KWELI Bundi si mchawi, ana uwezo mkubwa wa kunusa seli zilizokufa

KWELI Bundi si mchawi, ana uwezo mkubwa wa kunusa seli zilizokufa

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Nimesoma sehemu kuwa ndege aina ya Bundi, licha ya kuhusishwa na imani za kichawi kama mikosi, mtu kufariki akionekana au kusikika akilia jirani, kutokea ghafla nk eti si kweli kwamba ni mchawi bali ana uwezo wa kunusa mtu aliyekaribia kufa.

IMG_7903.jpeg

Je, ukweli wake ni upi?
 
Tunachokijua
Bundi ni nani?
Bundi ni moja ya aina ya ndege wawindao, huishi kwa kutegemea kula nyama, huwinda chakula chake wakati wa usiku hasa wakati wa giza ili kuepusha ushindani dhidi ya ndege wengine walao nyama kama vile mwewe na tai, pia hii humsaidia kukamata wanyama hawa kwa urahisi usiku wakiwa wamelala.

Mara nyingi bundi huutumia mchana kwa mapumziko.

bundi-pic.jpg

Sifa za bundi na tabia zake
  • Bundi huwinda wanyama wadogo wadogo kama vile: panya , mijusi, ndege na wadudu
  • Bundi jike huwa na umbo kubwa zaidi, rangi yake imekoza zaidi na huwa mkali kuliko dume.
  • Bundi jike huwa na uwezo wa kutaga mayai yapatayo 12, lakini kwa mara nyingi hutaga mayai 4 – 8 yakipishana siku moja hadi mbili.
  • Bundi wana uwezo wa kuishi mabara yote isipokuwa bara la Antaktika, bundi waishio kwenye maeneo yenye baridi huwa na maumbo makubwa zaidi wakilinganishwa na wale wanaoishi kwenye maeneo yenye joto.
  • Bundi mkubwa ana uwezo wa kumuwinda bundi mwenye umbo dogo wa aina(spices) nyingine, yaani cannibalism.
  • Bundi ana uono wa mara saba (7) ya uono alionao binadamu, lakini pamoja na sifa hiyo hawezi kuona vitu vilivyo karibu, hivyo bundi hatumii macho kuvamia windo lake, ana uwezo wa kukamata windo lake akiwa amefumba macho
  • Kichwa cha mviringo na macho yake yenye uwezo wa kuyafumba na kuyafumbua kama binadamu, umbo lake na rangi yake, mwonekano wa kichwa chake uwezo wa kugeuza kichwa chake pande zote kwa nyuzi 270° pasipo kuhusisha mwili mzima.
  • Bundi hupaa kimyakimya bila ya mabawa yake kupiga kelele, hii ni kutokana na umbo la mabawa yake na mfumo wa manyoa, manyoa yaliyopo miguuni mwa bundi hufyonza kelele zitokanazo na upepo, hivyo kuzuia kelele akiwa anapaa. Zaidi soma Mfahamu Bundi
Je, imani za kumuhusisha Bundi na uchawi, mikosi au vifo zina ukweli gani?
JamiiForums imepitia tafiti mbalimbali kuhusu maisha ya ndege aina ya bundi na imejiridhisha kuwa imani za uchawi au bundi kuhusishwa na vifo pamoja na mikosi ni imani potofu, bundi si mchawi wala hana mahusiano na mikosi wala vifo vya binadamu.

Moja ya tafiti imefanywa na mtafiti kutoka Taasisi ya Kudhibiti Viumbe hai Waharibifu katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Dk Nicolaus Mwakalinga ambaye ameeleza kuwa imani zinazohusishwa na bundi ni uzushi na potofu na yeye amegundua bundi wana faida nyingi kwa binadamu ikiwemo ulinzi wa mazao shambani dhidi ya panya kutokana na uwezo wao wa kula panya saba hadi 12 kwa siku mbili hadi tatu. (Soma zaidi: Utafiti wa bundi wa chuo Kikuu SUA)

Baadhi ya maswali yanayozalisha imani Potofu kuhusu bundi
Kwa nini Bundi hutokea ghafla(kichawi)

Bundi hatokei ghafla ila huja bila kugundulika kirahisi kutokana na kupaa kimyakimya bila ya mabawa yake kupiga kelele, hii ni kutokana na umbo la mabawa yake na mfumo wa manyoa, manyoa yaliyopo miguuni mwa bundi hufyonza kelele zitokanazo na upepo, hivyo kuzuia kelele akiwa anapaa.

