Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Fuatilia kinachojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 15, Kikao cha 3, leo Aprili 4, 2024.
NAIBU WAZIRI: SERIKALI INA MKAKATI WA KUPELEKA GESI KATIKA NYUMBA 10,000 ZA DAR
DODOMA: Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Serikali inatarajia kuongeza huduma ya matumizi ya Gesi Hasilia kwa wakazi wa Dar es Salaam na tayari kuna mpango wa kuifikisha katika nyumba 10,000 Jijini hapo.
Ameongeza “Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) imesambaza Miundombinu ya Gesi Hasilia katika nyumba 880 za Dar, imejenga Bomba la Gesi lenye urefu wa Kilometa 12.4 kutoka Mwenge hadi Mbezi Beach kupitia Barabara ya Bagamoyo na tayari viwanda viwili na hoteli sita vimeunganishwa na bomba hilo.”
Ametoa maelezo hayo Bungeni baada ya Mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima kuhoji lini Serikali itaweka Bomba la Gesi kila nyumba kwa Wakazi wa Dar ili Wananchi wapate nishani nafuu.
Esther Bulaya: Serikali inachukua pesa kwenye mifuko ya hifadhi lakini hairejeshi
Esther Bulaya amezungumzia kuwa adha wanayopata wastaafu haswa kwenye janga la kikokotoo, Mahitaji yao ilikuwa kuchukua asilimia 50 kwa mkupuo. Bado kuna mlalamiko kwa madaktari, polisi, hizi ni pesa zao mafao wapate kwa asilimia 50 sio kupewa kwa Mwezi.
Mifuko yetu ina shida, serikali inachukua hela kwenye mifuko kwenye uwekezaji lakini hawalipi, hivyo kufanya mifuko hiyo kutokuwa stable. Tathimini za uwezekezaji hazifanyi vizuri, hiyvo hela hizo zikikopwa kwenye mifuko kwa ajili ya kuwekeza lakini hazina faida za kurudisha pesa hizo katika mifumo hio ya waajiriwa.
NAIBU WAZIRI: SERIKALI INA MKAKATI WA KUPELEKA GESI KATIKA NYUMBA 10,000 ZA DAR
DODOMA: Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Serikali inatarajia kuongeza huduma ya matumizi ya Gesi Hasilia kwa wakazi wa Dar es Salaam na tayari kuna mpango wa kuifikisha katika nyumba 10,000 Jijini hapo.
Ameongeza “Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) imesambaza Miundombinu ya Gesi Hasilia katika nyumba 880 za Dar, imejenga Bomba la Gesi lenye urefu wa Kilometa 12.4 kutoka Mwenge hadi Mbezi Beach kupitia Barabara ya Bagamoyo na tayari viwanda viwili na hoteli sita vimeunganishwa na bomba hilo.”
Ametoa maelezo hayo Bungeni baada ya Mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima kuhoji lini Serikali itaweka Bomba la Gesi kila nyumba kwa Wakazi wa Dar ili Wananchi wapate nishani nafuu.
Esther Bulaya: Serikali inachukua pesa kwenye mifuko ya hifadhi lakini hairejeshi
Esther Bulaya amezungumzia kuwa adha wanayopata wastaafu haswa kwenye janga la kikokotoo, Mahitaji yao ilikuwa kuchukua asilimia 50 kwa mkupuo. Bado kuna mlalamiko kwa madaktari, polisi, hizi ni pesa zao mafao wapate kwa asilimia 50 sio kupewa kwa Mwezi.
Mifuko yetu ina shida, serikali inachukua hela kwenye mifuko kwenye uwekezaji lakini hawalipi, hivyo kufanya mifuko hiyo kutokuwa stable. Tathimini za uwezekezaji hazifanyi vizuri, hiyvo hela hizo zikikopwa kwenye mifuko kwa ajili ya kuwekeza lakini hazina faida za kurudisha pesa hizo katika mifumo hio ya waajiriwa.