia kura, hii inaacha maswali mengi, kwa nini waangalizi waruhusiwe kuingia wakati wote kuanzia zoezi la kupiga kura mpaka kuhesanu halafu waandishi wawekwe kando?

4. Mawakala hawataruhusiwa kuingia na simu wala kutumia kwenye vituo vya kupigia kura, kwanini mawakala wazuiliwe isipokuwa msimamizi wa kituo na mlinzi pekee, kwanini mawakala wanahofiwa kuingia na simu? Kama dhana ni uchaguzi unaozingatia dhana ya uwazi,binafsi sioni tatizo kwa wakala kuingia na simu.

5. Matokeo ya Urais kutopingwa mahakamani,je nchini Tanzania Kwa nini sheria iweke katazo hili?tunaamini haitakuja kutokea matokeo ya Urais yakawa na mazongwe ambayo yanahitaji HAKI ikasakwe mahakamani?

Hata kwenye hatua hii ya utezi kumekuwa na matatizo ya Kisheria na kikanuni, mfano

1. Sheria na kanuni zake zinaposema maamuzi ya tume ya kumkata mgombea ndiyo yatakuwa maamuzi ya mwisho na hayatapingwa kwenye mahakama yeyote, kwangu hili ni tatizo,yaani leo mimi haki yangu ikibinywa na tme naambiwa sina haki ya kwenda mahakama yeyote?ila nisubiri mpaka uchaguzi utakapoisha ndiyo nitakuwa na hiari ya kwenda kupinga ushindi mahakamani? Kwa niniuamizi wa tume uwe wa mwisho? Na kipindi hiki tumeshuhudia maamuzi mengi yenye utata kutoka tume.

2. Chama kutokupewa nafasi ya kubadili mgombea pale aliyepitishwa anapopatwa na shida, mfano kwa mujibu wa sheria na kanuni za uchaguzi, mgombe anatakiwa yeye mwenyewe kuwasilisha fomu yake, vipi kama atapatwa na shida ya afya? Ama kukamatwa kama ilivyojitokeza jimbo la Mtama mkoani Lindi?
 
Hizi sheria zimetungwa na ama watu wasio na akili kabisa ama ni maelekezo ya mtu asie na akili wala hisia kama jiwe!
 
Nyerere aliasisi ile sheria ya NEC ikishatangaza matokeo ya Urais hakuna nafasi ya kupinga mahakamani au kwenye chombo chochote kingine. Alifanya hivyo kwa nia ya kuhakikisha chama alichokiasisi haking'oki madarakani. Athari ya Sheria hiyo ilianza Zanzibar katika uchaguzi wa mwanzo wa vyama vingi pale ambapo "mpira ulishavuka msitari wa goli" lakini refa ( ZEC)) baada ya kimya cha siku kadhaa akaibuka na kusema SIO GOLI!!! Na huo ndio umekua utaratibu

Baada ya Mwalimu waliofuatia wamekua "wakiboresha" sheria na kanuni hizo kwa lengo la kuhakikisha uchaguzi unakua ni ile kamari maarufu ya "CHEUSI CHEKUNDU". Yaani cheza uchezavyo, fanya lolote lakini kamari ile HUWEZI KUSHINDA! Anayeshinda ni mchezeshaji tu na ukileta hoja zako unaweza kutobolewa macho maana wanakua ni genge la maharamia wa kuibia watu
 
Asilimia kubwa ya Sheria na Kanuni zilizotungwa nchi hii kwenye hii miaka 5

Nasikitika kusema zote zilitungwa kumbana TUNDU LISSU[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Najiulizaz akina Tundu Lissu wakiwa wengi nchi hiii, Izo sheria na kanuni itakuaje?

Mpaka hili la Kuzuia Drones, nikisa tu Nyomi la Lissu lisionekane .[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hii siyo tume ya kusimamia uchaguzi bali ni ya kuvuruga uchaguzi kwa manufaa ya watawala
 
Asante mtoa mada ndio maana tunamhitaji Lissu tuwe na katiba bora tupate uhuru, haki, ustawi,umoja na maendeleo.
 
Mtoa mada umeandika ukiwa umetulia!! Kuna maprofessor wa sheria wengi tu ,wengine ni wandamizi serikalini inaskitisha sheria za ovyo namna hii zmeangaliwa na maprofessor hawa kwa muda mrefu pasipokuangalia mstakabar wa Taifa letu.

Sheria mbofumbofu znazotudhalilisha kama Taifa Znaendelea kutumika katika maisha yetu zikitunyanyasa wenyewe na Wasomi wa sheria wapo!!Hivi nini mana ya usomi namna hii. Ninani yuko nyuma ya Sheri mbofumbofu hizi?

Na wasomi wa sheria na mabaraza yenu Mumeifanyia nini Nchi hii? Kwanini wanasiasa Wamehodhi ufahamu wenu kiasi hiki? Taifa lolote msingi wa ustaarabu huanzia kwenye mifumo imara ya utawala na mfumo mzuri wa upatkanaje wa mamlaka ya wananchi ndy msingi wa Taifa lolote makin.

Je, Wasomi wetu wa Sheria nani amechukua akili zenu?
 
CCM ILITUNGA HIZI SHERIA KANDAMIZI ILI WATUTAWALE MILELE. SAFARI HII KAMA NOMA NA IWE NOMA
 
Vita, Machafuko, Ugaidi na vikundi vya Waasi ktk Nchi za Afrika sababu zake ni Sheria kandamizi pamoja na dhuluma toka Kwa watawala na vyama vyao...

Machafuko safari hii Kwa Tanzania sioni kama yanaepukika, CCM haitaki kushindana na vyama vingine kwenye uwanja sawa..

Nchi imejaa Uvumilivu tu na hakuna Amani kabisa Tanzania hii...
 
Hizi sheria ni mbovu kuliko za utawala wa shetani. Dawa ni kuitoa nchi mikononi mwa magaidi policcm na cccm lao
Wee unadhani kwanini wananchi wa Chato walikuwa wakiimba...
" Bora Corona kuliko CCM? "
 
Sheria yoyote inalenga kutekeleza sera fulani au kutatua tatizo fulani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…