Pia rangi za manyoya ya bundi hufanana Sana na mazingira yake hivyo kumfanya bundi asionekane kwa urahisi hasa wakati wamchana, na ikitokea mtu kamuona hudhani katokea ghafla hali ya kuwa anaweza kuwa alikuwepo hapo kwa muda mrefu nyuma.

Pia bundi huweza hukaa kwenye tawi la mti au sehemu nyingine bila kutingishika hivyo kuonekana kama kiumbe kisicho na uhai kama vile jani la mti au kisiki hali ambayo hufanya watu wasimuone kwa wepesi na ikitokea kahisi hatari huweza kutikisika au kutoa mlio ambao huwaogopesha binadamu na kuhisi katokea kichawi wakati huo.

Bundi hulia usiku na kuleta mikosi
Mlio wa bundi usikikapo usiku sio mkosi kama wasemavyo watu wengi, kama ilivyo kwa ndege wengine bundi hutoa mlio kwa ajili ya mawasiliano baina yao hii inaweza kuwa; kuitana, kuogopa, kumtishia au kumkimbiza adui na sababu nyingine ziwafanyao ndege wote kutoa milio.

Bundi hulia usiku kwa kuwa ndio muda ambao yeye huutumia kufanya shughuli zake za uwindaji, hasikiki mchana kwa kuwa mchana huutumia kama muda wake wa kupumzika(kulala) ivyo kulia kwake hakuna mahusinao na imani hizo potofu bali ni maisha yake ya kawaida kama ndege wengine.

Kwa nini bundi akionekana mara nyingi mtu hufariki eneo hilo?
Bundi ana uwezo mkubwa sana wa kuvuta harufu ya mzoga kutoka mbali. Uwezo huu wa kunusa harufu unapita uwezo walionao binadamu.

Hivyo inapotokea katika nyumba fulani kuna mgonjwa mahututi ambaye seli za mwili wake zimeshaanza kufa lakini mapigo ya moyo bado yanafanya kazi; Bundi huweza kunusa harufu ya seli hizo, harufu ambayo binadamu hawawezi kuihisi, na hivyo huvutiwa kuisogelea kwa ajili ya kujipatia chakula, ila hataweza kuingia ndani kwa kuhofia binadamu.

Aidha, maneno ya Makheya, Afisa kutoka Taasisi ya TAWA wakati akizungumza na Nipashe kwenye maonesho ya Sabasaba, Julai 5, 2023 yanayosema "Huyu ndege ni ndege kama walivyo ndege wengine, kama nilivyosema ana uwezo wa kunusa seli zilizokufa kwa maana ya chakula, wakati anatafuta chakula......Kama kuna mgonjwa au mgonjwa ambaye yupo kwenye hatua za mwisho anauwezo wa kunusa harufu ya seli zilizokufa" yana ukweli.

Kwa kawaida binadamu hafi mara moja, bali hufa hatua kwa hatua (mchakato).

Huwa zinaanza kwanza kufa seli za mwili, baadaye ogani mbalimbali za mwili. Ogani za mwisho kufa ni moyo ikifuatiwa na ubongo. Hivyo bundi anapoonekana kwenye nyumba yenye mgonjwa mahututi ni dalili kwamba mgonjwa huyo ameshaanza hatua za kufariki, na hivyo uwezekano wa mgonjwa huyo kufariki siku za karibuni ni mkubwa sana.

Inapotokea kwamba mgonjwa amekufa baada ya bundi kuonekana, tafsiri sahihi siyo kwamba kifo kimesababishwa na bundi bali ni kwamba dalili za kifo cha mgonjwa huyo zimetambuliwa na bundi.

Hivyo cha kufanya siyo kumtafuta mchawi.

Pia soma: Bundi hunusa seli za aliyeanza kufariki
Nimesoma sehemu kuwa ndege aina ya Bundi, licha ya kuhusishwa na imani za kichawi kama mikosi, mtu kufariki akionekana au kusikika akilia jirani, kutokea ghafla nk eti si kweli kwamba ni mchawi bali ana uwezo wa kunusa mtu aliyekaribia kufa.


Je, ukweli wake ni upi?
Ila arudi field atafute kuna uhusiano gani kati ya bundi na mchawi....
Tusikaze fuvu haya mambo yapo🤣🤣
 
Hiyo ya bundi kuonekana jirani na nyumbani ni kisanga kingine, unaposoma huu uzi na ukaja kumuona bundi kwenye mti hapo kwako, fasta unauliza kama kuna mtu anajisikia vibaya (kuumwa) 😂!.

Vinginevyo utakimbiza familia hospitali kwa check-up.
 
Hiyo ya bundi kuonekana jurani na nyumbani ni kisanga kingine, unaposoma huu uzi na ukaja kumuona bundi kwenye mtu hapo kwako, fasta unauliza kama kuna mtu anajisikia vibaya (kuumwa) [emoji23]!.

