Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Fuatilia yanayojiri Bungeni leo Februari 7, 2023 kwenye Mkutano wa 10, Kikao cha 6
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imebaini Miamala kufutwa au baadhi ya tarakimu kurekebishwa bila idhini ya Maofisa Masuhuli au bila kuwapo kwa nyaraka za Uthibitisho wa uhalali wa marekebisho hayo katika Halmashauri za #Ubungo, #Kigamboni #Ilemela na #Iringa
Mfano; Mnamo 4/09/2019 katika Manispaa ya #Ubungo, Tsh. Milioni 689.3 ziliingizwa katika akaunti ya Manispaa na kutolewa Siku hiyo hiyo kwa madai Benki ya #CRDB ilikosea na kuandika namba ya Simu ya Mteja
Hata hivyo, Kamati ilipotaka kujua kiasi halisi kilichopaswa kuandikwa haikupata maelezo, hivyo kuona dalili za Ubadhirifu na Utakatishaji wa Fedha.
Vilevile, Kamati ya Kudumu ya Bunge la Hesabu za Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imebaini kuwa 2019, 2020 na 2021 watumishi wa Manispaa ya #Kigamboni walifanya marekebisho ya Miamala ya mapato ya Tsh. Bilioni 10.8, bila idhini ya maafisa masuhuli
Aidha, maelezo ya Halmashauri hayakuwekwa bayana ndio maana kamati ikaona kuwa huenda nyuma ya marekebisho hayo kuna nia ovu dhidi ya mapato ya Serikali
Kamati imetoa wito wa Watumishi hao kushughulikiwa kwa mujibu wa #Sheria
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), imebaini Miamala kufutwa au baadhi ya tarakimu kurekebishwa bila idhini ya Maofisa Masuhuli au bila kuwapo kwa nyaraka za Uthibitisho wa uhalali wa marekebisho hayo katika Halmashauri za #Ubungo, #Kigamboni #Ilemela na #Iringa
Mfano; Mnamo 4/09/2019 katika Manispaa ya #Ubungo, Tsh. Milioni 689.3 ziliingizwa katika akaunti ya Manispaa na kutolewa Siku hiyo hiyo kwa madai Benki ya #CRDB ilikosea na kuandika namba ya Simu ya Mteja
Hata hivyo, Kamati ilipotaka kujua kiasi halisi kilichopaswa kuandikwa haikupata maelezo, hivyo kuona dalili za Ubadhirifu na Utakatishaji wa Fedha.
Vilevile, Kamati ya Kudumu ya Bunge la Hesabu za Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imebaini kuwa 2019, 2020 na 2021 watumishi wa Manispaa ya #Kigamboni walifanya marekebisho ya Miamala ya mapato ya Tsh. Bilioni 10.8, bila idhini ya maafisa masuhuli
Aidha, maelezo ya Halmashauri hayakuwekwa bayana ndio maana kamati ikaona kuwa huenda nyuma ya marekebisho hayo kuna nia ovu dhidi ya mapato ya Serikali
Kamati imetoa wito wa Watumishi hao kushughulikiwa kwa mujibu wa #Sheria