Vinginevyo utakimbiza familia hospitali kwa check-up.
Umenichekesha Mkuu, nilivyoelewa ni kuwa seli anazonusa si za binadamu pekee bali za viumbe hai vyote ambazo zimekufa.

Huenda hapo jirani kuna kiumbe kingine kilichokufa (mzoga) au kuna panya, mijusi ambavyo ni vyakula vyake ivyo atakuja tu kula si lazima awe binadamu kafa au kakaribia kufa.
 
Kama ilivyo kwa birds of prey (ndege walao nyama) wengine ukimtoa vulture (yule ndege anakula mizoga hifadhini) wana uwezo mdogo sana wa kunusa harufu. Kundi hili linahusisha ndege kama Tai, Mwewe, Bundi, nk..

Ndege walio katika kundi hili hutumia zaidi nguvu ya uono waliyonayo kuwinda kuliko kunusa harufu.

ndio maana ndege walio katika kundi hili hula hata nyama kama mizoga nk, nyama isiyolika na wanyama wengine walao nyama.

Kwa hiyo kusema Bundi ana uwezo mkubwa wa kunusa seli zilizoanza kufa SI KWELI!
 
Kama ilivyo kwa birds of prey (ndege walao nyama) wengine ukimtoa vulture (yule ndege anakula mizoga hifadhini) wana uwezo mdogo sana wa kunusa harufu. Kundi hili linahusisha ndege kama Tai, Mwewe, Bundi, nk..

Ndege walio katika kundi hili hutumia zaidi nguvu ya uono waliyonayo kuwinda kuliko kunusa harufu.

ndio maana ndege walio katika kundi hili hula hata nyama kama mizoga nk, nyama isiyolika na wanyama wengine walao nyama.

Kwa hiyo kusema Bundi ana uwezo mkubwa wa kunusa seli zilizoanza kufa SI KWELI!
Endelea sasa kukaza fuvu
 
Nimesoma sehemu kuwa ndege aina ya Bundi, licha ya kuhusishwa na imani za kichawi kama mikosi, mtu kufariki akionekana au kusikika akilia jirani, kutokea ghafla nk eti si kweli kwamba ni mchawi bali ana uwezo wa kunusa mtu aliyekaribia kufa.


Je, ukweli wake ni upi?
Kweli kabisa! Uzoefu wangu ni kwamba kwetu kule UK (UKerewe) bundi huhusishwa na wachawi na akitua kwenye nyumba au mti jirani usiku au mchana watu wanakuwa na hofu kwamba kuna mtu most probably 'atadondoka' nyumbani hivi karibuni. Kwa vile nilikulia katika hofu ya namna hii ya jamii inayonizunguka, nami haikuniacha salama (niseme hadi leo). Nilipata fursa ya kukaa Malawi almost miaka 7 na kule bundi haogopwi na hahusishwi na misfortunes, anapendwa kwa sababu ni ishara ya hekima/busara. Hivyo, bundi akilia karibu na nyumbani wenyeji kule hawaogopi kwa sababu hahusishwi na uchawi. Kwa sasa nipo huku kwetu Tz na nyumbani kwangu nimepanda miashoki mingi kuzunguka kiwanja na kwa vile hii miti hurefuka, nadhani bundi wanaona ni salama zaidi kututembelea mara kwa mara usiku. Na kama bundi angekuwa anaashiria hatari iliyopo au inayokuja nyumbani, basi sisi tungekutwa na misfortunes almost kila baada ya siku chache maana kila bundi akilia usiku most probably analilia kwenye hii miashoki ambayo mimi nadhani pamoja na hofu kidogo ambayo ninayo (siyo sana kama Watz na wana UK wengine, of course) ni kwa sababu bundi wanaona hapa kwetu wako salama zaidi. Hata wife, ingawa naye alikuwa na hofu kubwa, lakini kwa sababu anasikia bundi wanalia almost kila wiki au kila baada ya siku chache, naye hofu yake inaendelea kupungua. Ni hofu ya bure! Bundi siyo alama ya 'misfortune' if anything ni alama ya good news na maisha marefu.
 
Hiyo ya bundi kuonekana jirani na nyumbani ni kisanga kingine, unaposoma huu uzi na ukaja kumuona bundi kwenye mti hapo kwako, fasta unauliza kama kuna mtu anajisikia vibaya (kuumwa) [emoji23]!.

Vinginevyo utakimbiza familia hospitali kwa check-up.
Hahaha!! Family nzima unaipeleka Hospital ikakae ICU kabisa wapate uangalizi mkali
 
Back
Top Bottom